Connect with us

afyatips

kukosa ladha ya chakula mdomoni

Avatar photo

Published

on

kukosa ladha ya chakula mdomoni

Kukosa ladha ya chakula mdomoni ni tatizo ambalo kwa kitaalam hujulikana kama Ageusia, ikiwa na maana Loss of Sense of Taste.

Tatizo hili huweza kusababishwa na sababu mbali mbali ikiwemo;

  • Maambukizi ya magonjwa
  • Baadhi ya Dawa
  • Tatizo la Lishe,Upungufu wa virutubisho mwilini au nutritional deficiencies
  • Pamoja na Sababu Zingine

Pia,Kwa baadhi ya Watu,inaweza kuwa dalili kwa Mtu mwenye COVID-19. Na asilimia kubwa,kutibu chanzo husika cha tatizo hili huweza kukurudisha kwenye hali yako ya kawaida.

Kukosa ladha ya chakula mdomoni au tatizo la Ageusia huweza kusababisha iwe Vigumu kwa Mtu Kujua ladha mbali mbali za vitu yaani ladha kama vile;

  1. Tamu| sweet,
  2. Chachu|sour,
  3. Chumvi|salty 
  4. Au Chungu|bitter.

Kukosa ladha ya chakula mdomoni ni tatizo ambalo huweza kumpata Mtu yeyote,wa umri wowote, ingawa hutokea Zaidi ikiwa umri wako ni mkubwa,mfano Zaidi ya Miaka 50.

Tatizo hili sio Kubwa Sana, na baadhi ya tafiti zinaonyesha, Kati ya Watu 1,000, mtu 1 au 2 wanaweza kuwa na tatizo hili la Kukosa ladha ya chakula mdomoni.

Dalili Za Tatizo la Kukosa ladha ya chakula mdomoni

Dalili kubwa ni Mtu kushindwa kutofautisha ladha ya chakula chochote anachokula, Lakini pia unaweza kupata dalili Zingine ikiwemo;

– Kukosa Hamu ya Kula

– Shinikizo la Damu kuwa Juu

– Shida ya Pua Kuziba

– Kupata shida ya Kupumua n.k

Chanzo cha tatizo la Kukosa ladha ya chakula mdomoni

Zipo Sababu nyingi ambazo huweza kuchangia hali hii, na baadhi ya Sababu hizo ni Pamoja na;

  • Maambukizi ya magonjwa kama Vile COVID-19 n.k
  • Maambukizi au Sinus infection (sinusitis)
  • Tatizo la Mafua
  • Tatizo la Pharyngitis (sore throat).
  • Strep throat.
  • Maambukizi kwenye tezi la Mate au Salivary gland infections.
  • Magonjwa ya meno au Fizi,Gum (periodontal) disease.
  • Kuumia kichwani au kwenye Masikio n.k,(Injuries to your head or ear).

Pia,tatizo la Kukosa ladha ya chakula mdomoni huweza kuhusishwa na matatizo mengine ya Kiafya kama vile;

1. Tatizo la Unene au Uzito kupita kiasi(Obesity/overweight)

2. Ugonjwa wa Kisukari

3. Uvutaji wa Sigara

4. Lishe duni au Poor nutrition.

5. Matatizo kama vile Sjogren’s syndrome,Shinikizo la Juu la Damu

6. Upungufu wa Virutubisho mwilini kama vile zinc pamoja na vitamin B-12.

7. Tatizo la Mdomo mkavu Dry mouth (xerostomia)

8. Magonjwa kama vile Alzheimer’s disease,Parkinson’s disease,Multiple sclerosis (MS).n.k

9. Matumizi ya baadhi ya Dawa kama vile lithium, dawa za kutibu Saratani,dawa za tezi la thyroid n.k

Tatizo hili hukaa kwa Muda Gani?

Ageusia inaweza kudumu kwa muda gani?
Inategemea. Kwa kawaida, dalili zinaendelea hadi hali ya msingi itatibiwa. Watu ambao wana ageusia kama dalili ya COVID-19 kawaida hupona baada ya wiki moja hadi tatu. (Kumbuka: Watu wengi ambao huendeleza ageusia kama dalili ya coronavirus pia wana anosmia – kupoteza hisia.)

Vipimo vya tatizo la Kukosa ladha ya chakula mdomoni

Matatizo ya ladha kama vile ageusia kwa kawaida hutambuliwa na mtaalamu wa masikio, pua na koo (ENT). Watakuuliza maswali kuhusu dalili zako na kukagua historia yako ya afya ili kubaini ikiwa hali zozote zilizopo zinaweza kusababisha upotevu wako wa ladha.

Matibabu ya tatizo la Kukosa ladha ya chakula mdomoni

Ndiyo. Katika hali nyingi, kutibu hali ya msingi ambayo imesababisha ageusia husaidia kurejesha uwezo wako wa ladha ya chakula Mdomoni.

Ni mara ngapi baada ya matibabu nitajisikia vizuri?

Inategemea kile kilichosababisha tatizo la kukosa ladha mdomoni. Ikiwa mzio, baridi au homa ilisababisha ageusia, ladha yako inaweza kurudi baada ya kutumia dawa jamii ya antihistamines au decongestants.n.k

Maambukizi yanaweza kutibiwa na dawa jamii ya antibiotics. Mtoa huduma wako wa afya anaweza kukusaidia kuamua ni hatua gani ya kuchukua. Mara tu unapopona ugonjwa wako, hisia zako za ladha zitarudi.

Wakati mwingine, ageusia inaweza kutatuliwa kwa kuboresha tabia yako ya maisha. Kwa mfano, watu wanaoacha kuvuta sigara wanaweza kurejesha hisia zao za ladha katika muda wa saa 48. Ikiwa ageusia yako inahusiana na ugonjwa wa fizi, kuhakikisha usafi wa kinywa kunaweza kusaidia kurejesha utendakazi wako wa ladha haraka.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO HILI,TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa6 days ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa3 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa4 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa4 weeks ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Magonjwa1 month ago

Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga

“Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga” Kifo cha ghafla ni janga lisilotarajiwa ambalo linaweza kumpata...

Trending