Ticker

6/recent/ticker-posts

Ugonjwa wa Typhoid,Chanzo,Dalili na Tiba yake



Ugonjwa wa Typhoid,Chanzo,Dalili na Tiba yake

Ugonjwa wa Typhoid ni Ugonjwa wa homa ya matumbo,hujulikana pia kama Typhoid fever au enteric fever, na chanzo chake ni maambukizi ya bacteria wanaojulikana kama salmonella bacteria. 

Maji kuchafuliwa pamoja na vyakula tunavyokula huweza kupelekea bacteria hawa kusambaa na kuingia kwenye miili yetu,kisha kupelekea ugonjwa wa typhoid au homa ya matumbo.

DALILI ZA UGONJWA WA TYPHOID

Dalili zinaweza kuanza polepole, mara nyingi huonekana wiki 1 hadi 3 baada ya kuathiriwa na bakteria kama salmonella bacteria. 

Dalili za Awali;

Dalili za awali ni pamoja na;

1. Mtu kuwa na Homa,

Homa ambayo huanza chini na kuongezeka siku nzima, ikiwezekana kufikia 104 degrees Fahrenheit (40 degrees Celsius).

2. Mwili kutetemeka

3. Kupata maumivu ya Kichwa

4. Mwili kuchoka sana na kuwa dhaifu

5. Kupata maumivu ya Misuli

6. Kupata Maumivu ya Tumbo

7. Kuharisha au kupata Choo kigumu(constipation).

8. Wengine hupata upele au Rashes kwenye ngozi.

9. Baadhi pia huweza kuwa na dalili zingine kama vile;

  • Kupata kikohozi
  • Kukosa Hamu ya kula
  • Kutoa Sana jasho n.k

Dalili za baadae;

Wiki chache baada ya dalili kuanza, ugonjwa unaweza kusababisha matatizo katika tumbo. Watu wanaweza kuwa na:

– Maumivu makali ya Tumbo

– Tumbo kuvimba Sana

Pia Maambukizi yanayosababishwa na bakteria hawa tumboni yanaweza kuenea katika mwili wote na kusababisha hali inayoitwa sepsis.

VIPIMO:

#SOMA Zaidi Hapa Kuhusu Vipimo cha Typhoid au homa ya matumbo

Chanzo cha Ugonjwa wa Typhoid

Aina ya bakteria inayoitwa Salmonella enterica serotype typhi ndyo husababisha homa ya matumbo au Ugonjwa wa Typhoid. Aina zingine za bakteria wa salmonella husababisha ugonjwa kama huo unaoitwa paratyphoid fever.

Watu hupata bakteria hawa kwa kiasi kikubwa katika maeneo ambayo milipuko ya Ugonjwa wa Typhoid hutokea mara nyingi. Bakteria hutoka nje ya mwili kwenye kinyesi na mkojo wa watu wanaobeba bakteria.

Bila kuosha mikono kwa uangalifu baada ya kwenda Chooni, bakteria wanaweza kupita kutoka kwenye mikono hadi kwa vitu vingine kama maji,chakula n.k au kwa watu wengine.

Bakteria pia wanaweza kuenea kutoka kwa mtu ambaye hubeba bakteria. Wanaweza kuenea kwenye chakula ambacho hakijapikwa, kama vile matunda mabichi ambayo hayana maganda.

Pia Katika maeneo ambayo maji hayatibiwi ili kuua vijidudu, unaweza kuchukua bakteria kutoka kwenye chanzo hicho. Hii inajumuisha maji ya kunywa, kutumia barafu iliyotengenezwa kwa maji ambayo hayajatibiwa, au kwa kunywa maziwa au juisi ambayo haijasafishwa(unpasteurized milk or juice). n.k

IKIWA UNA SHIDA HII KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Post a Comment

0 Comments