Ticker

6/recent/ticker-posts

Ugonjwa Wa Zika,Chanzo,Dalili Na Tiba Yake



UGONJWA WA ZIKA,CHANZO,DALILI NA TIBA YAKE

Ugonjwa wa Zika ni ugonjwa ambao husababishwa na Virusi na kusambazwa na mbu aina ya Aedes mosquitoes ambao kwa asilimia kubwa humuuma mtu wakati wa asubuh sana,mchana au jioni,

Mbu huyu aina ya Aedes mosquitoes ndyo huyo huyo ambaye huweza kusambaza ugonjwa wa DENGUE,CHIKUNGUNYA,Pamoja na YELLOW FEVER.

Japo pia watu wengi wenye maambukizi ya virusi wa Zika hawaonyeshi dalili zozote,

DALILI ZA UGONJWA WA ZIKA NI PAMOJA NA;

- Joto la mwili kuwa juu sana au mtu kuwa na homa

- Mtu kupata rashes kwenye ngozi ya mwili wake

- Mtu kupata tatizo la macho kuvimba kwenye conjactiva hali ambayo kwa kitaalam hujulikana kama Conjuctivitis

- Mtu Kupata shida ya maumivu kwenye misuli pamoja na maumivu ya joint

- Mtu kupata maumivu ya kichwa cha mara kwa mara

- Mtu kupata uchovu wa mwili kupita kiasi n.k

VIPIMO VYA UGONJWA WA ZIKA NI PAMOJA NA

• Mtu kuchunguzwa dalili za ugonjwa kwa kuulizwa maswali,kuangaliwa na kuchukua histori ya ugonjwa kutoka kwa mgonjwa mwenyewe

• Pamoja na vipimo vya maabara yaani laboratory tests vinavyohusu kuchukua Sample ya Damu,mkojo,jasho,mate au maji maji ya aina yoyote kutoka kwenye mwili wa mgonjwa,

hii ndyo comfirmatory test,vipimo hivi ndyo hutoa uthibitisho kamili kama mgonjwa ana ugonjwa wa zika au hana

MADHARA YA UGONJWA WA ZIKA NI PAMOJA NA

- Mashambulizi ya virus wa zika huweza kumpata mama mjamzito kisha kuleta madhara mbali mbali kama vile;

• Mtoto kuzaliwa na kichwa kidogo kuliko kawaida yaani Microcephaly pamoja na matatizo mengine ambapo kwa kitaalam hujulikana kama Congenital Zika Syndrome

• Pia huweza kuleta madhara wakati wa ujauzito kama vile; ujauzito kuharibika wenyewe(miscarriage) au mama kujifungua mtoto kabla ya wakati yaani preterm birth

- Pia ugonjwa wa zika huweza kusababisha matatizo kwenye mfumo wa Nerves(Neurologic disorder) kwa Watu wazima na watoto ikiwemo tatizo la; Neuropathy pamoja na myelitis

MATIBABU YA UGONJWA WA ZIKA

✓ Kama ilivyo kwa magonjwa mengi ambayo chanzo chake ni virusi, Hakuna matibabu ya moja kwa moja ya kutibu kabsa au kuondoa kabsa kirusi hiki,

ila kuna matibabu yanayohusu kudhibiti dalili mbali mbali ambazo husababishwa na kirusi hiki kwenye mwili wako, kama vile homa,maumivu ya misuli,joints n.k

Pia kwa wale watu ambao wapo kwenye ukanda ambao kuna Mbu sana wanashauriwa kujikinga na mbu kwa kutumia Net wakati wa usku, pamoja na kuvaa nguo ndefu wakati wa mchana,kutoacha vichaka,au madimbwi ya maji karibu na makazi ya watu pamoja na njia nyingine za kujikinga na Mbu.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Post a Comment

0 Comments