Connect with us

News

WHO yaendesha kampeni ya “Afya yangu, haki yangu

Avatar photo

Published

on

#PICHA:Juliana Germano, mtaalamu wa afya kutoka Chama cha maendeleo ya familia Msumbiji, (AMODEFA) ndani ya kliniki tembezi.

Katika maadhimisho ya kuanzishwa kwake hii leo, Shirika la Afya Duniani WHO linazitaka nchi kuwekeza, kukabiliana na ubaguzi na kutovumiliana, na kupanua wigo wa upatikanaji sawa wa huduma bora za afya.

Katika maadhimisho ya Siku ya Afya Duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka  7 Aprili mwaka huu , WHO inaendesha kampeni ya “Afya yangu, haki yangu” ili kutetea haki ya afya ya kila mtu, kila mahali.

Kwa mujibu wa WHO kampeni hiyo inatetea kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za afya, elimu, na taarifa kwa wote, pamoja na maji safi ya kunywa, hewa safi, lishe bora, makazi bora, mazingira bora ya kazi na uhuru dhidi ya ubaguzi.

Kote duniani, changamoto kuu zinazoathiri haki ya afya mara kwa mara ni kutochukua hatua za kisiasa pamoja na ukosefu wa uwajibikaji na ufadhili, unaochangiwa na kutovumiliana, ubaguzi na unyanyapaa.

Shirika hilo linasema watu wengi wanaokabiliwa na kutengwa au mazingira magumu wanateseka zaidi, kama vile watu wanaoishi katika umaskini, waliokimbia makazi yao, wazee au watu wanaoishi na ulemavu.

 Vita inachochea kukosa haki ya afya

Kwa mujibu wa shirika hilo la afya duniani wakati kutochukua hatua na dhuluma ni vichochezi vikubwa vya kushindwa kwa kimataifa kutoa haki ya afya, migogoro ya sasa inaongoza kwa ukiukwaji mkubwa wa haki hii. Migogoro inaacha njia za uharibifu, changamoto ya kiakili na ya mwili, na vifo.

Limeongeza kuwa matumizi ya wa nishati ya mafuta kisukuku wakati huo huo yanachochea janga la mabadiliko ya tabianchi na kukiuka haki yetu ya kupumua hewa safi.

Pia limeongeza kuwa janga la mabadiliko ya tabianchi linasababisha hali mbaya ya hewa ambayo inatishia afya na ustawi katika sayari nzima na kuzorotesha upatikanaji wa huduma ili kukidhi mahitaji ya msingi.

Kila mtu anastahili kupata huduma bora za afya, kwa wakati unaofaa na zinazofaa, bila kubaguliwa au matatizo ya kifedha. Limesisitiza shirika hilo.

Hata hivyo limesema mwaka 2021, watu bilioni 4.5, zaidi ya nusu ya idadi ya watu wote ulimwenguni, hawakupata huduma muhimu za afya, na kuwaacha katika hatari ya magonjwa na majanga.

Hata wale wanaopata huduma mara nyingi hupata changamoto za kiuchumi, huku takriban watu bilioni 2 wakikabiliwa na ugumu wa kifedha kutokana na gharama za afya, hali ambayo imekuwa mbaya zaidi kwa miongo miwili.

Dola bilioni 328 zinahitajika kwa ajili ya afya

Ili kupanua wigo wa huduma, WHO inasema dola bilioni 200-328 za ziada kwa mwaka zinahitajika duniani kote kuweza kuongeza huduma za afya ya msingi katika nchi zenye kipato cha chini na cha kati yaani asilimia 3.3 ya matarajio ya pato la taifa.

Maendeleo yameonyesha kuwa inawezekana pale ambapo kuna utashi wa kisiasa. Tangu 2000, nchi 42, zinazowakilisha kanda zote na viwango vya mapato, zilifanikiwa kuboresha huduma za afya na ulinzi dhidi ya matumizi mabaya ya afya.

“Kutambua haki ya afya kunahitaji serikali kupitisha na kutekeleza sheria, kuwekeza, kushughulikia ubaguzi na kuwajibishwa na watu wao,” amesema Mkurugenzi Mkuu wa WHO Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus.

Ameongeza kuwa “WHO inafanya kazi na serikali, washirika na jamii ili kuhakikisha kiwango cha juu zaidi cha afya kinachofikiwa, kama haki ya msingi kwa watu wote, kila mahali.”

Haki ya afya imewekwa ndani ya Katiba ya WHO, na angalau nchi 140 zinatambua haki ya afya katika katiba zao za kitaifa.

Lakini utambuzi pekee hautoshi, amesema ndiyo maana WHO inaunga mkono nchi kutunga sheria za haki ya afya katika sekta zote na kuunganisha haki za binadamu katika sera na programu za afya. 

Amesema lengo la msaada huu ni kufanya huduma za afya zipatikane, ziweze kufikiwa na kukidhi mahitaji ya watu wanaowahudumia na kuongeza ushiriki wa jamii katika kufanya maamuzi ya afya.

Wakati wa siku ya afya duniani 7 Aprili 2023, walinda amani wa UN kutoka kikosi cha Tanzania cha kutoa msaada wa haraka, TANZQRF katika kwneye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani, MONUSCO nchini DRC wametoa huduma za kupima magonjwa yasiyo ya kuambukiza kwa wakazi wa kijiji cha Nzuma mjini Beni, huko Kivu Kaskazini.

Serikali ziwekeze katika afya

Katika Siku hii ya Afya Duniani na ziku zijazo, WHO inatoa wito kwa serikali kufanya uwekezaji wa maana ili kuongeza huduma za afya ya msingi, kuhakikisha uwazi na uwajibikaji na kuhusisha watu binafsi na jamii kwa kina katika kufanya maamuzi kuhusu afya. 

Shirika hilo linasema kwa kutambua uhusiano uliopo kati ya haki ya afya na haki nyingine za msingi, kampeni hiyo inajumuisha wito wa kuchukua hatua kuhusu fedha, kilimo, mazingira, haki, usafiri, kazi na masuala ya kijamii.

Watu binafsi, jumuiya na mashirika ya kiraia kwa muda mrefu wametetea haki yao ya afya, kuboresha upatikanaji wa huduma za afya kwa kuondoa vikwazo na kutetea usawa.

WHO inahimiza umma kujua, kulinda na kuendeleza haki zao za afya, ikiwa ni pamoja na zile zinazohusiana na huduma salama na bora, kutobagua, faragha na usiri, taarifa, uhuru wa mwili, na kufanya maamuzi.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...