Connect with us

Magonjwa

jinsi ya kuongeza uume,fahamu ukweli wa mambo hapa

Avatar photo

Published

on

jinsi ya kuongeza uume,fahamu ukweli wa mambo hapa.

Swala la Kuongeza Uume imekuwa mada maarufu, huku wanaume wengi wakihitaji kujua jinsi ya kuongeza uume au maumbile yao na wengine hata kutumia vitu ambayo huwasababishia madhara makubwa sana kwenye miili yao,

Na hata wanaume wenye maumbile madogo wamekuwa wakiambiwa kuwa wana vibamia(kibamia-jina maarufu likimaanisha kuwa Mwanaume ana maumbile madogo au uume mdogo)

je ni kwanini Swala hili hutokea?

Swala hili hutokea kwa Sababu Wanaume wengi wana dhana kwamba wakiwa na Uume mkubwa au maumbile makubwa basi wataweza kufanya tendo la ndoa vizuri na kumfikisha mwanamke kileleni,

Wengine hupata ushawishi kwenye jamii zao kwamba,sifa ya Mwanaume ni kuwa na Uume mkubwa, wengine wanaamini wakiwa na maumbile makubwa wataonekana Rijali na watawavutia wanawake walionao.

Lakini pia Baadhi ya Wanawake wenyewe wanadhana hii, kwamba wakipata Wanaume wenye maumbile makubwa,basi italeta raha Zaidi kwao, hali ambayo huwafanya baadhi ya wanaume wenye maumbile madogo kutafta namna ya kuyaongeza ili kukidhi haja za wapenzi wao.

Fahamu Zaidi Kitaalam ikoje na nini unapaswa Kufanya kama Mwanaume;

Raha ya tendo la ndoa,Mwanamke kuridhika au kufika kileleni,Mwanamke kupata msisimko zaidi kwenye tendo n.k, vitu vyote hivi havitegemei ukubwa wa Maumbile yako,

Ili ufanikishe hili inategemea na ujuzi wako binafsi, kuufahamu vizuri mwili wa mwanamke ikiwemo sehemu zake za siri jinsi zilivyoumbwa, kwa kutumia akili na viungo vya mwili kuleta raha,kuongeza msisimko na kumridhisha mwenza wako.

Usichokijua ni kwamba;  Mwanaume unatakiwa kuwa na uume wa wastani kuliko mkubwa uliopitiliza unaoweza kusababisha maumivu kwa mtu unayeshiriki naye tendo,

Hali ambayo huweza kumfanya Mwanamke asifurahie tendo hilo na kuongeza uwezekano wa kupata hofu kutokana na ukubwa huo.

Hivo basi, Fahamu kwamba unaweza kuwa na Uume mkubwa na ukawa ndyo chanzo cha maumivu makali,michubuko,kupata magonjwa, na kuongeza hofu kwa mwenza wako ikiwa huna ujuzi wa jinsi ya kufanya mapenzi ili kumridhisha mwenza wako.

Mamlaka za ndani na kimataifa kama vile Wizara ya Afya, Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), Shirika la Afya Duniani (WHO) na vyuo vikuu vilivyobobea kufanya utafiti kikiwemo chuo cha Havard, hakuna mahala ambapo wamepitisha na kupendekeza dawa au kifaatiba kwa ajili ya huduma hiyo ya Kuongeza maumbile au Uume.

Kitaalam: Hii inamaanisha swala sio kuhangaika na Size ya maumbile yako, Swala la msingi ni ujuzi wako binafsi, kuufahamu vizuri mwili wa mwanamke ikiwemo sehemu zake za siri jinsi zilivyoumbwa, kwa kutumia akili na viungo vya mwili kuleta raha,kuongeza msisimko na kumridhisha mwenza wako.

Fahamu maeneo muhimu ya kugusa wakati wa tendo la ndoa, hii italeta raha na kumfanya mwenza wako kuridhika Zaidi.

Watu wanene kupitiliza, shina la uume lililo chini ya kitovu humezwa na mafuta na nyama zilizorundikana hapo, hivyo kupunguza urefu wa kiungo hicho muhimu kwa tendo la ndoa,

Hivo kama ni mnene au Una Uzito mkubwa punguza uzito wako ili kuimarisha afya ya Uzazi ikiwemo nguvu zako za Kiume.

