Connect with us

News

Afrika hujumuisha asilimia 95 ya wagonjwa wa malaria duniani;WHO

Avatar photo

Published

on

Nchi zinazokabiliwa Zaidi na Vifo na milipuko ya ugonjwa wa Malaria kama vile Uganda, zimefaulu angalau kwa kiwango fulani.

Wakati ulimwengu ukiadhimisha siku ya kupambana na ugonjwa wa Malaria Tarehe 22.04.2024.

juhudi za mataifa yanayokumbwa zaidi na vifo na milipuko ya ugonjwa huo kama vile Uganda, zimefaulu angalau kwa kiwango fulani.

Uganda ambayo iko katika nafasi ya tatu barani Afrika kwa kuwa na idadi ya wagonjwa na vifo imewekeza katika mbinu kadhaa kupambana na ugonjwa huo.

Ila baadhi ya jamii bado wanakwamisha juhudi hizo kwa kutumia vibaya vifaa wanavyopewa. Kwa mfano baadhi ya watu hutumia vyandarua vya mbu kuvulia samaki au kuvigeuza kuwa uzio dhidi ya ndege wanaoharibu mashamba yao.

Afrika hujumuisha asilimia 95 ya wagonjwa wa malaria duniani. Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Duniani, WHO mataifa 10 barani Afrika na nchi ya India ndiyo yalio na idadi kubwa ya vifo na visa vya wagonjwa wa homa ya malaria.

Uganda inashikilia nafasi ya tatu barani Afrika ikiifuata Nigeria. Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ndiyo inaongoza. Waziri wa Afya dokta Jane Ruth Aceng anathibitisha hali hiyo huku akielezea kuwa vita dhidi ya malaria vinatakiwa kumuhusisha kila mtu katika jamii.

”Hii ina maana kuwa tatizo la malaria Uganda ni la kiwango cha juu, kwa hiyo hata idadi ya vifo ni ya juu. Ndiyo sababu sisi kama Uganda tunatakiwa kushirikiana kama jamii kupambana na tatizo hili la malaria.”

Ijapokuwa idadi ya wagonjwa wa malaria nchini Uganda imeshuka kutoka asilimia 42 ya idadi ya watu mwaka 2009 hadi chini ya aslimia 9 kwa sasa, takwimu za wizara zinaonyesha kuwa  watu 16 hufariki kila siku nchini humo kutokana na ugonjwa huo unaoambukizwa na mbu.

Wizara ya afya ikishirikiana na mashirika mbalimbali ya kimataifa imeendesha shughuli kadhaa za kukabiliana na ugonjwa huo na angalau juhudi hizi zimezaa matunda, kama anavyofafanua zaidi Dokta Jimmy Opigo, kamishna msaidizi anayesimamia shughuli za kukabiliana na homa ya malaria kama alivyozungumza na DW.

”Nchini Uganda kila familia ina chandarua cha mbu, familia pia hujigharamia kupambana na malaria kwa kununua dawa za kupuliza au kujipaka. Tuna viwanda vya vyandarua, vya dawa za malaria na pia vile vinavyotengeneza vifaa vya kupima malaria.”

Hata hivyo, baadhi ya watu hasa kwenye maeneo ya maziwa na mito hutumia vyandarua vya mbu kama nyavu za kuvulia samaki au kuvigeuza uzio dhidi ya ndege wanaoharibu mashamba yao. Dokta Daniel Kyabayinze ni mkurugenzi wa afya ya umma katika wizara hiyo.

”Tunapaswa kuwaambia watu watumie vyandarua kwa njia iliyokusudiwa. Malaria inaweza kuwaua na pesa wanazochuma kwa kutumia vibaya vyandarua hazitayaokoa maisha yao.”

Shirika la WHO linaeleza kuwa duniani, kila dakika moja mtoto mmoja mwenye umri wa chini ya miaka mitano hufariki kutokana na homa ya malaria. Idadi kubwa ya vifo hivyo ni barani Afrika. Katika wiki chache zijazo Uganda itatoa chanjo dhidi ya malaria kwa watoto ikijiunga na mataifa mengine ya Afrika yaliyotangulia kama vile Kenya mwaka 2019. Lakini waziri wa afya Jane Ruth Aceng anatahadharisha kuwa chanjo hiyo haitoi kinga kwa watoto wote wanaoipata.

”Kwa watoto, chanjo hiyo ina kinga ya asilimia 50 tu. Kwa hiyo siyo suluhisho lenye uhakika, suluhisho la uhakika tunalotegemea ni kuzidisha juhudi za kijamii.”

Uganda pia inazingatia kurejelea mpango wa kunyunyiza viwatilifu vya kuangamiza mbu hata kama itakuwa DDT ambayo mataifa ya Ulaya yalitumia kuangamiza malaria.Kamerun yazindua kampeni ya kihistoria ya chanjo ya Malaria Jitihadi za awali za kutumia mbinu hiyo zilipingwa na wanasiasa. Waziri Aceng anadai kuwa wanasiasa hao walichochewa na makampuni yanayouza dawa za kutibu malaria yakihofia kuwa yangepoteza soko la dawa zao.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa3 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa4 weeks ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa1 month ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa4 days ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa5 days ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa2 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa3 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...

Magonjwa3 weeks ago

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho Kuna magonjwa mengi yanayohusiana na macho, mengi yanatibika lakini kuna baadhi ya magonjwa...

Magonjwa4 weeks ago

Kunguni husababisha ugonjwa gani

Kunguni husababisha ugonjwa gani Kunguni ni wadudu wadogo ambao chakula chao kikubwa ni damu, wadudu hawa huweza kunyonya damu kutoka...