Connect with us

Magonjwa

Kukosa usingizi husababishwa na nini?

Avatar photo

Published

on

Kukosa usingizi husababishwa na nini?

Mtu mwenye afya bora hupaswa kupata usingizi wa kutosha ili kuweza kukua katika afya bora,Lakini kwa baadhi ya watu suala la kupata usingizi limekuwa ni tatizo la mda mrefu na lenye kuwatesa sana.

Tatizo hili la kukosa Usingizi kwa kitaalam hujilikana kama “Insomnia”.

Wengi wamekuwa wakikosa usingizi kabsa, na baadhi yao huupata usingizi lakini katikati ya usiku au wakati wakiwa wamelala hushtuka na mala washtukapo hukosa usingizi mpaka kuna kucha.

Matatizo haya hutokana na sababu mbalimbali za kiafya..kiakili..kimwili na hata kwa baadhi ya tabia za mhusika mwenyewe.

Kukosa usingizi husababishwa na nini?

Zipo sababu mbalimbali ambazo huchangia mtu kukosa usingizi kama vile;

  • Msongo wa mawazo/hofu ya jambo fulani
  • Matumizi ya dawa za kulevya,kahawa,nikotini, n.k
  • Mazingira mabovu ya kulala n.k
  • Pamoja na Sababu nyingine nyingi…!!!!

Kwa kawaida mtu mzima mwenye afya bora na asiye na matatizo yoyote hupaswa kupata usingizi kwa mda wa masaa 7-8.

• Soma Zaidi muda Sahihi wa Kulala kiafya(Masaa ya kulala)

Tumezoea mara nyingi kwamba Mtu anapaswa kulala wakati wa Usiku(ni sahihi kabsa na kiafya inashauriwa Zaidi hivi),

ingawa kuna baadhi ya watu hulala mchana tu na usiku hawalali,hali hii kiafya haishauriwi sana kwani hudumaza ubongo na kusababisha msongo wa mawazo.

MADHARA YA KUKOSA USINGIZI

> Kupata msongo wa mawazo na kuwa na hali ya uchovu kila wakati

> Akili kuchoka na kutoweza kufanya kazi kwa ufanisi mzuri zaidi

>Kupata maumivu ya mwili na pia mwili kuwa na homa za mara kwa mara

> kuanza kupata shida ya kusahau sahau vitu(Kupoteza kumbukumbu) n.k

TIBA ya Kukosa Usingizi

Mara nyingi tiba ya tatizo hili imekuwa ni Matumizi ya dawa mbali mbali za kuleta usingizi ambazo zimetengenezwa kwa kemikali mbalimbali,

kemikali hizi zimekuwa ni chanzo kingine cha kusababisha magonjwa ya akili na pia matatizo ya ubongo.

Ni muhimu sana kutafta chanzo cha kukosa Usingizi na kutumia njia mbadala za kukusaidia kupata Usingizi.

Fahamu njia/Tiba hizo za Asili za kukusaidia kupata Usingizi, Soma Zaidi hapa(Usingizi tips)

MAMBO 10 YA KUKUSAIDIA KULALA KAMA UNA TATIZO LA KUKOSA USINGIZI USIKU.

Inawezekana wewe ni moja kati ya ambao wamewahi kuwa na tatizo la kukosa usingizi wakati wa usiku(INSOMNIA),

Hii huwa ni hali ambayo mara nyingi inasumbua na kukera hususani kama mtu umechoka.

MAMBO YA KUZINGATIA kama unatatizo la Kukosa Usingizi

1. Fanya mazoezi wakati wa mchana

2. Kuwa na muda binafsi na tafakari ilivyokuwa siku yako;

Kabla ya kulala pia inashauriwa kupata muda binafsi ili kutafakari yaliyotokea kwa siku hiyo na jinsi siku inayofuata inaweza kuwa nzuri na ya mafanikio.

3. Fanya Sala;

Inashauriwa pia kwa dini na imani yoyote, kufanya ibada au sala kunasaidia akili ku relax na kufanya usingizi uje na unaweza kulala kwa amani.

4. Soma kidogo vitu chanya.

5. Kuwa na ratiba maalumu ya kulala;

Hii pia itasaidia kulala bila shida kwa wakati uliozoea.

6. Chunga tabia yako ya kulala;

Ni muhimu sana kuzingatia, kuachana na vitu vinavyoweza kusababisha tatizo la kushindwa kulala wakati wa usiku ikiwa ni pamoja na kulala wakati wa jioni jambo linaloweza kukata usingizi pindi muda wa kulala unapofika wakati wa usiku.

7. Acha kuangalia TV nyakati za usiku sana;

Pia ni muhimu kuachana na tabia ya kukaa macho na kuangalia TV nyakati za usiku sana kwani mwili hujijengea kutolala wakati huo unapofika kwani huwa ni muda ambao kwa kawaida unakuwa unaangalia TV.

Soma Zaidi hapa Madhara ya kuangalia TV au kutumia Simu nyakati za usiku sana;

8. Chunga unachokula au kunywa kabla ya kulala;

 Inashauriwa kuepuka kunywa kahawa au pombe kabla ya kwenda kulala kwa sababu ni vitu ambavyo vinachukua muda mrefu kuyeyushwa tumboni.

Vitu hivi pia ni chanzo kikubwa cha Mtu kukosa Usingizi.

