News
Boti yaua watu 94 waliokuwa wakikimbia mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu
![](https://afyaclass.com/mk_omb/uploads/2024/04/At-least-94-dead-in-Mozambique-after-unlicensed-ferry-boat-capsizes-official-says-1-b850e0b8-3f55-46ba-81ff-c10aa92a71da_Q5Musvxx77.jpeg)
Boti yaua watu 94 waliokuwa wakikimbia mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu
Takriban watu 94 wamefariki, 26 hawajulikani waliko nchini Msumbiji baada ya boti isiyokuwa na leseni kupinduka.
Takriban watu 94 wamefariki wakiwemo watoto na wengine 26 hawajulikani walipo baada ya boti ya feri kupinduka katika pwani ya kaskazini mwa Msumbiji.
Boti hiyo ilikuwa imebeba watu waliokuwa wakikimbia mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu unaolikumba taifa hilo la Afrika Mashariki, shirika la utangazaji la serikali TVM liliripoti.
Meli hiyo ilikuwa mashua ya wavuvi iliyojaa kupita kiasi na haikuwa na leseni ya kusafirisha watu, Lourenco Machado, msimamizi wa INSTRASMAR, alisema kwenye Television ya serikali Jumatatu.
“Siku ya Jumapili tulisajili tukio la baharini ambapo takriban watu 94 walikufa wakati mashua iliyokuwa imebeba watu 130 ilipopinduka. Tumepata miili 94 na 26 haipo,” alisema.
Boti hiyo ilikuwa ikisafirisha watu kutoka Lunga katika jimbo la Nampula kwenda Kisiwa cha Msumbiji, alisema, akiongeza kuwa ripoti za awali zilionyesha kuwa ilikumbwa na wimbi kubwa la maji.
Abiria walikuwa wakikimbia mlipuko wa kipindupindu, Lilisema shirika la utangazaji la TVM, likimnukuu msimamizi mwingine wa baharini wa eneo hilo.
Jaime Neto, waziri wa mambo ya nje wa jimbo la Nampula, pia alisema kuwa abiria hao walikuwa wakikimbia kipindupindu.
“Kwa sababu boti hiyo ilikuwa imejaa watu wengi na haikufaa kubeba abiria, iliishia kuzama,” akiongeza kuwa watoto wengi walikuwa miongoni mwa waliofariki.
Credits; TVM
Photos: TVM,LIB, BBC
Editor; @afyaclass
Reviewed by: Dr.Ombeni Mkumbwa
-
Magonjwa4 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Elimu&Ushauri6 days ago
Afya za watu bilioni 1.8 duniani matatani kwa kutokufanya Mazoezi – WHO
-
Uzazi/Ujauzito2 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa1 day ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Events3 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
Uzazi/Ujauzito10 hours ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
News6 days ago
Mlipuko Mbaya wa homa ya nyani watokea tena KIVU KASKAZINI
-
News2 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani