Ticker

6/recent/ticker-posts

Ni kwanini Wanaume hawawezi kupata Ugonjwa wa PID kama Wanawake?



Ni kwanini Wanaume hawawezi kupata Ugonjwa wa PID kama Wanawake?

Hapana, Mwanaume hawezi kuwa na Ugonjwa wa PID(Pelvic inflammatory disease),

Hii ni kwa Sababu PID ni ugonjwa ambayo huhusisha maambukizi ya vimelea vya magonjwa kama vile bacteria kwenye Via vya Uzazi vya Mwanamke.

Kwa Ujumla,Ugonjwa huu wa PID hushambulia mfumo wa Uzazi kwa mwanamke, ikiwa ni Pamoja na;

(1) Kizazi(Uterus)

(2) Mirija ya uzazi(fallopian tubes)

(3) au Vifuko vya Mayai(Ovaries)

Ingawa Wanaume hawawezi kupata PID lakini wanaweza kuwa carriers wa bacteria wanaosababisha Ugonjwa wa PID,

Hii inaweza kusababisha Mwanamke kuwa na maambukizi ya PID ambayo hujirudia rudia endapo mwanaume ambaye hushiriki naye tendo hakupata msaada wowote wa Matibabu.

Hivo basi kama Mwanamke ana PID ni vizuri yeye na mwenza wake kupata Tiba ili kuepuka tatizo hili kujirudia mara kwa mara.

SOMA Zaidi hapa,LINK IN HERE



Post a Comment

0 Comments