Connect with us

Story

Idara ya Uhamiaji ya Gambia (GID) imezindua rasmi sare mpya kwa wajawazito

afyaclass

Published

on

Idara ya Uhamiaji ya Gambia (GID) imezindua rasmi sare mpya zilizobuniwa mahsusi kwa Maafisa wajawazito, hatua inayolenga kuboresha ustawi wao na kuwawezesha kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa faraja na heshima katika kipindi chote cha ujauzito.

Kwa mujibu wa ripoti za Vyombo vya Habari Nchini huko, Uongozi wa Idara hiyo umeeleza kuwa sare hizo zimeundwa kwa kuzingatia mahitaji ya Maafisa wajawazito ili kuwawezesha kufanya kazi kwa ufanisi bila kulazimika kuvaa sare zisizowatosha kadri ujauzito unavyoendelea.

Inaelezwa kwamba, hatua hiyo pia inaonyesha dhamira ya taasisi hiyo ya kujenga mazingira jumuishi na rafiki kwa Maafisa Wanawake.

Kwa mujibu wa GID, uzinduzi wa sare hizo ni sehemu ya maboresho ya sera za Ustawi wa Watumishi, ukilenga kuimarisha usawa mahali pa kazi na kuthibitisha kuwa ujauzito haupaswi kuwa kikwazo kwa Mwanamke kutekeleza majukumu yake ya kikazi kwa hadhi na kujiamini.
#MillardAyoUPDATES

Karibu Afyaclass Jukwaa linaloongoza kwa utoaji wa elimu sahihi ya Afya. Hapa utapata Ushauri & Tiba,Elimu na Updates mbali mbali za Afya Duniani. Pia Pata dondoo za afya kila siku kwa kufuatilia kupitia: @Facebook | @Instagram | @YouTube.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *