Connect with us

News

Soma hapa Sababu za watoto kuwa na uzito mkubwa

Avatar photo

Published

on

Soma hapa Sababu za watoto kuwa na uzito mkubwa

Uzito sahihi wa mtoto wako unaotakiwa ni ule wa namba za umri wake ukazidisha mara mbili ukajumlisha na nane (yaani miaka 4×2+8= 16), zaidi ya hapo ni kiashiria cha uzito uliokithiri.

Imekuwa ni kawaida kwa wazazi wengi kufurahia hali ya watoto wao kuwa na uzito mkubwa, hata hivyo wataalamu wa afya wanasema ni uzito uliopitiliza au ni kiashiria cha homoni za mtoto kutokuwa sawa.

“Mtoto mwenye umri wa miaka minne anapaswa kuwa na uzito wa kilogramu 16 na mwenye umri wa miaka sita anapaswa kuwa na uzito wa kilogramu 22, hii haijalishi anaishi Ulaya au Tanzania, hii ndiyo kanuni ya afya,” alisema Mtaalamu wa Afya ya Jamii, Dk Ali Mzige.

Uzito wa kuzaliwa

Licha ya wale wanaonenepa kutokana na kutokuwa na mpangilio mzuri wa chakula, kuzaliwa na uzito mkubwa kupita kiasi (fetal macrosomia) au kile kinachojulikana kama uzito wa juu wa kuzaliwa ni hali ambayo mtoto anazaliwa na uzito wa kilogramu 4 au zaidi.

Daktari bingwa wa magonjwa ya watoto kutoka Idara ya Mafunzo na utafiti na magonjwa ya ndani Hospitali ya Kanda ya Rufaa Mbeya, Ernest Winchislaus anasema hali hiyo inaweza kuwa na athari kubwa kwa afya ya mtoto na mama na mara nyingi inahitaji ufuatiliaji wa karibu na matibabu.

Anataja sababu zinazochangia watoto kuzaliwa na uzito mkubwa ni pamoja na maumbile, mlo wakati wa ujauzito na hali ya kiafya ya mama.

“Hapa tunachunguza baadhi ya sababu na athari za watoto kuzaliwa na uzito mkubwa kupita kiasi. Tutaangalia ugonjwa wa kisukari cha mimba, wanawake wenye tatizo hilo wako katika hatari ya kumzaa mtoto mwenye uzito mkubwa,” anasema.

Dk Winchslaus anasema kisukari cha mimba husababisha kiwango kikubwa cha sukari katika damu ya mama, ambayo inaweza kusababisha ukuaji wa kichanga kuzidi kupita kawaida, wanawake wenye unene kupita kiasi au wenye uzito mkubwa kabla ya ujauzito wako katika hatari kubwa ya kumzaa mtoto mwenye uzito mkubwa.

“Hali hii inaweza kuhusishwa na tatizo katika kemikali ya kuchakata sukari mwilini ambayo inaweza kuchochea ukuaji wa kichanga kwa kiasi kikubwa,” anasema.

Maumbile

Dk Winchslaus anasema uzito wa mtoto unaweza kuathiriwa na mambo ya maumbile, ikiwa ni pamoja na jeni zinazohusiana na ukuaji wa kichanga.

Watoto ambao wazazi wao wana uzito mkubwa wanaweza kuwa na hatari kubwa ya kuzaliwa na uzito mkubwa.

“Baadhi ya matatizo ya kijenetikia katika mwili wa kichanga yanaweza pia kuchangia tatizo la uzito mkubwa, baadhi ya haya yanafahamika kitaalamu kama Beckwith-Wiedemann Syndrome, Sotos syndrome, Fragile x syndrome,” anasema.

Anataja historia ya watoto wenye uzito mkubwa katika mimba za awali, akisema tafiti zinaonyesha ikiwa hapo awali umeshazaa mtoto mwenye uzito mkubwa, una hatari kubwa ya kuzaa mtoto mwingine mwenye uzito mkubwa.

“Pia, ikiwa wewe mwenyewe ulizaliwa na uzito mkubwa zaidi ya kawaida, una uwezekano mkubwa zaidi wa kuzaa mtoto mwenye uzito mkubwa pamoja na kupitiliza kwa tarehe ya matazamio ya kujifungua,” anasema.

Dk Winchslaus anasema ikiwa ujauzito unazidi kwa zaidi ya wiki mbili baada ya tarehe ya kutarajia kujifungua, mtoto ana hatari kubwa ya kuzaliwa na uzito mkubwa, lakini pia huchangiwa na umri wa mama mjamzito.

Anasema wanawake wenye umri zaidi ya miaka 35 wana uwezekano mkubwa wa kupata watoto wenye uzito uliozidi.

Daktari bingwa wa watoto, Deashisaria Rimoy anasema mambo mengi yanaweza kusababisha mtoto kuzaliwa na uzito mkubwa au mtoto akazaliwa kawaida na kuendelea kukua katika uzito mkubwa zaidi.

“Kuna vinasaba, homoni, pia kuna uwezekano mtoto aliyezaliwa na uzito wa kawaida akaanza kuongezeka uzito, yanayochangiwa na kupangilia mlo, mtindo wa maisha, magonjwa, masuala ya kisaikolojia kama sonona wanakula sana na kunenepa, pia baadhi ya dawa hunenepesha,” anasema Dk Deashisaria.

Via:Mwananchi

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...