Connect with us

Elimu&Ushauri

Chanzo cha rangi nyeusi kwapani na jinsi ya kuondoa

Avatar photo

Published

on

Chanzo cha rangi nyeusi kwapani na jinsi ya kuondoa

Wataalamu wa afya wasema fangasi na uchafu ndio visababishi vikubwa vya weusi kwapani.

Usafi na kuepuka matumizi ya vifaa vya kunyolea visivyo sahihi ni mbinu ya kuepukana na tatizo hilo.

Weusi kwapani? Ndio.  Ni jambo la aibu  kwa baadhi ya watu na hawapendi kulizungumzia suala hili hadharani.

Baadhi yao hulazimika kuvaa nguo zenye mikono mirefu kwa kuepuka sehemu hizo kuonekana.

“Kwa sisi wanawake weusi kwapani unatutesa, unashindwa hata kuvaa nguo za kuogelea kwa amani ukihofia kuaibika endapo watu wakikuona,” anasema Anaheri Richard mkufunzi wa kuogelea (swim coach) jijini Dar Es Salaam.

Ikiwa wewe ni mmoja wa wahanga wa tatizo hili makala hii ni kwa ajili yako ambapo tutaangazia chanzo na jinsi ya kuondoa weusi kwapani.

Fangasi ndio chanzo cha weusi makwapani

Daktari Zabron Mbatiya kutoka Hospitali ya Kairuki ya jijini Dar es Salaam anasema chanzo kikubwa cha weusi kwapani ni maambukizi ya fangasi wa ngozi wanaopendelea kukaa sehemu zenye joto na unyevu unyevu.

“Tatizo hili husababishwa na fangasi aina ya ‘candida’ ambao huota kwenye makwapa, chini ya matiti, sehemu ya ndani ya mapaja na ndani ya  mashavu ya uke,” amesema Dk Mbatiya.

Fangasi hao hujishikiza kwenye vitundu vya vinyweleo na kusababisha miwasho ambapo kadri mtu anavyojikuna ndivyo weusi unavyoongezeka katika sehemu hizo.

Mbali na uwepo wa fangasi, Meshack Mhalila, mtaalamu wa afya wa kujitegemea kutoka mkoani Mbeya anasema kunyoa kwa vifaa visivyo sahihi kama viwembe butu pamoja na uchafu huchangia makwapa kuwa meusi.

Mtaalamu huyo amesema baadhi ya watu hawajisafishi ipasavyo na kusababisha mlundikano wa uchafu sugu ambao mwisho hutengeneza rangi nyeusi.

“Wengine hawajisafishi vizuri, hayo maeneo hayasuguliwi kabisa hapo lazima kuwe na rangi nyeusi… pia wale wanaovaa nguo za kubana kwa muda mrefu wanaweza kupata tatizo hilo,” anasema Mhalila.

Sambamba na hayo wataalamu hao wa afya wamesema matumizi yaliyokithiri ya vidhibiti harufu (vipodozi) makwapani na sehemu nyingine za mwili yanachangia sehemu hizo kuwa nyeusi kutokana na wingi wa kemikali zilizopo.

Fanya haya kuepukana na weusi kwapani

Licha ya kwamba tatizo hilo linatibika ikiwa utatembelea vituo vya afya na kutumia dawa, zipo mbinu zitakazokusaidia kuepukana nalo.

Wataalamu wa afya wanasema ili kuepukana na weusi kwapani njia ya kwanza ni kuhakikisha usafi wa sehemu hizo mara kwa mara.

“Sehemu ambazo zina uchafu ndipo fangasi wanapenda kukaa hivyo ukijisafisha na kujiweka safi unapunguza uwezekano wa fangasi kuzaliana na kusababisha weusi,” amesema Dk Mbatiya.

Kunyoa kwapani kwa vifaa sahihi ni miongoni mwa njia itakayokusaidia kupunguza weusi kwapani. Picha | Popsugar.

Kunyoa kwapani kwa vifaa sahihi

Baadhi ya vifaa vinavyotumika kunyolea huwa ndio kisababishi cha weusi kwapani. Wataalamu hao wa afya wanasema kutumia vifaa bora vya kunyolea kunaweza kusaidia.

“Watu wananyoa kwa kiwembe, hali lazima iwapate hususani akiwa amenyoa kwa muda mrefu,” amesema Mhalila.

Epuka matumizi yaliyokithiri ya vidhibiti harufu (vipodozi)

Matumizi yaliyokithiri ya vipodozi vinavyodhibiti harufu maarufu kama ‘deodorant na spray’ yanayoweza kusababisha ngozi ya kwapa kuwa nyeusi.

Mhalila anasema vipodozi hivyo huzuia mchakato wa utoaji taka mwili kwa njia ya jasho na kusabisha maeneo hayo kuwa meusi.

“Vipodozi vyenye viambata vya ‘aluminium salt’ husababisha seli za ngozi kufa ndio maana unakuta maeneo hayo ni meusi ikimaanisha kuwa maeneo hayo hakuna uhai,” ameongeza Mhalila.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...