Ticker

6/recent/ticker-posts

Ripoti:Visa vya unene wa kupindukia vimeongezeka kutoka asilimia 17 hadi 26 nchini Uganda



Ripoti:Visa vya unene wa kupindukia vimeongezeka kutoka asilimia 17 hadi 26 nchini Uganda

Kampala, Uganda

SikiaHii: Serikali ya Uganda imewahimiza watumishi wote wa umma kufanya mazoezi kwa angalau saa mbili kwa wiki kama sehemu ya kuimarisha afya zao.

Wito huo umetolewa baada ya ripoti ya afya kuonyesha kuwa visa ya unene wa kupindukia vimeongezeka kutoka asilimia 17 hadi 26 katika muda wa miaka 17 iliyopita.

Kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter, serikali ya Uganda imesema mazoezi ya watumishi wa umma yatasaidia kukabiliana na tatizo hilo la unene wa kupindukia.

Je, unafanya mazoezi mara ngapi kwa wiki? ?️‍♀️

Via:@dw_kiswahili

>>Soma Zaidi hapa kuhusu tatizo la Unene na jinsi ya kukabiliana nalo



Post a Comment

0 Comments