Events
Tukio la kuzama kwa meli iitwayo MV Maman Benita
Tukio la kuzama kwa meli iitwayo MV Maman Benita.
Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limetoa taarifa kuhusu tukio la kuzama kwa meli iitwayo MV Maman Benita iliyotokea katika Ziwa Tanganyika ambapo limesema meli hiyo iliyosajiliwa chini ya bendera ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, inamilikiwa na kampuni ya Kikongo, iitwayo Etablissement Manimani.
“Meli hiyo iliyoanza safari yake tarehe 6 Aprili 2024 majira ya saa 12:00 jioni ikitokea bandari ya Kigoma kuelekea Kalemie, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ilikuwa imebeba jumla ya abiria 27 wakiwemo Watanzania watano, Wachina wanne , Raia wa Kongo 16, Raia mmoja wa Kenya pamoja na Mtoto mdogo”
“Meli hiyo iliyotarajiwa kuwasili Kalemie majira ya saa 8:00 usiku, haikufika ambapo asubuhi ya tarehe 7 Aprili 2024, wavuvi walifanikiwa kumwokoa abiria mmoja mwenye asili ya China na kisha kutoa tarifa kwa Mamlaka za Serikali ya Kongo juu ya kuzama kwa meli ya MV Maman Benita katika eneo la Kabimba, Nchini Kongo, baada ya kupata taarifa hiyo, zoezi la utafutaji na uokoaji lilianza mara moja ambapo hadi kufikia majira ya saa 1:00 usiku wa tarehe 7 April, 2024, Wahanga 17 walikuwa wameshaokolewa, kati yao ikijumuisha Wachina 2, Watanzania 3, na Wakongo 12”
“Chanzo cha kuzama kwa meli bado hakijajulikana isipokuwa Nahodha wa meli hiyo ameokolewa na timu ya Wataalamu tayari imekwenda eneo la tukio kwa ajili ya ufuatiliaji, zoezi la utafutaji kuokoa abiria waliosalia linaendelea”
Credits:MillardAyoUPDATES
📸PhotosEditor: Via MillardAyo
Reviewed by; @afyaclass
-
Uzazi/Ujauzito5 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Magonjwa4 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
Magonjwa7 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Magonjwa2 days ago
kuharisha na kutapika ni dalili za ugonjwa gani
-
Events6 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
News4 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani
-
Utafiti22 hours ago
Zaidi ya vifo milioni 3 kila mwaka hutokana na matumizi ya pombe na madawa ya kulevya-WHO