Connect with us

Hali ya hewa

Kimbunga Hidaya na kinachoendelea kwa sasa

Avatar photo

Published

on

Kimbunga Hidaya na kinachoendelea kwa sasa

Pwani ya Afrika Mashariki hususan Tanzania inatazamiwa kukumbwa na Kimbunga Hidaya ambacho kitasababisha mvua kubwa.

Mapema wiki hii Mamlaka ya hali ya Hewa Tanzania (TMA) ilitangaza kuwepo kwa mgandamizo mdogo wa hewa ambao ulitarajiwa kutawala na kusababisha mvua kubwa na upepo mkali katika mikoa mitano nchini ikiwa ni pamoja na Mtwara, Dar es Salaam, Lindi, maeneo ya Tanga, Morogoro, visiwa vya Pemba na Unguja pamoja na maeneo jirani.

Kimbunga Hidaya kilianza kujitengeza siku ya Jumatano kusini mwa Bahari ya Hindi kuelekea mashariki mwa Tanzania na kaskazini-mashariki mwa visiwa vya Komoro.

Kwa mujibu wa TMA, kufikia sasa mienendo ya mifumo ya hali ya hewa baharini bado inaonesha uwezekano mkubwa wa Kimbunga Hidaya kuendelea kusogea karibu na pwani ya Tanzania na kuendelea kuwepo hadi Jumatatu, Mei 6 2024.

Kulingana na mamlaka hiyo, kimbunga hicho kinaendelea kuimarika na kwamba hadi kufikia usiku wa kuamkia leo kasi yake ilikuwa imeimarika na kufikia kilomita 110 kwa saa.

Taarifa ya mamlaka hiyo aidha ilisema kwamba kimbunga hicho kitaendelea kuimarika na kuwa kikubwa zaidi katika saa 24 zijazo.

Tahadhari zilizotolewa na TMA?

Serikali imewashauri wananchi kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri wa hali ya hewa ili kupata ushauri na mwongozo wa wataalamu katika sekta husika kwa lengo la kujikinga na athari zinazoweza kuibuka.

TMA imesema kwamba ongezeko la mvua na upepo mkali utakaoambatana na mawimbi makubwa baharini vinatarajiwa kusambaa katika maeneo mengi ya ukanda wa pwani kuelekea tarehe 4 hadi 6 mwezi Mei 2024.

Kutokana na hilo, TMA imetoa tahadhari kwa wananchi katika maeneo husika na wote wanaojihusisha na shuguli mbalimbali baharini .

Vilevile Mamlaka hiyo imewataka Watanzania kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri wa hali ya Hewa.

Kenya imesema nini?

Serikali ya Kenya siku ya Alhamisi tarehe 2, Mei ilionya kwamba eneo la Pwani huenda likakumbwa na kimbunga Hidaya ndani ya siku chache zijazo kutokana na mvua kubwa inayoshuhudiwa kwa sasa kote nchini humo.

Onyo hilo lilitolewa baada ya kikao maalum cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Alhamisi kujadili hatua za ziada za kukabiliana na athari mbaya zinazoendelea za mafuriko, maporomoko ya udongo na maporomoko ya ardhi.

Baraza la Mawaziri lilifahamishwa kuhusu utabiri wa hali ya hewa kwa muda wa miezi mitatu ijayo, ambao ulionyesha kuwa mvua za wastani hadi juu ya wastani zitaendelea kunyesha katika maeneo yote ya nchi.

Kimbunga ni nini?

Kulingana na Shirika la Hali ya Hewa Ulimwenguni, kimbunga cha kitropiki – ni dhoruba inayozunguka kwa kasi ambayo huanza juu ya bahari ya kitropiki.

Kimbunga cha Kitropiki katika Bahari ya Hindi kina nguvu zaidi kuliko dhoruba ya kitropiki.

Ilipewa jina la ‘Hidaya’ na Meteo France La Reunion, huku mifano ya utabiri ikiifuatilia magharibi-kaskazini-magharibi kati ya Mei 2-4, 2024.

Kimbunga cha mwisho kuikumba Tanzania ilikuwa mwaka 1952 (wakati huo koloni la Tanganyika) na kilitua mkoani Lindi katika pwani ya kusini ya Tanzania.

Kimbunga cha mwisho kuikumba Zanzibar kilikuwa mwaka 1872 na athari zake zilifika mpaka upande wab ara katika eneo la Bagamoyo, kaskazini mwa Dar Es Salaam.

Ikiwa Kimbunga Hidaya kitatua kwa kasi, itakuwa ni mara ya kwanza katika historia kwa Dar Es Salaam kukumbwa na kimbunga.

Katika miaka ya hivi karibuni, Tanzania pia ilikuwa katika ya kupigwa na vimbunga vingine viwili, mwaka 2019 Kimbunga Kenneth kilitabiriwa kupiga mkoa wa Mtwara lakini hata hivyo kilibadili mwelekeo na kutua nchini Msumbiji.

Mwaka 2021 ilitolewa tahadhari ya Kimbunga Jobo lakini hata hivyo kilipunguza makali na hakikusababisha maafa yeyote makubwa.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...