Ticker

6/recent/ticker-posts

AFCON: Mashabiki wa Ivory Coast wenye hasira wameharibu mabasi baada ya kufungwa bao 4 - 0 na Equatorial Guinea



AFCON: Mashabiki wa Ivory Coast wenye hasira wameharibu mabasi baada ya kufungwa bao 4 – 0 na Equatorial Guinea

Mashabiki wa Ivory Coast waliokuwa na hasira waliharibu mabasi kadhaa baada ya taifa mwenyeji (Ivory Coast) kupata kipigo kikali zaidi katika Kombe la Mataifa ya Afrika 2023 nchini Ivory Coast.

Ivory Coast ilichapwa mabao 4 – 0 kwenye ardhi yao ya nyumbani katika mechi ya mwisho ya hatua ya makundi Jumatatu, Januari 22.

Baada ya mchezo huo mashabiki waliokuwa na hasira walieleza machungu yao kwa kuharibu mabasi kadhaa nje ya uwanja.

Hata hivyo, Ivory Coast ina fursa ya kufuzu kwa hatua ya 16 bora kupitia njia ya wapotezaji bora ili kusalia kwenye kinyang’anyiro hicho.

Katika kundi A, Equatorial Guinea inaongoza kundi hilo ikiwa na pointi saba sawa na Nigeria lakini wanamaliza wakiwa kileleni mwa kundi hilo wakiwa na mabao saba.



Post a Comment

0 Comments