Ticker

6/recent/ticker-posts

Mlipuko waua watu 8 na kujeruhi 84 Guinea



Mlipuko waua watu 8 na kujeruhi 84 Guinea

Takriban watu wanane wameuawa na wengine 84 wamejeruhiwa kufuatia mripuko mapema leo katika bohari ya mafuta katika mji mkuu wa Guinea, Conakry.

Takriban watu wanane wameuawa na wengine 84 wamejeruhiwa kufuatia mripuko mapema leo katika bohari ya mafuta katika mji mkuu wa Guinea, Conakry. Hayo yameelezwa na afisa mkuu wa polisi nchini humo ambaye amesema idadi hiyo ni ya muda na kwamba moto huo umedhibitiwa.

Mlipuko katika bohari pekee ya mafuta katika taifa hilo la Afrika Magharibi, ulitikisa wilaya ya Kaloum katikati mwa jiji la Conakry, na kuwalazimisha mamia ya watu kulikimbia eneo hilo.

Moto mkubwa na moshi mweusi vilishuhudiwa hadi kwa umbali wa kilometa kadhaa huku vikosi vya zima moto vikiwasili na malori ya mafuta yakiondoka eneo hilo yakisindikizwa na polisi. Serikali ya Guinea imewataka raia wa mji mkuu kusalia majumbani mwao.



Post a Comment

0 Comments