Ticker

6/recent/ticker-posts

Mbinu za jinsi ya kupunguza tumbo kwa haraka



Mbinu za jinsi ya kupunguza tumbo kwa haraka

Kila mtu ana mafuta tumboni(belly fat),hata watu ambao wana tumbo dogo,Hiyo ni kawaida. Lakini ukiwa na mafuta mengi ya tumbo yanaweza kuathiri afya yako kwa njia ambayo mafuta mengine hayaathiri.

Baadhi ya mafuta yako yanahifadhiwa chini ya ngozi yako. Mafuta mengine huhifadhiwa ndani zaidi, karibu na moyo wako, mapafu, ini, na viungo vingine.

Sasa basi,mafuta yale ambayo huhifadhiwa ndani zaidi — yanayoitwa “visceral” fat — ndyo ambayo yanaweza kuwa tatizo kubwa, hata kwa watu wembamba.

Fahamu kama una mafuta mengi mno ya aina hii(Visceral fat), huenda ukaweza kupata matatizo mbali mbali ya kiafya kama vile;

Katika Makala hii tunaeleza madhara ya kuwa na tumbo kubwa(mafuta mengi tumboni), lakini baada ya madhara hayo,hizi ni mbinu muhimu za kukusaidia kukabiliana na tatizo hili.

jinsi ya kupunguza tumbo

1. Fanya Mazoezi ya mwili

Kufanya mazoezi ya mwili husaidia kupunguza mafuta mwilini yakiwemo Visceral fat.

Unashauriwa kufanya mazoezi angalau kwa dakika 30, kwa muda wa angalau siku 5 za wiki,

Fanya Mazoezi mbali mbali kama vile kuruka kamba,kutembea n.k

Pata Zaidi hapa: Maelekezo kamili ya Mazoezi kwa Ajili ya kukusaidia kupunguza Uzito wako pamoja na Tumbo kwa ujumla

2. Aina ya chakula unachokula(Diet):

Kula vyakula vyenye kiwango kikubwa cha nyuzinyuzi(fibers),

Na tafiti zinaonyesha,unapopanga Diet yako kwa ajili ya kupunguza Uzito, Moja ya vitu ambavyo ni vyakwanza kabsa kupungua ni pamoja na mafuta ya Tumbo(belly fat).

Pata Zaidi hapa: Full diet plan kwa Ajili ya kukusaidia kupunguza Uzito wako pamoja na Tumbo kwa ujumla

3. lala kwa muda Sahihi

Kupata kiwango sahihi cha usingizi husaidia kupunguza matatizo mengi ikiwemo hili la tumbo na Uzito wa mwili kwa ujumla.

Katika utafiti mmoja, watu waliopata usingizi na kulala muda wa saa 6 hadi 7 kwa usiku walipata mafuta kidogo ya visceral kwa miaka 5 ikilinganishwa na wale waliolala masaa 5 au machache kwa usiku au waliolala masaa 8 au zaidi kwa usiku.

Kulala kunaweza kuwa jambo pekee ambalo lina muhimu mkubwa katika afya ya binadamu.

Soma Zaidi hapa: Faida za kupata muda wa kutosha wa kulala

4. Msongo wa mawazo au Stress:

Kila mtu ana stress, ila Jinsi unavyoshughulikia stress ni muhimu, je,ukiwa katika hali ya Msongo wa mawazo au Stress ni njia gani unatumia ili kukabiliana na tatizo hili?

Mambo bora zaidi unayoweza kufanya ni pamoja na kupumzika na marafiki na familia, kutafakari, kufanya mazoezi ya kupumua, na kupata ushauri n.k Hiyo itakusaidia kuwa na afya njema na kufanya maamuzi mazuri.

Wapo baadhi ya watu wakiwa kwenye hali ya Stress hula Zaidi, sababu inayofanya ongezeko la mafuta tumboni kwa haraka, hivo,kudhibiti unachokula huweza kusaidia kupungua ukiwa katika hali hii.

Ingawa pia,wapo watu wakiwa kwenye hali ya Stress hawawezi kula kabsa.

JINSI YA KUPUNGUZA TUMBO(afyatips)

Kwa hivi sasa watu wengi hupambana na njia mbali mbali za kupunguza matumbo yao hasa wadada ili kuonekana warembo zaidi, na kuvaa nguo ipendeze, Hivo basi huwapelekea kutumia njia mbali mbali ili kupunguza tumbo, huku zingine zikiwa sahihi na zingine zikiwa hatari zaidi kwa afya zao. Hapa kuna baadhi ya mambo ya kuzingatia wakati unahitaji kupunguza tumbo lako,

1. Hakikisha unapendelea zaidi kula vyakula pamoja na matunda yenye nyuzi nyuzi au Fibers kama vile machungwa,maembe,maparachichi n.k

2. Epuka kula vyakula vyenye mafuta zaidi ikiwemo chips

3. Epuka matumizi ya pombe kupita kiasi

4. Kula vyakula vyenye kiwango kikubwa cha PROTEIN na sio kiwango kikubwa cha MAFUTA mfano; Maharage n.k

5. Punguza au epuka kabsa kuwa na msongo wa mawazo,watu wengi hawajui kwamba msongo wa mawazo huweza kusababisha tatizo la kuongezeka kwa tumbo au hata uzito kwa baadhi ya watu

6. Epuka kula vyakula vyenye kiwango kikubwa cha sukari

7. Fanya mazoezi ya mwili kila siku,angalau kwa dakika 30 au Nusu saa kila siku

8. Hakikisha unapata muda wa kutosha wa kupumzika pamoja na kulala

9. Unaweza kupendelea kula vyakula jamii ya samaki zaidi huku ukiepuka mafuta mengi

10. Japo juice za matunda ni nzuri sana, ila baadhi zina kiwango kikubwa sana cha sukari,hivo epuka juice kama hizi

11. Kunywa chai ya kijani maarufu kama GREEN TEA, najua wengi wenu hamjawahi kusikia hii,ila ipo na watu wanaitumia hivo ulizia itakusaidia pia.

12. Pamoja na Tips zingine za Afya

KUMBUKA; kufunga mkanda tumboni ili tumbo lipungue au kushinda na njaa kila siku huweza kuwa hatari kwako na sio njia salama ya kupunguza tumbo

• Soma pia: Jinsi ya Kupunguza Uzito wa Mwili

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Post a Comment

0 Comments