Magonjwa
Haya hapa ni Madhara ya Kuwa na Uzito Mkubwa(Overweight)
Haya hapa ni Madhara ya Kuwa na Uzito Mkubwa(Overweight,Obesity),
Katika makala hii tumechambua baadhi ya madhara ambayo huweza kukupata kama una tatizo la Uzito mkubwa au Uzito kupita kiasi(Overweight/Obesity)
1. Kuwa kwenye hatari ya Kupatwa na Ugonjwa wa Presha(High blood pressure),
Hali ambayo pia huweza kusababisha madhara mengine kama vile;stroke n k
2.Tatizo la Kiharusi au STROKE
3. Kuwa kwenye hatari ya kupatwa na shambulio la Moyo(Heart attack),
Hii huweza kuchangiwa kwa kiasi kikubwa na shida ya high blood pressure,Cholestrol pamoja na blood sugar
4. Kuwa kwenye hatari ya kupatwa na magonjwa ya Ini ikiwemo Ini kushindwa kufanya kazi(Liver failure), hasa kutokana na kujengwa kwa Mafuta mengi(Excess fat) kwenye eneo hili
5. Kuwa kwenye hatari ya kupatwa na Saratani mbali mbali ikwemo; Saratani ya Ini,Figo,Utumbo mpana pamoja na kongosho
6.Kuwa kwenye hatari ya kupatwa na shida ya mawe kwenye figo, mawe kwenye vifuko vya nyongo(Gallstones) n.k
7. Kuwa kwenye hatari ya kupata Ugonjwa wa Kisukari hasa Type 2 Diabetes, kutokana na Mwili kukinzana na Insulin
8. Misuli na mifupa ya mwili kuwa dhaifu na kuvunjika kwa haraka kutokana na kulemewa zaidi
9. Kuwa kwenye hatari ya kupatwa na tatizo la Acid reflux au Gastroesophageal reflux disease-GERD
10. kuwa kwenye hatari ya Figo kushindwa kufanya kazi(Kidney failure)
11. kupatwa na maumivu ya mgongo,kiuno,misuli pamoja na joints
12. Kuwa kwenye hatari ya kupoteza uwezo wa kuzaa au kuzalisha(Infertility) n.k
BOFYA HAPA: Kupata Ebook ya kukusaidia Kupunguza Uzito wako hata Ukiwa Nyumbani kwako