Connect with us

Elimu&Ushauri

Maini, figo chanzo kikuu cha viinilishe mwilini

Avatar photo

Published

on

Maini, figo chanzo kikuu cha viinilishe mwilini

By DK. SHITA SAMWEL

Upo uvumi wa miaka mingi duniani kuhusu ulaji maini na figo za ng’ombe, mbuzi na kuku kuwa una madhara kutokana na ogani hizo kufanya kazi ya kuondoa sumu mwilini.

Kiujumla minofu ya nyama ya wanyama wanaoliwa ni moja ya vyakula ambavyo huwa na virutubisho mbalimbali, ikiwamo protini nyingi, iliyo muhimu kwa afya zetu.

Katika nyama hiyo, moja ya sehemu ambazo zina virutubisho vingi zaidi kuliko unavyoweza kupata katika minofu ni ogani ya ini. Sehemu hii ina protini nyingi zaidi kuliko ile inayopatikana katika minofu.

Ini ni ogani kubwa kuliko nyingine ndani ya tumbo, lina kazi kubwa na muhimu katika mwili, ikiwamo kuvunjavunja na kuchakata sumu, kemikali na dawa zenye usumu.

Vitu hivyo bila kuchakatwa na ini vikiingia katika mfumo wa damu na kusambaa maeneo mbalimbali ya mwili moja kwa moja zinaweza kudhuru.

Hapa unapata picha kuwa ini inafanya kazi hiyo tu, halifanyi kazi ya kuzihifadhi sumu hizo. Kazi hiyo ambayo kitabibu hujulikana kama detoxication.

Ikiwa utakula kitu chenye sumu au hata dawa lazima itapita katika ini, itavunjwa vunjwa hatimaye kufifishwa au kuondolewa sumu, aidha kwa kubadilishwa kuwa katika hali isiyo na madhara.

Baadaye baada ya uchakataji huo huweza kufika katika figo, ambazo zenyewe huchuja damu na kuondoa takasumu na mabaki yasiyohitajika mwilini kwa njia ya mkojo.

Figo nayo ina kazi nyingi, lakini kazi kuu mbili huwa ni kuondoa takasumu mwilini na kuweka usawa wa maji na madini.

Mkojo unaotengenezwa na figo ni salama, ambao huhifadhiwa katika kibofu mpaka pale mwili utakapohisi haja. Mkojo umebeba sumu za urea na nyingine zinazokuwa sumu endapo tu zitabaki ndani ya mwili kwa kiwango kikubwa.

Na wenyewe siyo sumu unapokuwa nje ya mwili. Kwa hiyo ile imani potofu ambayo unaweza kuikuta mtaani au mitandaoni kuwa ulaji wa maini na figo si sahihi, hawana ufahamu wa kina juu ya kazi za ini na figo kisayansi.

Kama ini na figo zingekuwa zinahifadhi sumu, ina maana kuwa ulaji wake ungelikuwa si salama. Maana makali ya sumu hizo yangekuwa palepale na ingeliweza kumdhuru yule atakayekula ogani hizi.

Ini huwa na kazi nyingi mwilini, ikiwamo kuhifadhi viini lishe, uundwaji wa protini, kudhibiti sukari ya mwili, kudhibiti joto la mwili, kuzalisha nyongo ambayo inahusika kusaga vyakula vya mafuta.

Kutokana na kazi zake, ndiyo maana huwa limesheheni virutubisho vingi vyenye faida kubwa kiafya kwa mlaji, ikiwamo madini kama kopa, chuma, patasiamu na vitamini kama A, B na D.

Protini inayopatikana katika ini huwa ni nyingi, ikiwa katika ubora wa juu ukilinganisha na ile ya minofu.

Kwa upande wa madaktari wa mifugo, wanashauri kutokula mnyama mgonjwa au ambaye amekula kitu na kumfanya aumwe.

Ndiyo maana inashauriwa kula nyama ambayo imekaguliwa na mabwana afya, ambazo ndizo zinazouzwa katika masoko ya nyama au machinjio maalumu.

Ulaji wa figo na maini ni salama kwa sababu zinavunja vunja, kufifisha sumu na hatimaye kuziondoa mwilini. Ogani hizi hazihifadhi sumu yoyote mwilini. Ni salama kuliwa na ni chanzo kikubwa cha viinilishe.

 

Karibu AfyaUpdates Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In https://afyaclass.com  Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 months ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 months ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa3 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa3 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa5 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake5 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa4 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri

Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri Yapo magonjwa mbali mbali ya ngozi ambayo huweza kuathiri Sehemu za Siri za Mwanaume...

Magonjwa6 days ago

Dalili za acid reflux,Soma hapa Kufahamu

Dalili za acid reflux: Tatizo la Gastroesophageal reflux disease (GERD), ni tatizo ambalo huwapata Watu wengi,Tatizo hili hujulikana kwa jina...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO

Ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe,VITILIGO Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi kuwa nyeupe au ni ugonjwa ambao huhusisha ngozi kupoteza rangi...

Magonjwa3 weeks ago

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni,...

Magonjwa4 weeks ago

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu

Scabies ni ugonjwa gani? Soma hapa kufahamu Utangulizi: Scabies huhusisha mtu kuwa na vipele na muwasho kwenye ngozi yake ambapo...

Magonjwa4 weeks ago

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume

Dalili za ugonjwa wa gono kwa mwanaume Gono ni neno maarufu ambalo kirefu chake ni Gonorrhea na kiswahili chake ni...

Magonjwa1 month ago

Dalili Mpya za ukimwi kwenye ngozi

Zipi ni Dalili za ukimwi kwenye ngozi Zipi ni dalili za Ukimwi kwenye ngozi ya mtu? Fahamu hapa kupitia makala...

Magonjwa1 month ago

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu

Madhara ya COVID-19: Athari za Ugonjwa, Asili na Matibabu Huu ni ugonjwa wa kuambukiza uliosababishwa na kirusi cha corona, ambao...

Magonjwa1 month ago

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake

Ishara za Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) kwa Wanaume na Wanawake Karibu! Hapa kwa makala yenye taarifa muhimu kuhusu...

Magonjwa1 month ago

Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga

“Vyanzo Vya Kifo cha Ghafla: Sababu Zinazotisha na Jinsi ya Kujikinga” Kifo cha ghafla ni janga lisilotarajiwa ambalo linaweza kumpata...

Trending