Ticker

6/recent/ticker-posts

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake



Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake.

Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu)

Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?

Ugonjwa wa Pink eye ni ugonjwa wa macho pia ingawa ni nadra sana kutokea, ila wapo baadhi ya watu hupatwa na Ugonjwa huu.

Ugonjwa wa Pink eye,huweza kusababisha macho kuwa ya Pink, kuwasha,kuuma,kuhisi hali ya kuungua,kutoa uchafu au kuvimba ndani na kuzunguka jicho au macho.

Ingawa ni nadra sana kutokea ugonjwa huu, ila upo na wapo baadhi ya watu hupata.

Mtu mwenye Pink eye hupata tatizo la Conjunctivitis, au kuvimba kwa conjunctiva —

Pink eye huweza kuambukizwa na mara nyingi huhusishwa na watoto, lakini mtu yeyote anaweza kupata. Matibabu itategemea ikiwa maambukizi kwenye jicho lako yanatokana na virusi, bakteria, mizio, au vitu vya kuwasha jicho.

Pia Ugonjwa wa Pink eye husababisha wekundu kwenye macho, kuwasha, maumivu, kuchoma, kutokwa na uchafu na uvimbe ndani na karibu na macho. Kusababisha tatizo la kuona marue rue, ukungu na kukufanya uhisi mwanga zaisi, lakini bado utaweza kuona.

Pink eye inaweza kutokea kwa mtu yeyote, bila kujali umri, lakini ni kawaida Zaidi kwa watoto. Inaweza kuambukiza sana, kuenea kwa haraka katika shule na vituo vya kulelea watoto wachanga, lakini ugonjwa huu ni mara chache sana kutokea.

Ugonjwa huu Hauwezi kuharibu uwezo wako wa kuona, hasa ikiwa utapata matibabu kwa haraka. Unapotunza, kuzuia kuenea kwake na kufanya kila kitu ambacho daktari wako anapendekeza, jicho la pink husafishwa bila matatizo ya muda mrefu.

Chanzo cha Pink Eye

Je unawezaje kupata Pink Eye?

Hizi hapa ni baadhi ya Sababu ambazo huongeza hatari ya wewe kupata Ugonjwa wa pink Eye;

1. Maambukizi ya Viruses

2. Maambukizi ya Bacteria

3. Tatizo la Mzio au Allergies dhidi ya vitu mbali mbali kama vile; vumbi,moshi, pollen, n.k

Irritants zingine ni kama vile shampoos, uchafu, moshi na klorini ya bwawa

4. Reactions kwenye baadhi ya dawa za macho yaani eye drops

5. Reactions baada ya kuvaa miwani au contact lens

6. Maambukizi ya Fangasi, amoebas, au parasites.

Ugonjwa huu wa Pink Eyes wakati fulani hutokana na magonjwa ya Zinaa(STDs). Ugonjwa kama Kisonono unaweza kuleta aina hatari ya bakteria ambayo huweza kushambulia macho na kusababisha tatizo la conjunctivitis.

Na Unaweza kusababisha kupotea kwa uwezo wa kuona ikiwa hautatibu. Klamidia inaweza kusababisha conjunctivitis kwa watu wazima. Ikiwa una chlamydia, kisonono, au maambukizi ya bakteria wengine katika mwili wako unapojifungua, unaweza kupitisha tatizo la jicho la pinki(Pink Eye) kwa mtoto wako kupitia njia ya kujifungua(Ukeni).

Pink eye, inayosababishwa na baadhi ya bakteria na virusi, inaweza kuenea haraka kutoka kwa mtu hadi mtu. Lakini sio hatari kubwa kiafya ikiwa itagunduliwa mara moja. Hata hivyo, ikiwa hutokea kwa mtoto mchanga, mwambie daktari mara moja, kwani inaweza kuwa maambukizi ambayo yanaweza kuathiri macho ya mtoto.



Post a Comment

0 Comments