Connect with us

Utafiti

Hatari ya Mlipuko wa Surua,kwa watoto kukosa kinga dhidi ya ugonjwa wa surua

Avatar photo

Published

on

Hatari ya Mlipuko wa Surua,kwa watoto kukosa kinga dhidi ya ugonjwa wa surua

Janga la Uviko -19 lilitatiza utoaji wa chanjo za kawaida dhidi ya ugonjwa wa Surua duniani kati ya mwaka 2020 na 2021 na kuacha mamilioni ya watoto wengi katika nchi maskini, wakiwa hawana kinga dhidi ya ugonjwa huo.

Kulingana na data za Kituo vya Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa nchini Marekani (CDC), kufikia mwisho wa 2024, zaidi ya nusu ya nchi zote duniani zitakuwa katika hatari ya mlipuko wa Surua.

moja ya magonjwa ya kuambukiza, ambayo yanaweza kusababisha upofu, homa ya mapafu na hata kifo. 

>>Soma Zaidi hapa; Ugonjwa wa Surua,chanzo,dalili,kinga.

Wengi wa watu wanaokufa kutokana na mlipuko wa ugonjwa huo wa Surua ni watoto. Kabla ya kuanza kufurahia utoto wao, wanakufa kutokana na ugonjwa huu unaoweza kuzuilika kwa urahisi, anasema Abdirizak Ahmed,  mkurugenzi wa shirika la msaada la Save the Children mjini Jijiga nchini Ethiopia ambalo liliripoti kesi 10,000 za ugonjwa huo mwaka 2023, hii ikiwa idadi kubwa zaidi duniani baada ya Yemen, Azerbaijan, Kazakhstan na India. Takwimu hizi ni kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni, WHO.

Juhudi za Ahmed za kupambana na mripuko wa surua nchini Ethiopia zilipata pigo mwezi uliopita wakati wafanyakazi wenzake wawili walipopoteza watoto wao kutokana na ugonjwa huo, ambao umeibuka tena kutoka barani Afrika kuelekea India na Uingereza.

Watoto hao wote wa kiume walifariki kabla ya kufikisha miezi 13 ama 14 ya maisha yao, hali ambayo Ahmed anasema ni ya kusikitisha.

Watoto 12,000 wafa kwa surua, utapiamlo

Katika kile ambacho wataalamu wa afya wamekiita “kurudi nyuma zaidi katika kizazi kimoja”, nchi 51 – nyingi yao zikiwa barani Afrika – zilishuhudia  miripuko mikubwa na ya kutatiza ya ugonjwa wa Surua mwaka jana, hili likiwa ongezeko kutoka nchi 37 katika mwaka wa 2022 na nchi 22 mwaka 2021, huku hali hiyo ikitarajiwa kuendelea kuwa mbaya zaidi.

Kulingana na data za Kituo vya Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa nchini Marekani (CDC), kufikia mwisho wa 2024, zaidi ya nusu ya nchi zote -takriban 105 – zitakuwa katika hatari kubwa ya mripuko wa ugonjwa wa Surua.

Katika ujumbe wa msemaji wa CDC alioandikia kupitia barua pepe, kati ya nchi zinazokabiliwa na hatari, takribani nusu ni zile zenye mapato ya chini na ya kadri, huku watoto wakikabiliwa na hatari zaidi ya kupata ugonjwa huo.

Kwa kawaida, ugonjwa wa Surua husababisha homa kali, kikohozi na upele. Miongoni mwa wanawake wajawazito, ugonjwa huo huongeza hatari ya kuharibika kwa mimba na kuzaliwa mapema kwa mtoto.

Ugonjwa wa surua unaongezeka kufuatia wazazi kutowapa chanjo watoto wao

Ugonjwa wa surua unaongezeka kufuatia wazazi kutowapa chanjo watoto wao.

Hata hivyo, wataalamu wanasema kwa miaka mingi, ufanisi wa chanjo ya Surua umesababisha hali ya kuridhika na sasa idadi inayoongezeka ya wazazi katika nchi ambazo ugonjwa wa Surua ulikuwa umetokomezwa kwa muda mrefu, ikiwa ni pamoja na Marekani na Ulaya, wanachagua kutowapa chanjo watoto wao.

Mnamo mwezi Desemba, WHO ilisema kulikuwa na ongezeko la mara 30 zaidi la visa vya ugonjwa wa surua kote Ulaya.

Uingereza, ambayo ilikuwa imeshauangamiza ugonjwa huo mnamo 2017, sasa inajitahidi kudhibiti maambukizo yanayoongezeka kwa sababu ya kupungua kwa idadi ya chanjo inayotolewa.

DR Congo: Vifo kutokana na ugonjwa wa surua vyapindukia 6000

Imani katika umuhimu wa chanjo kwa watoto dhidi ya magonjwa sugu kama Surua na Polio ilipungua wakati wa janga hilo katika nchi 52 kati ya 55 zilizofanyiwa utafiti na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, mwaka 2023.

Niklas Danielsson, mtaalamu mkuu wa chanjo katika shirika la UNICEF, amesema habari potofu kuhusu chanjo za UVIKO- 19

huenda zimesababisha kushuka kwa imani katika chanjo nyingine.

Kulingana na WHO, Surua inaweza kuzuilika kwa dozi mbili za chanjo. Hata hivyo, watoto milioni 22 ulimwenguni kote walikosa dozi yao ya kwanza mnamo mwaka 2022 na wengine milioni 11 dozi yao ya pili, hii ikiwa hatua bora kidogo ikilinganishwa na mwaka uliopita.

Mashirika ya misaada na watalaamu wa afya wanasema kuwa mifumo ya afya barani Afrika iko hatarini haswa kutokana na ukosefu wa fedha na wafanyakazi, hasa katika nchi kama vile Ethiopia ambako migogoro, ukame, mafuriko na utapiamlo kunawafanya watoto kuwa katika hatari zaidi ya kuambukizwa magonjwa hatari.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...