9. Andaa mazingira mazuri ya kulala;

Kulala kwenye mazingira mazuri ni muhimu. Inashauriwa kulalia mashuka masafi na mito misafi, huku eneo zima kama chumbani liwe safi lisilo na vumbi wala harufu.

10. Tumia choo kabla hujalala;

Baadhi ya watu hupoteza kabisa usingizi na kushindwa kuupata tena pindi wanapoamka usiku ili kwenda chooni au kwa sababu nyingine zozote. Kwa mantiki hiyo wataalamu wanashauri ni vyema kwenda haja kabla ya kwenda kulala ili kwamba mwili usisumbuliwe wakati umelala.

 FAIDA ZA USINGIZI PAMOJA NA NJIA 13 ZA KUPATA USINGIZI MZURI

Japokuwa kadri umri unavyokuwa Mkubwa ndivo masaa ya kulala hupungua,ila bado umuhimu wa kulala vizuri ni Mkubwa sana, Tafiti Zinaonyesha Mtu anayepata usingizi au anayelala vizuri,Mfano kwa Mtu Mzima wastani wa masaa 8 yanatosha kabsa,Humsaidia sana katika vitu vitu mbali mbali.

SUMMARY:

Katika Sehemu hii tunajadili Faida za kupata Usingizi Mzuri na Njia 13 za kukusaidia wewe mwenye matatizo ya kukosa usingizi kila siku,kutatua tatizo hili kwa haraka sana.Na kuendelea kufurahia Maisha.

Baadhi ya Faida za kupata Usingizi Mzuri ni pamoja na hizi hapa;

âś“ Kuimarisha Kinga yako ya Mwili

âś“ Kuongeza Uwezo wako wa akili pamoja na uwezo wako wa Kufikiri Vizuri

âś“ Huondoa uchovu wa Mwili pamoja na kuupa mwili Nguvu ya Kutosha

âś“ Husababisha Ngozi ya mwili kunawiri pamoja na afya ya seli hai za mwili

âś“ kuboresha afya ya Ubongo na uwezo wa kukumbuka n.k

NJIA 12 ZA KUKUSAIDIA KUPATA USINGIZI MZURI

Zifuatazo ni Njia ambazo zitakusaidia wewe kwa kiasi kikubwa kupata Usingizi mzuri na kuleta Nguvu na si uchovu katika Mwili wako;

1. Punguza Matumizi ya vitu vyenye mwanga wa Blue wakati wa siku,kama vile kwenye Taa au simu,Tv, Computer n.k.

Tafiti zinaonyesha kwamba mwanga wa Blue hupunguza uzalishaji wa Homoni au kichocheo aina Ya Melatonin ambacho ndyo huhusika na kuleta Usingizi.

2. Kaa kwenye Mwanga wa Kutosha wakati wa Mchana,

Hii husaidia mwili wako kuweza kutofautisha wakati wa usiku ni upi na wakati wa Mchana ni upi,hivo kukusaidia wewe kupata usingizi mzuri wakati wa usku.

3. Epuka Matumizi ya Vinywaji vyenye Caffeine hasa wakati wa Usiku,

kwani vinywaji kama hivi huuchangamsha mwili wako na kukusababishia kukosa Usingizi kabsa wakati wa Usku. Hivo epuka matumizi haya ya Vinywaji vyenye Caffeine wakati wa Usku.

4. Punguza tabia ya kulala wakati wa mchana,hii itakusaidia wewe kulala vizuri wakati wa Usku.

Inashauriwa kwa asilimia kubwa muda wa kulala na kumka kila siku uzingatiwe sana,hali hii huuzoesha mwili kwamba sasa ni wakati wa usku na ni wakati wangu wa kulala.

5. Epuka matumizi ya pombe au kilevi chochote,kwani hivi huathiri uzalishaji wa kichocheo au homoni hii ya Melatonin ambayo inahusika na Usingizi moja kwa moja.

6. Boresha Mazingira yako ya kulala,

Tafiti zinaonyesha watu wengi wanaosumbuliwa na matatizo ya kukosa Usingizi, hulala kwenye vyumba ambavyo si rafiki,

mfano; Chumba ambacho kina mwanga sana,chumba chenye Joto sana,Chumba chenye baridi sana,Chumba ambacho kina makelele ya aina yoyote,mfano Redio au watu.n.k

7. Epuka matumizi au ulaji mwingi wa chakula wakati wa usiku,pia Epuka kula vyakula vizito sana wakati wa Usku.

8. Pumzisha akili yako na iburudishe na vitu  kama Mziki laini n.k kabla Ya kulala na epuka kutazama vitu kama Movies ndefu za kutisha wakati wa usku.

9. Hakikisha umeoga kabla ya kwenda kulala Au kuupumzisha mwili wako kitandani.

10. Tumia godoro zuri na mto safi kama wewe ni mpenzi wa mto wakati wa kulala, Kulala chini au kwenye kamba n.k,ni ngumu sana kupata usingizi mzuri

11. Fanya mazoezi kila siku wakati wa mchana kabla siku yako haijaisha au kabla hujaenda kulala kitandani.

12. Epuka kunywa kwa wingi vimiminika,kwani vitakufanya uanze kuamka amka mara kwa mara wakati wa usku,hivo kupelekea kukosa usingizi mzuri.

NA KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Ushauri|Tiba|CheckIn 🩺🌡️ContactUs; +255758286584 or INBOX📩. For More Healthtips everyday Link In https://afyaclass.com Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...