Ticker

6/recent/ticker-posts

Chanzo cha mwanaume kushindwa kurudia tendo



Chanzo cha mwanaume kushindwa kurudia tendo

Baada ya mwanaume kufanya mapenzi na kuridhika awamu ya kwanza huweza kurudia tendo na kuendelea kwenye awamu ya pili, hapo katikati hukutana na kipindi ambacho kitaalam hujulikana kama refractory period

Refractory period: Hiki ni kipindi cha muda baada ya kufika kileleni ambapo mtu hana msisimko wa kufanya tendo.

(the span of time after having an orgasm during which a person is not sexually responsive).

Ukiwa kwenye kipindi hiki huwezi kufanya tena tendo la ndoa,wala kufika kileleni.

Muda wa Kipindi hiki hutofautiana kati ya mtu na mtu, huweza kuchukua dakika chache mpaka hata zaidi ya siku moja,

Ukiwa na afya bora ya mwili kwa ujumla ikiwemo afya ya moyo,kula vizuri,kufanya mazoezi n.k huweza kupunguza muda wa kipindi hiki.

Chanzo cha mwanaume kushindwa kurudia tendo

mwanaume kushindwa kurudia tendo au kushindwa kwenda roundi ya pili,tafsiri yake ni kwamba yupo kwenye kipindi cha refractory period,

Swala la kwamba amekaa muda gani au hali hii imedumu kwa muda gani,kwa lugha nyingine tunaweza kusema refractory period yake imekuwa ya muda mrefu au muda mfupi.

Kumbuka: Kama tulivyosema awali, mtu akiwa kwenye kipindi ambacho hujulikana kama “refractory period”,

hupoteza hisia au hamu ya kufanya tendo tena na wakati mwingine hushindwa kabsa kufanya tendo tena,

huweza kupata shida ya uume kushindwa kusimama tena, na kushindwa kufika kileleni.

Chanzo halisi ya refractory period kuchukua muda mrefu ni nini?

Mpaka sasa hakuna sababu ya moja kwa moja,kwanini baadhi ya watu huwa na kipindi kirefu zaidi “Long refractory period” kuliko wengine,

Ingawa baadhi ya tafiti zimeonyesha vitu vyenye uhusiano wa karibu sana na tatizo hili, vitu hivo ni pamoja na;

1. Mabadiliko ya vichocheo mwilini ikiwemo kichocheo cha Prolactin,

Utafiti wa mwaka 2002 ambao ulifanyika kwa kijana wa kiume mwenye umri wa miaka 25 ulionyesha uhusiano wa karibu kati ya refractory period na uzalishwaji wa vichocheo aina ya prolactin.

Pia utafiti huu ulionyesha kwamba vichocheo vya Prolactin vinaweza kuhusika katika uwezo wa mwanaume kufika kileleni kwa zaidi ya mara moja yaani “multiple orgasms”.

2. Sababu zingine ni pamoja na;

  • Afya ya mtu kwa ujumla ikiwemo; afya ya moyo,mishipa ya damu,usukumaji wa damu,presha ya damu,magonjwa kama kisukari n.k
  • Ubora wa mahusiano husika, je tendo hilo linafanyika kwa mtu unayempenda,unavutiwa naye,unakuwa na hamu naye kila wakati, je hufanyi tendo ukiwa na hasira?, je hampo kwenye ugomvi,migogoro n.k
  • Kuwa na shida ya msongo wa mawazo au Stress
  • Pia mnafanya tendo mara ngapi(frequency of sex), unaweza kuchukua muda mrefu kwenye kipindi cha refractory period ikiwa unafanya tendo mara nyingi zaidi, hii inaweza kusababisha wewe kushindwa kabsa kurudia tendo,kushindwa kufika kileleni,uume kushindwa kabsa kusimama n.k

Zingatia mambo haya ili kukabiliana na tatizo hili;

✓ Hakikisha unafanya mazoezi ya mwili ikiwemo;

  • Kutembea
  • Kukimbia n.k

✓ Hakikisha unazibiti shida ya Uzito mkubwa

✓ Hakikisha unakula mlo kamili,mlo wenye afya, epuka vyakula vya mafuta mengi sana,chumvi nyingi n.k

✓ Kama una magonjwa ya moyo, Ugonjwa kama kisukari,Presha n.k hakikisha unapata tiba

✓ Epuka matumizi ya Pombe kupita kiasi

✓ Epuka uvutaji wa Sigara au kutumia dawa zozote za kulevyia.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

rejea za mada:



Post a Comment

0 Comments