Connect with us

Magonjwa

Ipi njia bora ya kuzuia ujauzito kwa Wanawake?

Avatar photo

Published

on

Ipi njia bora ya kuzuia ujauzito kwa Wanawake?

kwanza Njia za Uzazi wa Mpango zimegawanyika katika Makundi yafuatayo;

(a) Kuna Njia za asili au Tradition methods Mfano; KALENDA

(b) Kuna Njia za kisasa au Modern methods Mfano; Vipandikizi

Lakini pia Hizi za Kisasa tunaweza kuzigawanya zaidi katika Makundi yafuatayo;

(1) Njia za Mda Mfupi Mfano; Kondom za kike na za Kiume pamoja na Vidonge

(2) Njia za mda Mrefu Mfano; Vipandikizi au Njiti za miaka 3 na 5, Lupu au kitanzi cha miaka 10-12

(3) Njia za kudumu Mfano; Kufunga uzazi kwa mwanaume au mwanamke

NJIA ZOTE ZA UZAZI WA MPANGO NA MAELEZO YAKE

(1) KALENDA

Njia hii ni salama kwa asilimia mia moja(100%)  kwa mtumiaji japo kuna angalizo; Kama mzunguko wako wa hedhi haubadiliki badiliki basi njia hii inafaaa kwako, japo asilimia kubwa ya wanawake mizunguko yao ya hedhi hubadilika badilika hivo ni rahsi sana kupata Ujauzito wakitumia Njia hii.

?Hitimisho: Kalenda ni Njia bora na salama ya Uzazi wa Mpango ila kwa mtu ambaye Mzunguko wake wa hedhi haubadiliki badiliki yaani ni STABLE MENSTRUAL CYCLE

(2) KONDOM ZA KIUME NA KIKE

Hii pia ni Njia ya Uzazi wa Mpango salama na Nzuri kwani Ina faida mara mbili

(i) Kuzuia mimba

(ii) Kukukinga na Magonjwa ya Zinaaa kama Kaswende,Ukimwi n.k

Japo pia Wengine husema Hupunguza ladha ya Tendo la Ndoa.

(3) VIDONGE VYA MAJIRA

Njia hii huhusisha mtumiaji kumeza kila siku kidonge kimoja kimoja,na endapo ataacha au kusahau hata siku moja,yupo kwenye hatari ya Kupata Mimba au Ujauzito

Kutokana na vichocheo vilivopo katika Njia hii ya Uzazi bas Kuna maudhi madogo madogo huweza kumpata Mtumiaji kama vile; kuumwa na kichwa sana,kupata kichefuchefu na kutapika n.k

Hitimisho: Njia hii sio nzuri kwa Mtu ambaye anapanga Uzazi kwa mda mrefu kama miaka 2 au 3, kwani itamlazimu kumeza vidonge kila siku na kwa Mda mrefu

(4) SINDANO

Njia hii huhusisha uchomaji wa Sindano maarfu kama DEPO-INJECTION na haya ni maelezo kwa kina Juu ya Madhara ya athari za Sindano. ?

⚠️ MADHARA YA SINDANO ZA UZAZI WA MPANGO

Je Wajua kwamba sindano za uzazi wa mpango zinaweza;

âś“ kukusababisha ukakaa mda mrefu bila kubeba mimba Yaani kitaalam huitwa LONG INFERTILITY

âś“kulainisha mifupa yako ya mwili?

âś“zinaweza kuvuruga kabsa mzunguko wako wa hedhi? ikiwemo kukusababisha usipate kabisa hedhi kwa mda mrefu au kupata damu nyingi ya hedhi na kublid kwa mda mrefu pia?

âś“Maumivu makali ya kichwa,kichefu chefu,na kutapika

(5) NJITI/KIPANDIKIZI

kuna Njiti ya Miaka 3 na vile vya Miaka 5

Njia hii pia ina vichocheo ndani yake hivo,ni rahsi kwa mtumiaji kupata madhara yafuatayo;

* Kuumwa na kichwa sana pamoja kizunguzungu

* Kubalika kabsa kwa Mzunguko wa hedhi yaani IRREGULAR MENSTRUAL CYCLE,kupata blid kama vitone tone bila kukata au kutoka kwa mda mrefu,Kupata damu nyingi ya Hedhi na kwa mda mrefu mfano zaidi ya wiki moja.

* Kupatwa na kichefuchefu pamoja na Kutapika

MAUDHI AU MADHARA YA MATUMIZI YA NJITI/KIPANDIKIZI KAMA NJIA YA UZAZI WA MPANGO

Ukweli ni kwamba,kwa,asilimia kubwa Njia za uzazi wa Mpango ambazo zina vichocheo ndani yake huleta mabadiliko makubwa katika mwili wa Mtumiaji.

Mfano; Njia ya vidonge vya Majira,Sindano,Njiti au vipandikizi zote hizi ni aina za Njia za Uzazi wa Mpango zenye vichocheo ndani yake.

