Ticker

6/recent/ticker-posts

TANZIA: Askofu Erasto Kweka afariki dunia



Askofu Mstaafu wa Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Erasto Kweka amefariki dunia Novemba 25, 2023, kweye Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), alilokuwa anapatiwa matibabu.

Katibu Mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa hilo, Zebadiah Moshi kupitia taarifa yake aliyoitoa leo, amethibitisha kutokea kwa kifo hicho na kueleza kuwa, Dk Kweka amekuwa kiongozi wa Dayosisi ya Kaskazini toka mwaka 1976 mpaka 2004 alipostaafu.

“Uongozi wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini una masikitiko makubwa kutangaza kutwaliwa kwa baba Askofu Mstaafu Dk Erasto Kweka, kifo kimetokea leo, Novemba 25, 2023 saa nne asubuhi katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI),” imeeleza taarifa hiyo.



Post a Comment

0 Comments