Magonjwa
UGONJWA WA PANGUSA(chlamydia,chanzo,dalili tiba)
PANGUSA
• • • • • •
UGONJWA WA PANGUSA(chlamydia,chanzo,dalili tiba)
Ugonjwa wa pangusa ni ugonjwa wa zinaa au ugonjwa unaoambukizwa kwa njia ya kufanya ngono, na ugonjwa huu kwa kitaam hujulikana kama Chlamydia.
CHANZO CHA UGONJWA WA PANGUZA
Ugonjwa wa pangusa au Chlamydia husababishwa na vimelea mbali mbali vya magonjwa ikiwa ni pamoja na Backteria jamii ya haimophilus ducrey.
Bacteria hawa husambazwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana.
DALILI ZA UGONJWA WA PANGUSA NI PAMOJA NA;
– Mgonjwa huanza kuwa na viupele sehemu za siri ambavyo baadae huchubuka na kuwa vidonda
– Mgonjwa kupata maumivu makali kwenye vidonda hivi
– Mgonjwa kuhisi muwasho kwenye vidonda
– Vidonda hivi hutoa damu pale vinapoguswa au kubinywa
– Joto la mwili la mgonjwa kuwa juu au mgonjwa kuwa na homa
– Mgonjwa kukosa hamu ya kula chakula
– Na wakati mwingine mgonjwa kupata shida wakati wa kutembea
– kupata maumivu wakati wa kukojoa
– Kutokwa na uchafu(discharge) kwenye uume au Ukeni
– Kupata maumivu wakati wa tendo kwa wanawake
– Kutoa damu(blid) katikati ya period na baada ya tendo la ndoa
– Kupata maumivu kwenye korodani
– Kupata maumivu sehemu ya haja kubwa n.k
MAMBO YA KUEPUKA ILI KUJIKINGA NA UGONJWA HUU WA PANGUSA
– Epuka kufanya ngono zembe(mapenzi bila kinga au condom)
– Epuka tabia ya kuwa na wapenzi wengi
– Epuka tabia ya kufanya mapenzi kinyume na maumbile
– Kamuone mtaalam wa afya baada ya kuhisi haupo sawa
MATIBABU YA UGONJWA WA PANGUSA
✓ Matibabu sahihi ya ugonjwa wa pangusa huhusisha matumizi ya dawa mbali mbali kama vile Azithromycin na Doxcycline kutwa mara mbili kwa siku 7 au siku 14.
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.