BAADHI YA MADHARA AU MAUDHI MADOGO MAGODO YA KUTUMIA NJITI KAMA NJIA YA UZAZI WA MPANGO.
Kuna kijiti cha Miaka 3 Na kuna vile vya Miaka 5, Vyote hivi ni aina ya Vipandikizi au Njiti.

(1)Kublid vitone vitone alafu kwa mda mrefu

(2)Kuwa na mzunguko wa hedhi unaobadilika badilika,Hapa tunaamanisha kitaalam kama Irregular Menstrual cycle Mfano; Mwezi huu umeona period yako siku ya 28,mwezi unaofata 21,Mwezi mwingine 33.Yaani hakuna Mpangilio maalumu unaoeleweka

(3)Maumivu makali ya kichwa,hili pia huweza kumpata mwanamke mtumiaji wa Njia hii Mara kwa Mara

(4)Kujisikia vibaya na kutapika pia

(5)Kukonda sana au kunenepa Sana

(6)Kublid damu nyingi na kwa Mda mrefu pia

(7)Kuchelewa kupata Ujauzito baada ya kuacha kutumia Njia hii.

(8)Kukaa mda mrefu bila Mwanamke kuona Siku zale

NB: SIO KILA NJIA YA UZAZI WA MPANGO NI MBAYA, mfano kalenda ni Njia ya Uzazi zuri sana kwa Mwanamke ambaye Mzunguko wake wa Hedhi haubaliki badiliki,Mfano kama ni Siku 28, ni hizo hizo siku zote. Cha muhimu ni upate Elimu ya kutosha Juu ya Mzunguko huu

ANGALIZO

Tafiti zinaonyesha Wanawake wengi huchagua njia flani za Uzazi wa Mpango kutokana na ushaur au ushawishi wa Mafariki,Ndugu,Jamaa,Majirani au Watu wanaowazunguka sio kutokana na Ushauri wanaopewa na Wataalm wa afya,Alafu wakija kupata Madhara wanalalamika.

NI VIZURI KWENDA HOSPTAL AU KUONA WATAALM WA AFYA USHAURIWE NJIA SALAMA INAYOENDANA NA MWILI WAKO.

Au pia unaweza kuwasiliana nasi kupitia namba +255758286584 tutakupa Maelekezo sahihi kwa ajili ya Afya Yako.

(6) LUPU/KITANZI

Njia hii kwa asilimia kubwa ni safi na salama kwani haihusishi uwepo wa kichocheo chochote ambacho kinaweza kuleta athari kubwa kwa mwili wa Mtumiaji kama vile kuvuruga vichocheo vya mwili yaani Hormone Imbalance n.k.

P2 NI NINI? NA MADHARA YAKE NI YAPI?

p2 ni dawa ya dharura (emergency contraceptive),inazuia mtu asipate Mimba kwenye mazingira ambayo umefanya sex pasipo kupanga na upo siku za hatari,au umelazimishwa kufanya sex au umebakwa,ili kuzuia mimba zisizotarajiwa unalazima Kunywa hizi dawa

P2-Ni Dawa iliyotengenezwa kutumiwa mara chache tu,inapokulazimu.Sio dawa unayotakiwa kutumia kama njia ya uzazi wa mpango ya muda mrefu. Kuna wanawake humeza p2 kila mwezi,hii haitakiwi. Katika mazingira ya kawaida,haipaswi kumezwa zaidi ya mara 3 kwa mwaka. Kuendekeza kila mwezi kunywa hizi p2 sio sahihi,Unatakiwa ende hospitali ili upate njia sahihi ya uzazi wa mpango ya muda mrefu.

Baadhi ya Side effects/madhara ni ya matumizi holela ya dawa hizi ni

1.Unaweza kujisikia kichefuchefu au kutapika baada ya kumeza,

2.Maumivu ya tumbo

3.Matiti kuuma na kujaa

4.Pia hedhi zako zinazofuata zinaweza zikawahi au zikachelewa au zikatoka nyingi sana( ukiona zimezidi siku 8 fika muone daktari) au ukawa unapata hedhi nyepesi sana,au pia haupati hedhi kabisa (amenorhoea)

5.Kichwa kuuma na kizunguzungu

6.Mabadiliko ya Ute ukeni (change in cervical secretion,hapa unakuta Ute wa ovulation mtu hapati).

7.Kupata maambukizi ukeni,vaginal infections

8.Hatari ya kupata PID

9.Maumivu wakati wa sex(dyspareunia)

10.Mama anakuwa hatarini kutungisha mimba nje ya kizazi yaani ectopic pregnancy.

11.Lakini pia kuna wanawake hupata Ovarian cyst,vivimbe kwenye mfuko wa mayai.

Kuna sababu hapo juu kama PID,kutopata UTE,infections kwenye uke hizi zinakuja athiri mwanamke anakuwa anapata taabu kwenye Kupata mimba

Kama hujapanga kupata mimba,tafadhari fuata njia ya uzazi wa mpango ya muda mrefu inayokufaa,achana na kumeza p2 kila mwezi.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Ushauri|Tiba|CheckIn 🩺🌡️ContactUs; +255758286584 or INBOX📩. For More Healthtips everyday Link In https://afyaclass.com Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...