Ticker

6/recent/ticker-posts

Maumivu chini ya kitovu,chanzo na Tiba yake



Maumivu chini ya kitovu,chanzo na Tiba yake

Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza chanzo chake ni nini?

Maumivu chini ya kitovu yanaweza kuwa dalili za hali kadhaa, kama vile maambukizi ya njia ya mkojo, maumivu ya hedhi, matatizo ya utumbo kama vile kuvimba kwa utumbo, au hata mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi. Ni muhimu kushauriana na daktari ili kupata uchunguzi sahihi na matibabu sahihi.

Katika Makala hii, nitajadili chanzo cha maumivu chini ya kitovu kwa undani zaidi.

Maumivu chini ya kitovu ni tatizo linaloweza kutokea kwa watu wa umri na jinsia zote, na sababu zake zinaweza kutofautiana kulingana na hali ya mtu binafsi. Hapa nitaelezea baadhi ya sababu za kawaida za maumivu hayo:

1. Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI):

Maambukizi ya njia ya mkojo ni sababu ya kawaida ya maumivu chini ya kitovu, haswa kwa wanawake. Bakteria wanaweza kusababisha maambukizi haya, ambayo huathiri mfumo wa mkojo, kuanzia kwenye kibofu hadi kwenye urethra.

Dalili zinaweza kujumuisha maumivu wakati wa kukojoa, hisia ya kutaka kwenda kukojoa mara kwa mara, na maumivu chini ya kitovu.

>>SOMA Zaidi hapa Kuhusu Maambukizi ya njia ya mkojo(UTI)

2. Matatizo ya Utumbo:

Pia Matatizo kama vile kuvimba kwa utumbo, spastic colon (colon ambayo hufanya kazi ya ziada), au matatizo mengine ya utumbo yanaweza kusababisha maumivu chini ya kitovu.

Hali kama vile colitis (kuvimba kwa utando wa utumbo mpana) au ileitis (kuvimba kwa sehemu fulani ya utumbo) zinaweza kusababisha dalili kama maumivu, kuharisha, au mabadiliko katika kula.

#SOMA Hapa Zaidi Kuhusu Saratani ya Utumbo mpana(Colon cancer)

3. Matatizo ya Uzazi kwa Wanawake:

Kuvimba kwa mirija ya uzazi au maambukizi kwenye viungo vya uzazi kama vile ovari, kibofu cha uzazi, au mfuko wa uzazi yanaweza kusababisha maumivu chini ya kitovu kwa wanawake.

Matatizo kama vile endometriosis (ambapo tishu zinazofanana na utando wa ndani wa uterasi hukua nje ya uterasi) au fibroids (uvimbe katika uterasi) ni sababu za kawaida za maumivu haya.

#SOMA Hapa Zaidi Kuhusu PID

4. Matatizo ya Figo:

Matatizo kama vile maambukizi ya figo au mawe ya figo yanaweza kusababisha maumivu chini ya kitovu. Maumivu yanayohusiana na figo mara nyingi huenda yakawa ya upande mmoja wa mwili, lakini yanaweza kusambaa hadi sehemu ya chini ya tumbo.

5. Matatizo ya Misuli na Viungo:

Maumivu chini ya kitovu yanaweza pia kusababishwa na matatizo ya misuli au viungo katika eneo hilo. Kuvuta misuli, kuharibika kwa tishu, au hata misuli iliyokwama inaweza kusababisha maumivu haya.

MAUMIVU YA CHINI YA KITOVU,MGONGO NA MATITI BAADA YA KUJIFUNGUA/KUZAA

Maumivu ya tumbo hasa chini ya kitovu,
mgongo na matiti mara baada ya
kujifungua/kuzaa na ambayo huongezeka
wakati wa kunyonyesha kitaalamu yanaitwa "afterpains"

Mara kadhaa watu wamekuwa wakiamini kuwa maumivu yanayoambatana na zoezi zima la kujifungua hupotea mara baada ya kujifungua. Kitu ambacho inawezekana si sahihi kwa wote.

Nyakati za awali mara baada ya kujifungua inaaminika kunakuwa na mabafiliko katika baadhi ya maeneo ya ubongo ambayo kwa namna moja ama nyingine hupelekea fikira na mitazamo ambayo hupelekea kuhisi maumivu makali isivyo kawaida.

Kuzaa kwa upasuaji au kuzaa kwa njia ya kawaida lakini kwa kusaidiwa na vifaa kunaambatana na maumivu makali baada ya kujifungua ukilinganisha na unapozaa kawaida. Kwa kawaida maumivu haya hutegemea hisia, mawazo na mtazamo.

Maumivu ya tumbo hutokea ikiwa ni matokeo ya mji wa mimba kunywea au kupungua kwa mji wa mimba katika hatua ya kurudi katika umbo la awali kabla ya kubeba ujauzito.

Namba ya nzao inahusishwa na kiwango cha maumivu haya. Katika mimba ya kwanza maumivu haya huweza kuwa sio makali sana n uweza kuisha ndani ya muda mfupi, lakini baada ya mimba mbili na kuendelea inaaminika maumivu huongezeka kutokana ukweli kuwa misuli ya mji wa mimba inakuwa imepunguza nguvu ya mvutano hivyo hupitia katika kipindi cha kunywea na kujilegeza hivyo kupelekea maumivu kuwa endelevu kwa muda.

Mimba zenye mapacha, watoto wakubwa, kiwango kikubwa cha maji katika mfuko wa mtoto, maambukizi nk zinaaminika kuambatana na maumivu haya mara baada ya kujifungua.

Kunyonyesha huweza kuleta au kuongeza kiwango cha maumivu kwasababu kitendo cha kunyonyesha hupelekea kutolewa kwa homoni ya oxytocin ambayo huchochea kunywea kwa mji wa mimba na hivyo maumivu.

Maumivu haya huweza kuwa chini ya kitovu, mgongoni au kwenye matiti.

Asilimia 64 ya kinamama hufananisha maumivu haya na maumivu ya hedhi. Baadhi hufananisha na maumivu au hisia mtoto akicheza awapo tumboni, wengine hufananisha na maumivu ya njaa na wengine huyafananisha na kitu kigumu kinachotembea kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

NAMNA YA KUZIA AU KUPUNGUZA
kukojoa mara kwa mara, kulalia tumbo (kulala kifudi fudi) AU kujikanda na maji ya vuguvugu inaweza kusaidia.

Matumizi ya dawa , za kutuliza maumivu, hupelekea kukata au kutulia kwa maumivu haya

Hitimisho

Kumbuka kuwa hizi ni sababu chache tu za maumivu chini ya kitovu, na kila mtu anaweza kuwa na sababu tofauti. Ni muhimu kwa mtu mwenye maumivu haya kutafuta ushauri wa kitaalam ili kupata utambuzi sahihi na matibabu stahiki.

Kwa kujua chanzo cha maumivu, matibabu yanaweza kutolewa ipasavyo ili kupunguza au kutibu kabisa tatizo.

NA KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Post a Comment

0 Comments