Connect with us

Ebola

Kasi ya Ugonjwa wa Ebola ni kubwa kuliko mwitikio

afyaclass

Published

on

Kasi ya Ugonjwa wa Ebola ni kubwa kuliko mwitikio

Akizungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani siku ya Jumatano Julai 29 kutokea Bunia jimboni Ituri, Mratibu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Ebola Julien Harneis amegusia kasi ya ugonjwa akisema.

«Katika saa 24 zilizopita watu 15 wamekufa kwa Ebola DRC na idadi ya wagonjwa inaongezeka kwa kasi, ikiwa ni maradufu katika kila siku 20. Kasi ya ongezeko ni kubwa kuliko kasi yetu ya mwitikio.”

Amezungumzia pia watoa huduma wanaosaidia harakati za kudhibiti ebola akisema,

Lakini nimeshuhudia pia kazi ya kipekee ya watu kwenye jamii kama Grace na Christine wanaopika chakula cha WFP kwa ajili ya wagonjwa walioko kwenye vituo karibu na nyumbani kwao. Pia wahudumu wa kujitolea kwa Msalaba MWekundu wanaozika waliofariki dunia, vile vile wauguzi, madaktari na wakongomani kutoka bara la Afrika na kote duniani. »

Credits: Source UN(Umoja wa Mataifa)

Karibu Afyaclass Jukwaa linaloongoza kwa utoaji wa elimu sahihi ya Afya. Hapa utapata Ushauri & Tiba,Elimu na Updates mbali mbali za Afya Duniani. Pia Pata dondoo za afya kila siku kwa kufuatilia kupitia: @Facebook | @Instagram | @YouTube.