Connect with us

News

Mafuriko yaathiri kaya 29,510 watu 125,668, Morogoro kaya 12,824 watu 51,491 na Mbeya kaya 27, 000 watu 96,000.

Avatar photo

Published

on

SERIKALI imesema wananchi 273,159 hawana makazi kutokana na mvua inayoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini.

Kadhalika, viongozi wa dini wataondoka leo na treni ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam kuelekea Dodoma kwa ajili ya kufanya maombi na dua ya kuliombea taifa kesho.

Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Mobhare Matinyi, amesema jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Alikuwa akizungumzia mafuriko, Muungano na safari ya majaribio ya treni ya kisasa (SGR).

Amesema idadi ya walioathirika kwa Mkoa wa Pwani ni

kaya 29,510 watu 125,668, Morogoro kaya 12,824 watu 51,491 na Mbeya kaya 27, 000 watu 96,000.

Katika maeneo ya Rufiji mafuriko yameanza kupungua kutokana na mvua kupungua katika baadhi ya mikoa ambayo mito yake huingiza maji katika Bonde la Rufiji.

Matinyi amesema kutokana na athari hizo za mvua walianzisha makazi ya muda na hadi sasa kuna kambi sita zenye waathirika 2,883 kwa Mkoa wa Pwani yenye kaya 29,510 zilizoathirika.

Amesema mvua hiyo imeathiri miundombinu ya barabara, vituo vya afya, shule, nyumba, mifumo ya maji na mashamba 152,956. 24 yenye mazao ya chakula.

Aidha, amesema misaada inaendelea kupelekwa katika mikoa ya Pwani, tani 700 za chakula, mafuta ya kula lita 7,880, vyandarua 2,260, mablanketi 1,290 na vifaa vingine ikiwamo mahema 26, magodoro 1,258, mafuta ya petroli lita 3,000 na dizeli 2,900.

Matinyi amesema mahitaji mengine kwa Mkoa wa Pwani ni boti mbili zaidi, umeme wa nguvu za jua, magodoro 2,000, vitanda 150, matangi 50 ya lita 5,000, mahema makubwa manne na madogo 10, mafuta ya petroli lita 100,000 na dizeli 50,000.

“Misaada inaendelea kuja na wahisani wanaombwa kuelekeza misaada Wilaya ya Kibiti ambapo hadi sasa kumekuwa na uhaba wa misaada kutokana na mingi kupelekwa Rufiji,” amesema Matinyi.

Amesema kwa Mkoa wa Morogoro kuna jumla ya kata 50 zilizoathirika na mafuriko na watu 78 waliokolewa na serikali. Sasa kuna kambi sita za waathirika zenye watu 1,500 na Mlimba kuna waathirika 1,365, Ifakara 135 zilizopo halmashauri mbili za Wilaya ya Kilombero.

Alisema watu wote waliopata mafuriko wapo katika makambi wanahudumiwa na serikali kwa kupewa chakula, makazi, tiba, maji na usalama.

Matinyi amesema tathimini ya mafuriko ya mvua inaendelea kufanywa na watatoa taarifa ikiwamo idadi kamili ya vifo vilivyotokana na mafuriko ya mvua.

Aidha, amesema viongozi wa dini, watendaji wa serikali, watumishi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) na waandishi wa habari baada ya kumaliza ibada kesho watapanda treni hiyo majira ya saa nane mchana na kuwasili Dar es Salaam majira ya saa moja usiku.

Amesema treni hiyo ipo katika majaribio, na isije kuonekana imetumia muda mrefu kusafiri. “Hizi ni shughuli za majaribio mwendokasi sio kipimo cha kazi haya ni majaribio.”

Amesema hadi sasa wameshapokea mabehewa ya treni ya kisasa 65 na vichwa tisa “kipande cha Dar es Salaam hadi Morogoro kimekamilika kwa asilimia 98.9 na kipande cha Morogoro kwenda Dodoma kimekamilika kwa asilimia 96.1.”

Amesema nchi inaadhimisha miaka 60 ya Muungano na kumekuwa na matukio mbalimbali ya kuzindua mradi, tukio kubwa linalofuata Aprili 22, mwaka huu jijini Dodoma ni kuliombea taifa na mgeni rasmi ni Makamu wa Rais, Dk. Philip Mpango.

Amesema wananchi wataanza kuingia katika uwanja kuanzia saa 12 asubuhi kutakuwa na burudani mbalimbali ikiwamo kwaya na shughuli la kuliombea taifa itaongozwa na viongozi wa dini.

Amesema tukio jingine kubwa ni Aprili 24, mwa huu kutakuwa na uzinduzi wa kitabu cha miaka 60 ya historia ya Makamu wa Rais iliyoanzishwa baada ya Muungano kutokea.

Aidha, amesema Aprili 25, majira ya saa tatu Rais Samia Suluhu Hassan, atalihutubia taifa kutoa ujumbe wa maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano saa sita kamili usiku, mikoa ya Arusha, Dodoma, Dar es Salaam, Geita, Mbeya, Mwanza na Zanzibar kutakuwa na urushwaji wa fataki.

Amesema Aprili 26, kilele cha shughuli hizo zitafanyika katika kiwanja cha Uhuru na mgeni rasmi atakuwa Rais Samia.

Taifa linatarajia kuwa na wageni kutoka mataifa ya jirani na marafiki katika siku hiyo.

MASWALI&MAJIBU kuhusu afya| Link...👇

https://afyaclass.com/afyaforums

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 weeks ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa1 month ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa1 month ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake3 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa5 days ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa6 days ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa2 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa2 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...

Magonjwa2 weeks ago

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho Kuna magonjwa mengi yanayohusiana na macho, mengi yanatibika lakini kuna baadhi ya magonjwa...

Magonjwa3 weeks ago

Kunguni husababisha ugonjwa gani

Kunguni husababisha ugonjwa gani Kunguni ni wadudu wadogo ambao chakula chao kikubwa ni damu, wadudu hawa huweza kunyonya damu kutoka...

Magonjwa4 weeks ago

je ugonjwa wa pumu unaambukiza

je ugonjwa wa pumu unaambukiza? Hili ni Swali ambalo watu wengi huuliza,hata kwenye page za afyaclass, kwa kuliona hilo, tumeona...

Magonjwa1 month ago

Dalili za mwanzo za ugonjwa wa ini

Dalili za mwanzo za ugonjwa wa ini Ugonjwa wa ini (hepatic disease) mara nyingi huanza taratibu na dalili zisizo wazi,...