Zipo njia chache ambazo jumuiya za kimataifa na mamlaka za afya wanakubali kuwa zinaweza kusaidia angalau kuongeza urefu, lakini usiozidi nchi moja, njia hizo ni pamoja na kupunguza unene.

Hivyo, kupunguza unene kwa njia ya vyakula na mazoezi inakubalika. Vilevile kwa njia ya upasuaji kwa lengo la kupunguza mafuta ya eneo hilo inakubalika pia.

Tahadhari; Vitu vinavyotumika kiholela kunenepesha na kurefusha uume ni pamoja na vidonge, sindano, virutubisho, mashine maalumu, upasuaji wa kupandikiza, vifaa vya mazoezi ya uume, mafuta ya kupaka uumeni na mitishamba.

Vitu hivi vinauzwa kisiri katika baadhi ya maduka ya dawa, kwa njia ya mtandao, kutembezwa mtaani au matangazo kwenye magazeti na vyombo vingine vya habari.

Lakini, kati ya hivyo nilivyotajwa, hakuna vinavyofanya kazi kwa ufanisi na kukidhi vigezo vya kitaalam kupitia vyombo vikubwa vya matibabu na uthibiti wa magonjwa ikiwemo WHO.

Kwa sababu hakuna utafiti wa kisayansi kuthibitisha ubora, ufanisi na usalama wa vifaatiba hivyo au njia zilizopendekezwa ingawa ni kweli, vipo baadhi ambavyo kwa muda mfupi, vinaweza kukusaidia lakini vikikuacha na madhara makubwa hapo baadaye.

Madhara hayo ni pamoja na;

  • kupungua au kukosa kabisa nguvu za kiume,
  • kuchubuka kwenye uume,
  • kuvunjika kwa misuli sponji ya uume,
  • madhara ya nerve
  • Pamoja na kupata maumivu sugu wakati wa kujamiana.

Taarifa zinaonyesha wanaume wengi hujikuta wakinasa na kununua vifaa hivi kwa sababu ya kuathirika kwao kisaikolojia ambako huongeza shauku iliyopitiliza ya kuongeza maumbile.

Ukidadisi unakuta wengi wao hawajawahi kwenda kwenye kituo cha huduma za afya au hospitali kwa ajili ya uchunguzi na ushauri. Wengi wanaojihisi wana uume mdogo hugundulika kuwa hawapo chini ya inchi tatu baada ya uume kusimama.

Chukua Tahadhari, jikinge na Madhara ya Muda Mrefu.!!!

Credits: #Dr.Ombeni Mkumbwa, #afyaclass, #Mwananchi, #WHO

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa1 month ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa2 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa4 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa3 days ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa4 days ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Magonjwa6 days ago

Chuchu kutoa maziwa ni dalili ya nini

Chuchu kutoa maziwa ni dalili ya nini Chuchu kutoa maziwa inaweza kuwa dalili ya ujauzito au inaweza kutokea kwa sababu...

Magonjwa1 week ago

Vipele Sehemu za Siri,Chanzo na Tiba yake

Vipele kwenye uume Ni dalili inayotokea sana kwa wanaume, licha ya kuweza sababishwa na magonjwa ya zinaa, mara nyingi vipele...

Magonjwa1 week ago

Ukambi ni ugonjwa gani,Soma hapa kufahamu

Ukambi ni ugonjwa gani? Ukambi kwa jina lingine rahisi ni surua),ambapo ni ugonjwa wa kuambukiza unaoenezwa sana kupitia mgusano, Ugonjwa huu...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa wa CHLAMYDIA,chanzo,dalili na Tiba yake

Ugonjwa wa CHLAMYDIA,chanzo,dalili na Tiba yake Chlamydia ni ugonjwa unaowapata watu wengi na unaenezwa kwa ngono,Hivo chlamydia ni miongoni mwa...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa wa zinaa pangusa,chanzo,dalili na Tiba

Ugonjwa wa zinaa pangusa,chanzo,dalili na Tiba Pangusa ni miongoni mwa magonjwa ya Zinaa ambayo hutokea kwa jinsia zote mbili(mwanaume na...

Magonjwa2 weeks ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa3 weeks ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...