Ticker

6/recent/ticker-posts

Mwanaume mmoja amua mke wa kaka yake na watoto wawili nchini Kenya



Idara ya Upelelezi ya Makosa ya Jinai (DCI) imemkamata mwanaume mwenye umri wa miaka 27, Alex Ayata Migosi, amua mke wa kaka yake mkubwa na watoto wawili katika kijiji cha Mesaria Kaunti ya Kisii, Kenya.

Mshukiwa huyo aliwachinja Edna Moraa Nyairo, 27, na watoto wake wawili, Quinter Kemunto, 4, na Mark Dismas, 3, mnamo Jumanne, Novemba 14, 2023, kutokana na mzozo wa muda mrefu wa familia.

DCI katika taarifa yake Jumatano, ilisema mshukiwa, ambaye alijificha baada ya mauaji hayo alinaswa Jumanne usiku, eneo la Kegogi katika kaunti ndogo ya Marani, Kisii, saa chache baada ya mauaji hayo.

“Muda mfupi kabla ya shambulio la kikatili la mke mwenye umri wa miaka 27 na watoto wake wawili wenye umri wa miaka 4 na 3, majirani waliripotiwa kushuhudia makabiliano makali kati ya mshukiwa wa mauaji na kakake Patrick Omuga kuhusu suala ambalo halijathibitishwa,” ilisema taarifa hiyo.

“Katika azimio la kuchukiza la kusuluhisha matokeo, Ayata aliingia kisiri ndani ya nyumba ya ndugu huyo akiwa na panga, akiwaua kwa uchungu wale watatu waliokuwa wanyonge kwa hofu na shutuma za ujirani.

“Vikosi vya usalama vya eneo hilo vilihamasishwa kumzuia mhalifu kabla hajaondoka mkoani humo, juhudi ambazo zilizaa matunda jana usiku. Kwa sasa anashughulikiwa kwa ajili ya kusomewa mashitaka.”

Miili ya waathiriwa ilipelekwa katika hifadhi ya maiti ya Hospitali ya Rufaa ya Kisii.



Post a Comment

0 Comments