Ticker

6/recent/ticker-posts

Chai ya Tanzania, chai bora kuliko zote Duniani



Chai ya Tanzania imetajwa kuwa ni ya kipekee na kwamba hauwezi kuilinganisha na chai yoyote duniani huku upekee wake ukitokana na rangi yake asilia ambayo huwezi kuilinganisha na chai yoyote Duniani na hivyo masoko ya nje yanahitaji chai ya Tanzania ili wachanganye na chai nyingine na wapate rangi.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Angelina Ngalula amesema hayo wakati wa mnada wa kwanza wa Kimataifa wa chai ambao umefanyika kwa mara ya kwanza nchini ukilenga kuongeza thamani ya zao la chai ili kuchangia pato la Taifa, kabla ya hapo mnada huo ulikuwa unafanywa Kenya “Lazima tuilinde chai yetu na tujipongeze kuwa tuna chai nzuri”

Tani 560 sawa na 48% ya chai iliyopelekwa mnadani, imeuzwa kwa wastani wa USD cent 77 kwa kilo ambapo Mgeni rasmi wa mnada ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo,Dkt. Hussein Omar.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa TBT, Mary Kipeja amesema faida za mnada huo ni kuongeza uwazi kwenye soko la chai, kuongeza kipato cha wakulima wa chai ambapo pia Serikali itapata mapato zaidi kupitia bandari za Tanga na Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa ajira kwa Wananchi kama wakulima na wanufaika wa mnyororo wa thamani



Post a Comment

0 Comments