Connect with us

Magonjwa

Maambukizi ya Dengue wakati wa ujauzito huweza kudhuru afya ya watoto wachanga

Avatar photo

Published

on

Maambukizi ya Dengue wakati wa ujauzito huweza kudhuru afya ya watoto wachanga:

Utafiti unaonyesha kwamba hata maambukizi madogo ya Dengue yanahusishwa na tatizo la kuzaa watoto wenye uzito mdogo na hatari ya kulazwa hospitalini.

Takwimu zinaonyesha Watoto ambao mama zao walikuwa na homa ya dengue wakati wa ujauzito wako katika hatari kubwa ya kuzaliwa na uzito mdogo na kuhitaji matibabu/huduma ya hospitali katika miaka yao mitatu ya kwanza ya maisha,

Watafiti wametaka dengue kuongezwa katika orodha ya magonjwa yanayowasumbua wajawazito, ambayo wanawake wanashauriwa kuchukua hatua za kuepuka kwa sababu ya hatari kwa watoto wao ambao hawajazaliwa.

Ugonjwa wa dengue wakati wa ujauzito ulisababisha ongezeko la asilimia 27% la hatari ya kulazwa hospitalini katika miaka mitatu ya kwanza ya maisha, na kuongeza kwa kiasi kikubwa gharama za matibabu(medical expenditures).

Dengue ni maambukizi ya virusi yanayosambazwa kwa kung’atwa na aina kadhaa za mbu aina ya Aedes, ambapo inatishia afya ya takriban nusu ya idadi ya watu duniani.

Ingawa visa vingi havina dalili yoyote, virusi hivyo vinaweza kusababisha ugonjwa wa homa kali, na mara kwa mara kifo, lakini bado kumekuwa na ushahidi mdogo wa kuhusisha matokeo mabaya zaidi kwa Watoto wanaozaliwa hadi sasa.

Watafiti katika Vyuo Vikuu vya Surrey na Birmingham nchini Uingereza walichambua rekodi za afya kwa wanawake na watoto wanaoishi katika jimbo lenye wakazi wengi kusini-mashariki mwa Brazili la Minas Gerais kati ya Mwaka 2011 na 2017, wakiunganisha takwimu za kuzaliwa, vifo, kulazwa hospitalini na maambukizi ya dengue kwa muda.

Utafiti huo uliochapishwa katika jarida la American Economic Journal: Applied Economics, uligundua kuwa maambukizi ya dengue ya wastani wakati wa ujauzito yalihusishwa na kuzaliwa kwa watoto wachanga wenye Uzito mdogo.

Athari hiyo ilijitokeza haswa kwa watoto wachanga walio katika kiwango cha chini mwisho kwenye kipimo yaani “lower end of the birth weight scale”, na ongezeko la asilimia 15%, 67%, na 133% katika matukio ya kuzaliwa kwa uzito wa chini(low birth weight) na Uzito wa chini sana(extremely low-birth weight). Hii inasikitisha kwa sababu tafiti za awali zimehusisha tatizo la Uzito mdogo kwa watoto wanaozaliwa na hali duni ya afya kwa muda mrefu,hali ya kijamii na hali duni ya kiuchumi.

Watafiti pia waligundua kuwa dengue wakati wa ujauzito ilisababisha ongezeko la asilimia 27% la hatari ya kulazwa hospitalini wakati wa miaka mitatu ya kwanza ya maisha, na iliongeza kwa kiasi kikubwa gharama za matibabu(medical expenditures).

Mwandishi mwenza wa utafiti huo Dk Martin Foureaux Koppensteiner katika Chuo Kikuu cha Surrey alisema: “Sasa kuna ushahidi wa kutosha juu ya madhara ya maambukizi ya dengue kwenye uzazi hasa wakati wa mtoto kuzaliwa. Hii Inasisitiza umuhimu wa kuongeza ufahamu, kuzuia, na kuchukua hatua zinazolengwa ili kupunguza athari za ugonjwa huu ulioenea kwa afya ya mama na mtoto.”

Alipendekeza kuwa homa ya dengue inapaswa kuongezwa kwenye orodha inayoitwa TORCH,

TORCH: ni Orodha ya maambukizi au magonjwa yanayohitaji kudhibitiwa na kuepukwa wakati wa ujauzito – Hii ni pamoja na maambukizi kama vile;

  • toxoplasmosis,
  • rubela,
  • VVU,
  • kaswende,
  • tetekuwanga,
  • Zika,
  • Pamoja na virusi vya herpes simplex.

” Kuweka homa ya dengue katika orodha hii,itahakikisha kwamba wajawazito wanafahamu hatari zinazotokana na maambukizi haya wakati wa ujauzito na wanaweza kuchukua tahadhari kama vile ya kutumia dawa za kuua wadudu,kujikinga n.k” alisema Dk Martin Foureaux Koppensteiner.

Ushauri|Tiba|CheckIn 🩺🌡️ContactUs; +255758286584 or INBOX📩. For More Healthtips everyday Link In https://afyaclass.com Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...