Ticker

6/recent/ticker-posts

Jinsi ya Kupunguza Uzito kwa Ufanisi: Mbinu Rahisi Zaidi



Jinsi ya Kupunguza Uzito kwa Ufanisi: Mbinu Rahisi Zaidi

Linapokuja Swala la Uzito,Zipo Makala nyingi na njia nyingi Sana utazikuta mtandaoni zinazohusu kupunguza Uzito, Je zinafanya kazi? na je hazina madhara yeyote?

Kwanza,Ili ujue Una Uzito Mkubwa kupita kiasi ni Lazima upime, na Vipimo vinategemea na nchi au Mahali Ulipo,Kitaalam ukienda kwa ajili ya Checkup za aina hii vitu hivi huweza kufanyika;

  • Kupata historia ya afya yako kwa Ujumla, ikiwemo historia ya uzito wako,njia ulizowahi kutumia kupunguza uzito,aina ya kazi unayofanya,mazoezi,historia ya watu kuwa na Uzito mkubwa kwenye familia yako n.k
  • Vipimo muhimu kama vile,Uzito wako,Urefu wako,Mapigo ya Moyo,Presha,afya ya moyo,mapafu n.k
  • Baada ya Vipimo hivi tunafanya mahesabu ya BMI, Hii sasa ndyo itakuambia Uzito wako umezidi,upo kawaida,au mdogo sana.

#SOMA KWA kina Hapa,Jinsi ya kufanya mahesabu ya BMI,

Baada ya kufanya vyote hivo na Kujua Una shida ya Uzito mkubwa(Overweight), Hapa ndyo tunakuja na njia za jinsi ya kupunguza Uzito wako wa mwili;

Jinsi ya Kupunguza Uzito kwa Ufanisi: Mbinu Rahisi Zaidi

Hapa kuna Vidokezo rahisi vya kufuata,Ingawa tumekuandalia kitabu mfumo wa ebook ambacho ukikipata utafuata hatua Zote kwa Kina na kupunguza Uzito hata ukiwa mwenyewe nyumbani. Kukipata Bofya Hapa.

1. Badilisha aina ya Mlo unaokula

Tafiti zinaonyesha kupunguza kiwango cha calories na kula mlo unaotakiwa kiafya ni NJIA KUU ya kukabiliana na tatizo la Uzito Mkubwa.

Punguza kalori; Njia kubwa ya kupunguza uzito ni kupunguza kalori,Hatua ya kwanza ni kukagua tabia zako za kawaida za kula na kunywa.

Unaweza kuona ni kalori ngapi unazotumia kwa kawaida na wapi unaweza kupunguza. Wewe na mtaalamu wako wa afya mnaweza kuamua ni kalori ngapi unazohitaji kutumia kila siku ili kupunguza uzito. Kiasi cha kawaida ni kalori 1,200 hadi 1,500 kwa wanawake na 1,500 hadi 1,800 kwa wanaume.

Fanya chaguzi bora la Mlo kwa Afya; Unashauriwa kula vyakula vya mimea zaidi yaani plant-based foods. Hapa ni pamoja na MATUNDA,MBOGA ZA MAJANI pamoja na Nafaka nzima,

Pia unashauriwa kula vyanzo bora vya proteins kama vile maharage,soya,nyama,samaki n.k kwa kiwango kidogo.

Dhibiti Matumizi ya chumvi nyingi,Sukari nyingi au Mafuta mengi

Epuka kula vyakula vyenye kiwango kikubwa cha Wanga, vyakula vya Mafuta mengi sana, au Vinywaji vyenye kiwango kikubwa  cha Sukari kama POMBE n.k.

2. Fanya Mazoezi ya Mwili,

Baadhi ya Tafiti zinaonyesha Mtu mwenye Uzito Mkubwa anatakiwa kufanya Mazoezi angalau kwa dakika 150 ndani ya wiki Moja,

Hii inaweza kusaidia kuzuia kupata uzito zaidi au kudumisha upotezaji wa uzito wa kawaida. Pengine utahitaji kuongeza hatua kwa hatua kiasi unachofanya mazoezi kadri ustahimilivu wako unavyoboreka.

3. Mabadiliko ya Kitabia ikiwemo Msongo wa Mawazo

Hapa unaangalia ni vitu gani vinakusababishia Uzito wako kuongezeka,kisha unavibadilisha,

Watu wengi hawafahamu Msongo wa mawazo huweza kusababisha baadhi ya Watu Uzito wao wa mwili kuongezeka kwa kasi sana

#SOMA ZAIDI hapa madhara ya Msongo wa mawazo(Stress)

4. Pata Ushauri kutoka kwa Wataalam

Hii ni hatua muhimu sana,kwani huwezi kupunguza kitu ambacho hukijui,

Hakikisha unapata Maelekezo kutokwa kwa Wataalam au

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU NA TIBA TUWASILIANE NDANI YA AFYACLASS,HIZI HAPA NI NJIA ZA MAWASILIANO



Post a Comment

0 Comments