Magonjwa
Madhara Ya Muingiliano Wa Rhesus Factor Kwa Ujauzito(Kwa Mama Mwenye Blood Group Negative Na Baba Positive) Hasa Katika Ujauzito Wa Pili
Madhara Ya Muingiliano Wa Rhesus Factor Kwa Ujauzito(Kwa Mama Mwenye Blood Group Negative Na Baba Positive) Hasa Katika Ujauzito Wa Pili
Kama tulivyoeleza kwenye makala mbali mbali zilizopita kuhusu makundi ya Damu kati ya Baba na Mama pamoja na umuhimu wake,
Moja ya vitu muhimu kufwatilia Wakati wa Ujauzito ni pamoja na Makundi ya damu(Blood groups)
Tuna makundi manne ya Damu yaani: A,B,AB, pamoja na O
Lakini kuna rhesus factor ambapo huweza kuwa POSITIVE au NEGATIVE
Hivo utakuta kila baada ya kufanya Vipimo vya Kujua group lako la Damu ni lazima uandikiwe hivi;
A+,A-,B+,B-,AB+,AB-,O+,O-
Hizi Positive na Negative ndyo majibu ya rhesus factor,
Wapo baadhi ya watu huchanganya hizi Positive na Negative kama Majibu ya Ukimwi(HIV/AIDS),
Hapana: hizi ni rhesus factor na sio majibu ya HIV.
Hapa nimeelezea baadhi ya Madhara ambayo huweza kutokea kama Mama mjamzito ana kundi lolote la damu rhesus factor Negative, Wakati Baba ana kundi lolote la Damu rhesus factor positive
1) Mtoto alieo tumboni kupungukiwa damu (Fetal anemia)
2) Mtoto kuvimba akiwa tumboni (oedema)
3) Mtoto kuvimba tumbo akiwa tumboni (ascitis)
4) Moyo wa mtoto kujaa maji akiwa tumboni (pericardial effusion)
5) Mapafu ya mtoto kujaa maji (pleural effusion)
6) Mtoto kufia tumboni (IUFD)
7) Mimba kuharibika (misacariage)
8) Mtoto kuzaliwa lakini hufariki ndani ya Muda mfupi, hasa kutokana na tatizo la kuishiwa na damu,kukosa hewa ya oxygen n.k
JE MAMA MWENYE HALI HII HUSAIDIWAJE?
Mama mwenye hali kama hii ni Lazima ahakikishe anapata SINDANO YA ANTI-D,
ambapo ataanza kuchoma Sindano ya ANTI-D Mara baada ya Ujauzito kufikisha wiki 28 au Miezi 7, na dose ya Pili kuchoma ndani ya Masaa 72 baada ya Kujifungua.
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.