Connect with us

blogupdates

Wakunga ni matumaini kwa wajawazito na watoto wachanga

Avatar photo

Published

on

Yemen: Wakunga ni matumaini kwa wajawazito na watoto wachanga licha mzozo na janga la tabianchi

UNFPA ilikarabati kituo cha afya cha Shahir mwaka wa 2021 kwa kuongeza dawa na vifaa vya matibabu, pamoja na makumi ya wakunga waliofunzwa na sasa wanatoa huduma mbalimbali za kina.

Mona alipoanza kufanya kazi ya ukunga katika kituo cha afya mtaani anapoishi miaka 30 iliyopita, alikuwa wa kwanza katika jimbo la Hadramout nchini Yemen.

“Wakati huo, eneo letu lilikuwa nyuma sana katika huduma za afya ukilinganisha na ulimwengu wa sasa,” aliliambia shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi, UNFPA. Kwa sasa Mona ni kiongozi wa idara ya wataalam wa ukunga katika kituo cha afya cha Shahir huko Hadramout.  Aliielezea jinsi jamii yake ilivyokuwa masikini, kukosa shule, vituo vya matibabu na wahudumu wa afya.

“Wanawake walikumbana na ujauzito bila huduma au ufuatiliaji unaofaa. Licha ya nia njema ya mkunga wa jadi, alikumbwa na vikwazo vya rasilimali,” aliongeza Mona. “Huduma nyingi za uzazi zilikumbwa na matatizo. Haikuwezekana kufika hospitali iliyopo mjini kutokana na gharama, usafiri, na kutokuwepo kwa ufahamu wa kutosha.”

Fatima, si jina lake halisi, ni mgonjwa katika kituo cha afya anakofanya Mona, alithibitisha maelezo haya ya hali ilivyokuwa awali: “Uhai kwa mama na mtoto ulitegemea bahati tu”.

Yemen ina mojawapo ya viwango vya juu zaidi vya vifo vya uzazi duniani, na ni kituo kimoja tu kati ya vitano vinavyofanya kazi kwa sasa kinatoa huduma za afya ya uzazi na watoto wachanga.

Yemen ina viwango vya juu vya vifo vya wajawazito

Yemen ina mojawapo ya viwango vya juu zaidi ya vifo vya akinamama duniani, na ni kituo kimoja tu kati ya vitano kinachotoa huduma za afya ya akinamama wanaojifungua . Takribani watu milioni 17.8 wanahitaji msaada wa huduma za afya, kati yao wakiwa ni wanawake milioni 5.5 wanaohitaji huduma za afya ya uzazi, mwaka huu.

Baada ya kumaliza shule, Mona alipata hamasa ya kubadilisha hali hiyo na akajisajili katika mafunzo ya ukunga katika mji jirani wa Mukalla. Mara tu kituo cha afya cha Shahir kilipofunguliwa kitongojini mwake, hakusita kuomba kazi.”Licha ya ufadhili mdogo na wafanyakazi wachache, tulipigania kwa udi na uvumba ustawi wa wanawake wetu.”

Wakiwa msingi wa huduma za afya za uzazi na jinsia katika jamii, wakunga wana umuhimu mkuu kwa kufanikisha huduma za afya katika mazingira yenye migogoro, hususan kwa walio katika mazingira magumu zaidi.

Ukosefu wa usawa katika mabadiliko ya tabianchi

Mona alikumbuka siku ya kutisha mwaka 2015, wakati kimbunga Chapala kilipiga Yemen mapigano yalipokuwa yakianza. Yeye pamoja na timu kutoka kituo afya anakofanya kazi, alisema, “tulivuka maeneo hatari kwa miguu ili kufikia watu waliokuwa katika madhila.”

Licha ya upepo mkali na ukosefu wa umeme , “wazo la maisha ya watu watatu yaliyokuwa hatarini, yaani mwanamke aliyekuwa katika maumivu ya kujifungua mapacha, lilichochea azimio letu na tuliwafikia kwa wakati.”

Wakati majanga ya tabianchi yanapotokea au mzozo unapoibuka, wakunga mara nyingi huwa wa kwanza kutoa msaada, ikiashiria njia moja yenye ufanisi zaidi ya kuzuia vifo vinavyoweza kuzuilika vya kina mama. Utafiti unaonyesha kuwa janga la tabianchi huleta tishio la kipekee kwa wanawake na wasichana, kwani majanga haya yanaweza kusababisha matatizo ya ujauzito na yanaongeza hatari kama mtoto kuzaliwa njiti au mimba kuharibika.

Huduma za mama na mtoto Yemen sasa ni bure

Kwa ufadhili kutoka Muungano wa Ulaya (EU), UNFPA iliimarisha kituo cha afya cha Shahir mwaka 2021 kwa kukipatia dawa, vifaa vya  matibabu na kufadhili mafunzo kwa wafanyakazi wa afya. Tangu wakati huo, viwango vya vifo vya akinamama wajawazito katika eneo hilo vimepungua. Hii ni kwa sababu  wakunga waliofundishwa sasa wanatoa huduma kamili – ikiwa ni pamoja na elimu ya afya ya uzazi na huduma za upasuaji kwa wajawazito. Wana gari la kubebea wagonjwa, chumba cha upasuaji kilichojaa vifaa, na dawa zinazotolewa bure.

“Baada ya uharibifu kutokana migogoro na majanga ya tabianchi, ilikuwa kama ndoto,” alisema Mona. “Familia katika eneo hili, watu waliotawanywa wakikimbia mapigano na mafuriko, waliweza kupata faraja hapa.”

Mona alipoanza kufanya kazi kama mkunga katika kituo cha afya cha eneo lake miaka 30 iliyopita, alikuwa wa kwanza katika Jimbo la Hadramout la Yemen.

Sababu za uwekezaji: Idadi ya wakunga inapungua

Tangu mwanzo wa 2024, UNFPA imewafikia zaidi ya watu 350,000 nchini Yemen na kuwapa huduma za dharura za afya, ulinzi na maarifa ya uzazi na jinsia, pamoja na kuunga mkono zaidi ya vituo 100 vya afya.

Wakunga ni sehemu muhimu ya huduma hii, wakiwa  watunzaji wenye ufahamu wa kitamaduni,  na viongozi wa jamii wanaotoa msaada wa dharura. Lakini dunia imepungukiwa na wakunga takriban milioni moja: Kutokuwepo kwa dhamira ya kimataifa ya kuwekeza katika mafunzo yao, maendeleo na uungaji mkono kunapunguza uwezo wao na kuwaweka wanawake na wasichana wanaowategemea katika hatari.

Mazingira  ya kazi kwa wakunga ni dhalili

Kama Mona, wakunga wengi wanakabiliwa na mazingira magumu ya kazi, malipo duni na ukosefu wa maendeleo ya kazi – yote haya yakisababisha upungufu wa kimataifa. Ilhali utafiti wa UNFPA unaonyesha kuwa kuongeza idadi ya wakunga kwa asilimia 25 kunaweza kuokoa zaidi ya maisha milioni 2 kila mwaka ifikapo 2035.

Leo, Mona anakaribia kustaafu, lakini anasema amehisi faraja kulikabidhi kwa mwingine, jukumu la kituo chake cha afya. “Ni timu ya wakunga walio na maarifa ya hali ya juu sana, wataalamu, walio na uwezo wa kuongoza mustakabali wa huduma za afya ya uzazi.”

Karibu AfyaUpdates Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In https://afyaclass.com  Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa2 days ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...