Ticker

6/recent/ticker-posts

UWT tunampongeza Rais Samia kwa kutengua uteuzi wa Gekul, uchunguzi ukamilike kwa haraka



Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM Tanzania (UWT), Mary Chatanda amesema Umoja huo umepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za tuhuma zinazomkabili Mbunge wa Babati Mjini Pauline Gekul kuhusu kumfanyia ukatili Kijana Hashim Ally Babati Mjini Mkoani Manyara ambapo wamesema ikithibitika ametenda kosa hilo achukuliwe hatua kali.

“UWT tunazunguka nchi nzima kupinga na kukemea ukatili wa kijinsia na kuporomoka kwa maadili, hivyo tunapinga vikali kitendo hiki na endapo tuhuma hizi za Gekul zitathibitika hatua stahiki zichukuliwe na adhabu kali itolewe dhidi yake, UWT haitovumilia Kiongozi yoyote Mwanamke atakayethibitika anafanya vitendo vya ukatili wa kijinsia.

“UWT tunampongeza Rais Samia kwa kutengua uteuzi wa Gekul kama Naibu Waziri wa Katiba na Sheria na tunaviomba Vyombo vya Dola kukamilisha uchunguzi kwa haraka ili kuleta imani kwa Wananchi.”



Post a Comment

0 Comments