Ticker

6/recent/ticker-posts

Utafiti mpya juu ya saratani ya Tezi Dume unaweza kusababisha utambuzi bora na matibabu mazuri Zaidi



Utafiti mpya juu ya saratani ya Tezi Dume unaweza kusababisha utambuzi bora na matibabu mazuri Zaidi.

Watafiti wanasema; Teknolojia ya artificial intelligence imewasaidia kugundua aina ndogo mbili za Saratani ya Tezi dume(two subtypes of prostate cancer).

Wanaeleza kwamba; Aina hizi mpya Za Saratani ya Tezi dume zilizogunduliwa na teknolojia hii zinaweza kutumika ili kugundua vizuri na kwa haraka mgonjwa wa Saratani ya Tezi dume pamoja na Kuboresha Matibabu yake.

Nanukuu maneno kwenye utafiti huu;

“The new prostate cancer “evotypes” could be used to better diagnose patients and improve treatments.

Pia waliongeza kwa Kusema; Matokeo ya utafiti huu yanaweza kuwa muhimu sana katika kutibu Ugonjwa huu pale ambapo tiba imetolewa kwa Kiwango cha chini au kupita kiasi.

The findings could be especially valuable in treating a disease where both under-treatment and over-treatment can occur.

Watafiti hao wanaeleza kwamba; mchakato huu ulisaidiwa na artificial intelligence (AI), Teknolojia hii ndyo iliyosaidia kugundua aina hizi mbili ndogo za Saratani ya Tezi Dume — Na matokeo haya yatasaidia sana kwenye kuboresha ugunduzi na matibabu kwa wagonjwa wa tezi dume pamoja na kuzuia kufanyiwa upasuaji usio wa walazima.

Matokeo yote ya Utafiti huu yalichapishwa kwenye jarida la “the journal Cell Genomics”.

Kwenye Utafiti huo, Watafiti kutoka chuo kikuu cha Oxford pamoja na Chuo kikuu cha Manchester nchini Uingereza; ndyo waliogundua aina ndogo mbili za Saratani ya Tezi dume “prostate “evotypes” kwa kutumia mfumo wa AI kuchambua data za DNA.

Utafiti huu ulifanyika kwa kuchukua Sample ya Washiriki 159, Na;

Watafiti wanasema matokeo hayo yanaweza pia kusaidia kukuza na kuboresha upimaji wa genes(genetic tests), Na hii inaweza kuwapa wagonjwa ubashiri na matibabu sahihi.

Rupal Mistry, PhD, meneja mkuu wa ushiriki wa sayansi katika Utafiti wa Saratani Uingereza, ambapo alisaidia kufadhili utafiti huo, aliiambia Medical News Today kwamba utafiti huo “uliweka misingi ya matibabu binafsi kwa watu walio na saratani ya tezi dume, na kuruhusu watu zaidi kuushinda ugonjwa huo”

“Utafiti wetu unaonyesha kuwa uvimbe wa tezi dume hubadilika kulingana na njia nyingi, hivyo basi kusababisha aina mbili za magonjwa,” alisema Dk. Dan Woodcock, mtafiti mkuu na kiongozi wa kikundi katika sayansi ya data ya tafsiri katika Idara ya Nuffield ya Sayansi ya Upasuaji katika Chuo Kikuu cha Oxford. ,

katika taarifa kwa vyombo vya habari. “Uelewa huu ni muhimu kwani huturuhusu kuainisha tumors kulingana na jinsi saratani inavyoibuka badala ya mabadiliko ya jeni au mifumo ya kujieleza.”



Post a Comment

0 Comments