Connect with us

Elimu&Ushauri

WATANZANIA wengi wana uzito uliopitiliza (mabonge) kutokana na kutozingatia ulaji unaofaa

Avatar photo

Published

on

WATANZANIA wengi wana uzito uliopitiliza (mabonge) kutokana na kutozingatia ulaji unaofaa huku takwimu zikionyesha ni watu saba pekee nchini katika 100 wanaozingatia mlo kamili.

Takwimu Aidha, Mtanzania mmoja katika watatu, ana uzito uliokithiri na watu wenye elimu na uhakika wa kipato ndio waathirika zaidi.

Mkurugenzi Msaidizi wa Magonjwa Yasiyoambukiza (NCD) katika Wizara ya Afya, Dk. Omary Ubuguyu, ameyasema Dar es Salaam wakati wa kongamano la kwanza la uimara wa afya kwa ajili ya biashara endelevu, lililoandaliwa na Mtandao wa Global Compact Tanzania (GCNT) na kukutanisha wadau wa sekta binafsi.

“Katika maeneo machache ambayo tunafanya vizuri ni kwenye mazoezi kwa sababu kumekuwa kwa mfano na marathoni nyingi. Hatufanyi vizuri kabisa katika masuala ya ulaji bado ni watu saba katika 100 ambao wanazingatia ulaji unaofaa.

“Suala la uzito na unene kupita kiasi pia hali imezidi kuwa mbaya, zamani ilikuwa ni katika kila watu wanne, mmoja anauzito uliokithiri, sasa hivi ni mtu mmoja katika kila watu watatu ana uzito au unene uliokithiri, kwa hiyo hatufanyi vizuri katika eneo hili,” amesema.

Dk. Ubuguyu amesema idadi ya watu ambao wanatumia pombe nchini imepungua lakini matumizi yameongezeka.

“Bahati mbaya kuliko zote vijana wanaathirika zaidi kuliko rika linguine lolote na wanawake wanaathirika zaidi kuliko wanaume katika haya tunayoyazungumza. Watu  wenye umri mdogo na wanawake ndio wako kwenye hatari zaidi,’ amesema.

Amesema utafiti unaonyesha kwamba magonjwa yasiyoambukiza kama saratani, kisukari, figo na shinikizo la juu la damu, yanaathiri zaidi watu wenye kipato cha chini, lakini ni kinyume chake katika baadhi ya nchi kama Tanzania ambako waathirika wakubwa ni wasomi na wenye uhakika wa kipato.

“Katika jamii mfano za wafanyakazi ndio wanaotumia vyakula vya viwandani zaidi, pombe zaidi, ndio watu wenye fursa ya kununua soda na vitu vingine ambavyo vinaathiri afya,” amesema.

Dk. Ubuguyu amesema wafanyakazi wanaathiri zaidi kutokana na mtindo wa maisha kwa kuwa hawana nafasi ya kupata chakula bora kwa kuwa wananunua vyakula wasivyojua namna vilivyoandaliwa na pia hawapati nafasi ya kufanya mazoezi.

“Kama taifa tuna mzigo mkubwa sana wa magonjwa yasiyoambukiza. Tukizungumzia gharama tunazozipata katika matibabu kwa mfano Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), vitu vikubwa vinavyouelemea ni kutibu magonjwa kama saratani, matatizo ya figo, shinikizo la juu la damu, kiharusi na kisukari. Hili ndilo janga kubwa katika taifa letu,” amesema.

Dk. Ubuguyu amesema serikali inapata matumaini inapoona jumuiya ya wafanyabishara na mashirika binafsi zikikutana na kujadili namna ya kukabili janga hilo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Global Compact Tanzania (GCNT), Mardha Macatta-Yambi, amezitaka kampuni binafsi na wawekezaji kuweka mazingira ya kuhakikisha afya za wafanyakazi ni nzuri, ili kukabili NCD.

Amesema wadau wote wanapawa kuunganisha nguvu kwa kuwa ongezeko la magonjwa hayo linaathiri biashara na uchumi wa nchi.

“Pamoja na serikali kuweka sera na mikakati ya kukabili magonjwa haya, makampuni yana nafasi kubwa kuhakikisha kwamba wafanyakazi wanakuwa na uelewa wa kutosha kuhusu afya zao kwa kuwa hawa ndio nguvu kazi ya kuwatengenezea faida kwenye kile walichowekeza,” amesema.

Katika kongamano hilo, GCNT na taasisi ya ImpactAfya, wametia saini makubaliano ili kuendelea kutoa elimu ya uimara wa afya sehemu za kazi na kuwakumbusha wafanyakazi na umma kwa ujumla, umuhimu wa kuwa na afya njema ili kupunguza mzigo wa matibabu.

Amewataka Watanzania kuhakikisha wanafanya mazoezi kila siku, kula vyakula vyenye virutubisho, kupima afya mara kwa mara na kubadili mtindo wa maisha unaochochea NCDs.

Kongamano hilo liliongozwa na kaulimbiu ya kupunguza NCDs kwa ajili ya biashara endelevu na kuhudhuriwa na madaktari, wafamasia na wakurugenzi wa kampuni na taasisi binafsi.

Mlo kamili unaopaswa kuzingatiwa kila siku na aina yake kwenye mabano ni wanga (ugali, wali au ndizi),  mboga (kabichi, spinachi, mchicha au figiri) protini (nyama, samaki, kunde, njegere na maharage), matunda (embe, chungwa, papai au tikiti), vitamini (karanga au korosho) na maji ya kutosha.

MASWALI&MAJIBU kuhusu afya| Link...👇

https://afyaclass.com/afyaforums

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 weeks ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa1 month ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa1 month ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake3 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa5 days ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa6 days ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa2 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa2 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...

Magonjwa2 weeks ago

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho Kuna magonjwa mengi yanayohusiana na macho, mengi yanatibika lakini kuna baadhi ya magonjwa...

Magonjwa3 weeks ago

Kunguni husababisha ugonjwa gani

Kunguni husababisha ugonjwa gani Kunguni ni wadudu wadogo ambao chakula chao kikubwa ni damu, wadudu hawa huweza kunyonya damu kutoka...

Magonjwa4 weeks ago

je ugonjwa wa pumu unaambukiza

je ugonjwa wa pumu unaambukiza? Hili ni Swali ambalo watu wengi huuliza,hata kwenye page za afyaclass, kwa kuliona hilo, tumeona...

Magonjwa1 month ago

Dalili za mwanzo za ugonjwa wa ini

Dalili za mwanzo za ugonjwa wa ini Ugonjwa wa ini (hepatic disease) mara nyingi huanza taratibu na dalili zisizo wazi,...