Connect with us

News

Hospitali binafsi zaanza kupokea bima za NHIF

Avatar photo

Published

on

Hospitali binafsi zaanza kupokea bima za NHIF

Baada ya wagonjwa wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kusitishiwa huduma kwa hospitali binafsi, baadhi ya hospitali zimeanza kutangaza kurejesha huduma kwa wanachama hao.

Kiini cha wanachama wa NHIF kusitishiwa huduma, ni Chama cha Watoa Huduma Binafsi za Afya nchini (APHFTA), kutangaza mgomo kikishinikiza kutokubaliana na matumizi ya kitita kipya cha mafao ya gharama za huduma 2023 kilichotolewa na NHIF, wakidai gharama zilizokokotolewa kwenye kitita hicho, ni hasara kwao.

Watoa huduma hao wamesema kama watatumia kitita kilichofanyiwa maboresho na NHIF, watakumbana na hasara ya hadi asilimia 30 kutokana na huduma nyingi kushushwa bei.

Mwenyekiti wa APHFTA, Dk Egina Makwabe ndiye aliyetangaza mgomo huo kuanzia Machi 1, 2024 kwa wagonjwa wote wanachama wa NHIF kutopokelewa kwenye hospitali binafsi, tamko ambalo lilifuatiwa na taarifa za hospitali mbalimbali kuwataarifu wanachama wa NHIF kuwa hawatapokelewa.

Hospitali ya Kairuki, Regency, T.M.J na Aga Khan ni miongoni mwa zilizotoa taarifa za kutopokea wanachama wa NHIF na baadaye NHIF ikiwaelekeza wanachama wake kutumia vituo mbadala kupata huduma, huku hospitali zinazomilikiwa na Serikali zikieleza kujipanga kupokea wagonjwa wote na kuwahudumia.

Akiwa mkoani Lindi, jana Ijumaa, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu aliziagiza Hospitali zilizositisha kuendelea na huduma akizitaka hospitali hizo kuingia kwenye mazungumzo na Serikali.

“Kamati ya kitaalamu niliyoiunda iendelee kufanya majadiliano na watoa huduma wakati huduma zikiendelea kutolewa. Naomba kusisitiza kuwa, majadiliano yatafanyika wakati huduma zinaendelea kutolewa,”alisisitiza Ummy.

Huduma zarejea

Kutokana na tamko hilo, Hospitali ya TMJ Dar es Salaam kupitia taarifa yake kwa umma jana ilitangaza kurejesha huduma.

“Bodi ya wakurugenzi wa Hospitali ya T.M.J baada ya kusikiliza kwa umakini hotuba ya Waziri wa Afya, wizara kufungua milango ya mazungumzo, tupo tayari kufanya makubaliano na NHIF chini ya wizara wakati huduma zikiendelea kwa wanufaika na bima ya NHIF.Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza,” imesema taarifa hiyo.

Pia nayo Hospitali ya Bochi ya Dar es Salaam Machi Mosi, ilitangaza kurejesha huduma za NHIF kwa wagonjwa kama kawaida.

“Wagonjwa wa bima ya afya zingine zote wanaendelea kupewa huduma kama kawaida kauli mbiu yetu ya OKOA MAISHA KWANZA itaendelea kutumika kwa wagonjwa wa dharura,”iliandikwa kwenye taarifa hiyo.

Taarifa hiyo ya Bochi, imewekwa na Waziri Ummy katika akauti yake ya X na kuandika, “Asanteni Bochi Hospitali na wote waliorudisha huduma kwa wanachama wa NHIF. Tunawashukuru sana sana. Ninawaahidi kuwa tutafanya maboresho katika maeneo mahususi mtakayoyaainisha ndani ya muda mfupi.”

Mbali na hizo, akaunti za kijamii za NHIF, zimeweka picha za Mkurugenzi Mkuu wa mfuko huo, Bernard Konga akiwa Hospitali ya Regency. Picha hizo zimeambatana na maelezo, “Mkurugenzi Mkuu wa NHIF Bw. Bernard Konga akishuhudia kurejea kwa huduma katika Hospitali ya Regency.”

“Uongozi wa NHIF ukiongozwa na Mkurugenzi Mkuu Bw. Bernard Konga umetembelea Hospitali ya Regency Medical Centre na kufanya mazungumzo na uongozi wa hospitali hiyo.”

Jana, baada ya kauli hiyo ya Waziri Ummy, Mwenyekiti wa APHFTA Dk Makwabe alisema wanamshukuru kiongozi huyo kwa kufungua majadiliano kwa mara nyingine.

Kwa mujibu wa chanzo cha taarifa zetu, APHFTA pamoja na Serikali leo wapo kwenye mazungumzo kuondoa sintofahamu baina yao.

Chanzo: Mwananchi

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...