Connect with us

afya news

Mkunga mmoja anatakiwa kuhudumia mjamzito mmoja,wakunga waeleza kinachowavunja moyo

Avatar photo

Published

on

#PICHA:Wakunga kisiwani Zanzibar wakifurahia wakati wa maadhimisho ya siku ya wakunga duniani yaliyofanyika mjini Unguja.

Kwa mujibu wa miongozo ya afya, mkunga mmoja anatakiwa kuhudumia mjamzito mmoja, huku muuguzi mmoja akihudumia wajawazito wanne.

Unguja. Licha ya wakunga kuwa watendaji wakuu wa kutoa huduma kwa mama na mtoto kwenye sekta ya afya, wamesema wanakabiliwa na changamoto nyingi, hivyo kushusha morali ya utendaji wao.

Miongoni mwa changamoto hizo ni kushindwa kutambuliwa mchango wao wanapofanya vizuri, bali hupokea lawama wanapokosea kutokana na sababu za kibinadamu kama uchovu unaotokana na kufanya kazi nyingi kupitiliza muda wao wa kazi.

Wamebainisha hayo katika risala iliyosomwa leo Mei 5, 2024 na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wakunga Zanzibar, Sanura Abdala Salim wakati wa maadhimisho ya siku ya wakunga duniani.

Ametaja changamoto nyingine ni ufinyu wa elimu ya utambuzi, upungufu wa vitendea kazi kama vifaa vya kupimia shinikizo la damu, vipimo vya mkojo, na vifaa vya kisasa vya kumfuatilia mtoto tumboni.

“Wakunga wakiwa ndio watendaji wakuu katika sekta ya afya ya uzazi bado wanakosa kutambuliwa wanapofanya vizuri, lakini hushushiwa lawama katika makosa ambayo mengine ni ya kibinadamu kutokana na uchovu wa kazi nyingi,” amesema.

Amesema changamoto nyingine ni upungufu mkubwa wa wauguzi na wakunga katika maeneo ya kutoa huduma za mama na mtoto ikiwemo wodi za wazazi, akieleza mkunga mmoja anahudumia zaidi ya watu 12.

Kwa mujibu wa miongozo ya afya, mkunga mmoja anatakiwa kuhudumia mjamzito mmoja, huku muuguzi mmoja akihudumia wajawazito wanne.

“Tunaomba viongozi wetu wa Wizara ya Afya kuwaangalia kwa jicho la tofauti na kuwapa motisha wauguzi na wakunga wanaofanya kazi katika wodi za wazazi, kwani wanahudumia idadi kubwa ya kina mama,” amesema.

Hata hivyo, kupitia risala hiyo wameahidi  kuyaendeleza mazuri na kuyaboresha kila mwaka ili kutoa huduma bora za afya ya mama na mtoto.

“Pia niwaombe wakunga wenzangu wote kufanya kazi kwa bidii, weledi, heshima, mapenzi, lugha nzuri kwa kina mama, watoto na jamii kwa ujumla,” amesema.

Mkunga mstaafu, Sharifa Hawadh amesema wakunga na wauguzi ni wanasayansi, lakini ili waweze kutenda vyema kazi zao lazima wasome na kujiongezea elimu, ujuzi na maarifa.

Amesema kazi ya ukunga pamoja na uzito wake lakini inahitaji watu wenye upendo na kuwajali wagonjwa.

Mkunga Asha Mkamba amesema kabla ya kufikia kilele cha maadhimisho hayo walifanya shughuli mbalimbali ikiwemo uchunguzi wa lishe na saratani ya kizazi kwa vijana wa umri kati ya mikaa 18 hadi 25 na kubaini kuwapo changamoto.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dk Habiba Hassan Juma amesema wizara ina mpango kuona watendaji wanaongezeka, kwani kuna upungufu mkubwa katika vituo vya afya.

Alisema kadri watakavyoruhusiwa na utumishi kuajiri watafanya hivyo ili kufikia uwiano sawa kati ya wauguzi na wagonjwa ili kuimarisha afya ya jamii.

“Tunatakiwa kuwa na subira kwani kazi hii ni nzito na ni ya wito wa kujitolea,” amesema.

Naibu Waziri wa Afya, Hafid Hassan, akisoma risala kwa niaba ya Mariam Mwinyi, mke wa Rais wa Znzibar, Dk Hussein Mwinyi amesema amepokea changamoto zinazowakabili lakini wasivunjike moyo.

Ameiagiza Wizara ya Afya kuzifanyia kazi na kutatua changamoto hizo kama zilivyojieleza katika risala yao.

Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ipo katika mikakaki ya kuimarisha afya ya uzazi kwa kuzuia na kupunguza vifo vya wajawazito na watoto wachanga.

Amesema ili kukamilisha malengo hayo wanahitaji kuwatumia wakunga ambao wana mchango mkubwa wa kufanikisha malengo ya nchi.

Ofisa uzazi salama kitengo shirikishi cha afya ya uzazi na mtoto, Safia Haidhuru Ramadhan amesema takwimu za mwaka 2022 zinaonyesha kulikuwa na vifo vya uzazi 52 ikilinganishwa na vifo 70 vilivyotokea mwaka 2021.

Kwa upande wa vifo vya watoto vilivyotokana na changamoto za uzazi amesema ni 1,727 kiwango ambacho kinaonekana kuwa bado kipo juu.

Karibu AfyaUpdates Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In https://afyaclass.com  Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...