Connect with us

Events

Kuongeza Nguvu Katika Mapambano Dhidi ya Malaria

Avatar photo

Published

on

LEO ni Siku ya Malaria Duniani ambayo imekuwa ikiadhimishwa kila mwaka tangu ilipoanzishwa na nchi wanachama wa Shirika la Afya Duniani (WHO) mwaka 2007 wakati wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Afya.

Lengo la kuadhimisha siku hii ni kuweka msisitizo katika mapambano ya ugonjwa huu hatari ambao umegharimu mamilioni ya watu duniani. Mapambano hayo dhidi ya malaria ni kuonyesha umuhimu wa uwekezaji endelevu na utashi wa kisiasa katika kukinga na kudhibiti malaria.

Kaulimbuiu ya mwaka huu katika kuadhimisha siku ni “Kuongeza Nguvu Katika Mapambano Dhidi ya Malaria” ikisisitiza jitihada za pamoja kwa mataifa yote duniani katika kuzuia, kupambana na kutokomeza malaria. Kwa Tanzania, maadhimisho yatafanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Uyui, Tabora na mgeni rasmi atakuwa Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu.

Wakati maadhimisho hayo yanafanyika pamoja na jitihada mbalimbali zinazofanyika kwa serikali kushirikiana na wadau wa maendeleo pamoja na sekta binafsi, takwimu zinaonyesha kuwa bado ni hatari hasa kwa watoto wachanga na walio chini ya miaka mitano pamoja na wajawazito.  Aidha, nchi za Afrika ikiwamo Tanzania, kwa mujibu wa takwimu, ndizo zinazoathirika zaidi na malaria hivyo jitihada zaidi zinatakiwa katika kupambana na kutokomeza maradhi haya.

Tamwinu za WHO zinabainisha kwamba mwaka 2022, kulikuwa na vifo 608 000 vilivyotokana na malaria na maambukizi mapya ya ugonjwa huo yalikuwa milioni 249. Asilimia 94 ya vifo na maambukizi hayo ilikuwa katika bara la Afrika na kwa mantiki hiyo, jitihada zaidi zinapaswa kufanywa kwa Afrika katika mapambano dhidi ya malaria.

Kutokana na ukweli huo, nchi za Afrika kupitia jumuia za kikanda kama vile Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Uchumi kwa nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS), Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Umoja wa Afrika (AU) zinapaswa kuweka moja ya ajenda za kipaumbele kwenye mikutano yao.

Nchi hizo, ambazo ndizo waathirika wakubwa wa malaria, kwa kushirikiana na washirika wa maendeleo na mashirika ya kimataifa zinapaswa pia kuweka mikakati thabiti katika kupambana na malaria ili kunusuru nguvu kazi na kuzifanya nchi ziwe na ustawi.

Kuna kampeni mbalimbali na mikakati ambayo imefanyika katika kupambana na malaria katika ngazi mbalimbali lakini bado tatizo ni kubwa, hivyo inahitajika mikakati zaidi katika vita hivyo. Ili kufanikisha hilo, mapambano yanapaswa kuanzia ngazi ya kaya hadi taifa na si kuachia wataalamu pekee.

Katika kufanya hivyo, kila Mtanzania anapaswa kuzingatia maelekezo yanayotolewa na wataalamu wa afya yakiwamo kuteketeza mazalia ya mbu katika maeneo ya makazi, kutumia chandarua chenye dawa, kuwakinga watoto wachanga na walio chini ya miaka mitano pamoja na wajawazito ambao ndio walio katika hatari zaidi ya kupatwa na ugonjwa huo.

Aidha, imekuwa ikisisitizwa kuwa mtu anapoona dalili za malaria, hana budi kufika katika kituo cha kutolea huduma za afya kwa ajili ya vipimo na atakapobainika apatiwe matibabu stahiki.

Licha ya maelekezo hayo, idadi kubwa ya Watanzania hawazingatii ndiyo maana ugonjwa huo umekuwa ukizidi kugharimu maisha ya watu huku taifa likiendelea kutenga bajeti kwa ajili ya kinga na tiba.

Ni dhahiri kwamba iwapo kila mtu atazingatia maelekezo ya wataalamu wa afya katika kujikinga na malaria, kutakuwa na mafanikio makubwa katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo na hatimaye kuwa na Tanzania isiyo na maambukizi wala vifo vitokanavyo na malaria.

Shime kila Mtanzania asimame katika nafasi yake huku akisema Tanzania, Afrika na dunia bila malaria inawezekana. Hapo ndipo ushindi dhidi ya maradhi haya utakapopatikana na hatimaye maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi kuonekana.

MASWALI&MAJIBU kuhusu afya| Link...👇

https://afyaclass.com/afyaforums

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa2 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa3 weeks ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa1 month ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa1 month ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake3 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa5 days ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa6 days ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa2 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa2 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...

Magonjwa2 weeks ago

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho Kuna magonjwa mengi yanayohusiana na macho, mengi yanatibika lakini kuna baadhi ya magonjwa...

Magonjwa3 weeks ago

Kunguni husababisha ugonjwa gani

Kunguni husababisha ugonjwa gani Kunguni ni wadudu wadogo ambao chakula chao kikubwa ni damu, wadudu hawa huweza kunyonya damu kutoka...

Magonjwa4 weeks ago

je ugonjwa wa pumu unaambukiza

je ugonjwa wa pumu unaambukiza? Hili ni Swali ambalo watu wengi huuliza,hata kwenye page za afyaclass, kwa kuliona hilo, tumeona...

Magonjwa1 month ago

Dalili za mwanzo za ugonjwa wa ini

Dalili za mwanzo za ugonjwa wa ini Ugonjwa wa ini (hepatic disease) mara nyingi huanza taratibu na dalili zisizo wazi,...