Others
Uganda yaripoti kifo cha kwanza kinachotokana na Virusi vya Homa ya nyani,Mpox
Imeboreshwa July 10, 2026 by Doctor Ombeni
Uganda yaripoti kifo cha kwanza kinachotokana na Virusi vya Homa ya nyani,Mpox
Takriban miezi mitatu baada ya maambukizi ya hapo awali kuripotiwa nchini. Maelezo kutoka kwa wizara hiyo yanaonyesha kifo hicho kiliripotiwa Masindi kutoka kwa mtu anayeugua na virusi vya ukimwi.
Kulingana na ripoti iliyonukuliwa kutoka kwa Wizara ya Afya na vyombo vya habari nchini Uganda, Wilaya ya Masindi imesajili maambukizi matatu ya ugonjwa wa Mpox, ambao hutambulika kwa kutoka majipu yaliyojaa usaha usoni, sehemu za siri na sehemu zingine za mwili.
Akizungumza na maofisa wa afya na viongozi wa wilaya wakati wa Misheni ya Kudhibiti Mpango wa Pamoja wa Afya wa Mwaka jijini Kampala siku ya Jumatano, Dkt. Jane Ruth Aceng, Waziri wa Afya, alitoa wito wa kuanzishwa upya kwa vikundi maalum vya kupambana na Mpox, kama vile ilivyokuwa wakati wa Covid-19.
Mlipuko wa Mpox, tunaweza kudhani ni suala rahisi lakini hali halisia ni suala gumu. Mlipuko huu ambao umeathiri dunia nzima unahitaji kudhibitiwa na kukomeshwa.
Nchini Uganda, maambukizi haya yalithibitishwa tarehe 24 Julai, 2024,” alisema.
“Mlipuko unaendelea kuenea. Hadi sasa, tuna jumla ya maambukizi 153, kati ya hizo 42 zilikuwa katika wiki moja iliyopita. Katika siku chache zilizopita, idadi ya maambukizi inaongezeka kwa kasi,” aliongeza.
Dkt. Aceng alifichua kuwa wilaya 19 zimeripoti maambukizi. Ilioathirika zaidi ni Kampala yenye maambukizi 55, ikifuatiwa na Nakasongola, jumuiya ya wavuvi, ambayo ina maambukizi 35, na Wakiso yenye maambukizi 23.
-
magonjwa ya wanaume6 days agoMaumivu ya korodani chanzo chake na Tiba
-
Uzazi/Ujauzito2 weeks agoVyakula vya kuongeza maziwa kwa mama anayenyonyesha
-
Stars Health4 days agoMuigizaji Kaylee Hottle wa Godzilla afariki dunia
-
magonjwa ya watoto4 weeks agoMadhara ya mtoto kunywa maji machafu au maji ya uzazi
-
magonjwa ya watoto4 days agoMtoto kujisaidia kinyesi cha kamasi
-
afyatips16 hours agoFahamu Uhusiano wa Kisukari na Ganzi
-
Stars Health4 days agoBaba wa Msanii Meja Kunta Afariki Dunia kutokana na Presha
-
magonjwa2 weeks agoUgonjwa wa ngozi kuwasha chanzo na Tiba

.jpeg)