Connect with us

News

ZAIDI ya kaya 2,500 katika Kata ya Muhoro, wilayani Rufiji, mkoani Pwani zimeathiriwa na mafuriko

Avatar photo

Published

on

ZAIDI ya kaya 2,500 katika Kata ya Muhoro, wilayani Rufiji, mkoani Pwani zimeathiriwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini.

Imeelezwa kuwa mafuriko hayo yamesababisha zaidi ya wananchi 10,000 kukosa mahali pa kuishi.

Diwani wa Muhoro, Abdul Chobo, akizungumza na Nipashe kwa simu jana, alisema mafuriko hayo yamewaacha katika hali ngumu kwa kuwa wengi wao hawana mahali pa kushi, huku mali na mashamba yao yakiharibiwa na maji.

Alisema kata yake ina vijiji sita na vitongoji 27. Kati ya vitongoji, viwili ndivyo havijakumbwa na maafa, lakini vilivyosalia vimeathiriwa.

Alisema wananchi waliokosa makazi kutokana na mafuriko ni wengi, wakihifadhiwa shuleni na wengine kupata hifadhi kwa ndugu.

“Kuna baadhi ya shule za msingi zimezingirwa na maji. Kwa mfano, Shule ya Msingi Muhoro imefungwa na nyingine wataalamu wanaendelea kufanya tathmini kuona kama zitafungwa au la.

“Kuna watoto wa sekondari wanaohitaji kuvuka maji ili wafike shuleni na kurudi majumbani, lakini wameshindwa kutokana na mafuriko. Wananchi wengi wamepoteza mazao, mashamba na mifugo yao,” alisema diwani huyo.

Chobo alisema kuwa awali Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) ilitahadharisha na kuwataka kuchukua hatua za kuhama, lakini wengine walipuuza ingawa kuna wachache waliochukua hatua na wameepuka madhara hayo.

Alisema kutokana na mvua ilivyokuwa inanyesha kwa wingi, walitarajia kupata mafuriko hayo tangu Desemba mwaka jana, lakini kuwapo Mradi wa Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere (JNHPP), kumesaidia kuzuia athari zaidi.

Hata hivyo, kuna dhana kwamba kufunguliwa kwa milango ya bwawa hilo kumesababisha hali inayoshuhudiwa sasa Rufiji.

“Hatuwezi kusema bwawa limesababisha mafuriko, si mara ya kwanza kutokea. Mara ya mwisho yalitokea mwaka 2020. Je, kulikuwa na bwawa? Je, na yale yaliyotokea mwaka 1978 na 1998 yalisababishwa na bwawa? Kwahiyo, bwawa si sehemu ni matokeo ya mvua kubwa na asili ya Rufiji,” alisema.

Diwani huyo alisema kilio kikubwa kwa sasa ni chakula na makazi mengine ya dharura, ili waliothiriwa wapate mahali pa kujisitiri huku wakisubiri hatua za serikali.

Pia aliomba huduma za afya zisogezwe haraka walioko wananchi hao ili kuepuka magonjwa ya mlipuko, akifafanua kwamba kutokana na mafuriko hayo, vyoo vingi vimezibuka na hivyo wanakijiji wengi wapo katika hatari ya kupata magonjwa ya mlipuko.

Alipoulizwa kuhusu hatua zilizochukuliwa na serikali mpaka sasa, diwani huyo alisema kuwa kwa mujibu wa mkuu wa wilaya, ofisi ya waziri mkuu imetoa mahindi tani 20 na wahisani mbalimbali wameanza kuchangia misaada ya chakula.

“Serikali, viongozi wa chama, wilaya na mkoa wamefika, timu za wataalamu wa takwimu na sasa mkuu wa wilaya anaendesha kikao kuona kinachopatikana kinawafikia walengwa,” alisema.

Mwenyekiti wa Kijiji Cha Muhoro Magharibi ambacho kimeathiriwa na mafuriko hayo, Amina Mnyimwa aliomba serikali ipeleke msaada wa chakula haraka.

Alisema tani zinazohitajika ni nyingi kwa kuwa walioathirika na mafuriko katika kata hiyo ni zaidi ya 16,000.

“Watu wakipata chakula watatulia, kilio kingine ni mazao yao mengi yamepotea, watu wangekuwa wanakula ndizi, mpunga ungekuwa tayari umekomaa, mahindi, ufuta hali ni mbaya sana,” alilalama mwenyekiti huyo.

Jana Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) lilitoa taarifa kwa umma, likisema: “Bwawa la JNHPP limesaidia kupunguza athari za mafuriko. Sababu kubwa ya mafuriko kwenye wilaya za Kibiti na Rufiji ni kuongezeka mtiririko wa maji katika Mto Rufiji kulikosababishwa na mvua kubwa za El-Nino zinazoendelea kunyesha katika mikoa ya nyanda za juu kusini.”

Mjumbe wa Kamati Kuu Taifa Chama Cha ACT Wazalendo, Husna Sungura alisema ni muhimu serikali ikachukua hatua za haraka kusaidia waathirika wa mafuriko hayo.

“Wanawake na watoto wanateseka sana, kinamama biashara zimekufa, watoto hawaendi shuleni, wananchi tunalipa kodi, sasa hizo kodi zetu matumizi yake ni wapi kama watu wanapata maafa na hawana pa kukimbilia?” Husna alihoji.

Karibu AfyaUpdates Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In https://afyaclass.com  Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...