Ticker

6/recent/ticker-posts

Fahamu ukweli, hatari na matibabu ya Vichwa vikubwa



Fahamu ukweli, hatari na matibabu ya Vichwa vikubwa

Kichwa kikubwa ni ugonjwa wa watoto wachanga wa kutanuka chemba za maji za kichwani na hivyo kupeleka muonekano wa kichwa kuwa mkubwa. Ugonjwa huu ni matokeo ya kuzalishwa kwa maji mengi kichwani ama kuziba kwa njia za kupitisha/kufyonzwa maji hayo.

Hutokana na sababu za kinasaba, hivyo mtoto kuzaliwa na kichwa kikubwa. Aina hii huambatana na matatizo mengine kama vile mgongo wazi (SPINE BIFIDA) na mguu kifundo (TALIPES). Sababu nyingine ni maambukizi ya mishipa ya fahamu pindi mtoto anapozaliwa au mara tuu baada ya kuzaliwa.

Ukweli kuhusu kichwa kikubwa 

  • Asilimia 50 ya watoto wa kichwa kikubwa huwa na changamoto ya ukuaji.
  • Kuanza matibabu mapema baada ya mtoto kuzaliwa hupunguza changamoto hizi za ukuaji.

Vihatarishi vyake

  • Ukosefu wa virutubisho (vitamins) aina ya folic acid wakati wa ujauzito.
  • Unywaji holela wa baadhi ya dawa za hospitali wakati wa ujauzito.
  • Ajali, hususani kwa watu wazima
  • BAADHI YA WATU WALIOZIDI MIAKA 60 (NORMAL PRESSURE HYDROCEPHALUS)

Dalili zake

Kwa watoto wachanga chini ya umri wa mwaka 1

  • Kulialia hovyo
  • Kushindwa kunyonya au kula vizuri.
  • Kuchelewa kukaza shingo
  • Kuvimba/kujaa utosi

Kwa watoto wakubwa na WATU WAZIMA

  • Kichwa kuuma
  • Kichefuchefu na kutapika
  • Matatizo ya kuona, kutembea, balance
  • Macho kuzama chini kamaa jua linalokuchwa

Matibabu yake

  • Kuwekewa mirija maalum ya kutoa maji (shunt)
  • Njia ya kisasa ya matundu (ETV)

Via:DR JUMA MAGOGO

>> Soma Zaidi tatizo la vichwa vikubwa au mtoto kuzaliwa na Kichwa kikubwa

>>Soma Zaidi kuhusu Faida za Vidonge vya Kuongeza Damu

>>Soma Zaidi tatizo la mgongo wazi (SPINE BIFIDA) 



Post a Comment

0 Comments