Connect with us

Events

Atolewa uvimbe wa kilo tano tumboni alioishi nao miaka 10

Avatar photo

Published

on

Atolewa uvimbe wa kilo tano tumboni alioishi nao miaka 10

“Nimezaa watoto 11 lakini mtoto wangu wa mwisho niliyemzaa mwaka 2010 nilikuwa nipoteze maisha, maana nilitokwa na damu nyingi sana, nikazimia mara tatu na wakati wote wa mimba damu ilikuwa inavuja, sikujua tatizo.”

Haya ni maneno ya Eveline Paulo, mkazi wa Biharamulo mkoani Kagera aliyetolewa uvimbe wenye uzito wa kilo tano tumboni.

Uvimbe huo alioishi nao kwa miaka 10 bila matibabu, ulikuwa umekaa nje ya kizazi.

Akizungumza na Mwananchi, akiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Geita baada ya kufanyiwa upasuaji, Eveline amesema tumbo lake lilikuwa limejaa na alihangaika kwenda hospitali mbalimbali lakini hakupata huduma kutokana na kusumbuliwa na shinikizo la damu.

“Nimehangaika kwenda hospitali huko Biharamulo na Mwanza, lakini kila wakitaka kunihudumia presha inapanda, narudishwa nyumbani, mwisho nikaamua kuishi na hali hiyo hadi nikaona kawaida, lakini nilikuwa nateseka sana,” amesema mama huyo.

Hata hivyo, amesema hivi karibuni alienda kumtembelea mwanawe aishie Geita na akamsimulia tatizo lake na mwanawe akaamua kumpeleka hospitali kwa matibabu zaidi na baada ya vipimo kuonyesha uvimbe alikokuwa nao tumboni ni mkubwa, madaktari wakaelekeza afanyiwe upasuaji kuuondoa.

Akizungumzia upasuaji huo uliochukua saa mbili na nusu, Dk Isaack Ajee, bingwa wa magonjwa ya wanawake ameasema uvimbe aliokuwa nao Paulo ulikuwa wa sentimita 38 na kama ingekuwa ni mimba, ni sawa na ya miezi tisa.

“Lakini hata hivyo, uzito wa uvimbe huu unazidi ule wa mtoto anayezaliwa, tunashukuru Mungu tumemaliza salama na afya ya mama kwa sasa iko sawa na akiendelea hivi baada ya siku mbili ataruhusiwa kutoka hapa hospitali,” amesema daktari huyo.

Dk Ajee amesema uvimbe huo ulikuwa na uzito wa kilo tano na ulikuwa pembeni ya kizazi hali iliyosababisha kukibanwa.

Amesema mama huyo pia alikuwa na uvimbe mwingine mdogo ndani ya kizazi.

“Tulibaini ana fibroids na ilikuwa kubwa, ilikuwa pembeni ya kizazi lakini pia ndani ya kizazi kulikua na vimbe ndogondogo hii ya pembeni ya kizazi ilikuwa ikipokea damu kutoka sehemu nyingine za mwili.”

“Upasuaji huu tuliufanya na wataalamu wenzangu watatu, mwanzoni tulihoifia unaweza kujishikiza kwenye matumbo au kwenye kibofu cha mkojo au unaweza kushika sehemu nyingine tofauti, ndiyo maana tuliingia watatu ili isijetokea tatizo.

“Tulihakikisha tunautoa vizuri na tumeikuta imejishikisha kwenye kizazi japo ni nje, lakini kizazi kilikuwa kimebanwa na ndani ya kizazi kulikua na vimbe ndogondogo,” amefafanua.

Kwa mujibu wa Dk Ajee, kutokana na uvimbe kuwa nje ya kizazi, kulimfanya mwanamke huyo asipate tatizo kama lile la uvimbe unaoota ndani ya kizazi.

Amesema endapo uvimbe huo usingetolewa na ukaendelea kuvimba, ungemfanya apate ugonjwa ya wa UTI mara kwa mara kutokana na kukandamiza kibofu, kupata choo kigumu na wakati mwingine kufunga.

Pia angeweza kupata msukumo kwenye kizazi na kushindwa kulala vizuri, ameongeza daktari huyo.

Amesema mwanamke anayeugua ugonjwa wa aina hiyo asipopata huduma sahihi, husababisha tumbo kujaa gesi na kushindwa kuhema vizuri na mara chache uvimbe wa aina hiyo husababisha pia saratani.

Sababu mwanamke kupata ‘fibroids’

Dk Ajee amesema hakuna sababu maalumu za kitaalamu zinazoonyesha husababishwa na nini, hata hivyo, anasema inaweza kumpata mtu kutokana na historia ya familia yake, pia wanawake wenye vitambi, wenye uzito mkubwa na wasiozaa (wagumba) au wanaotumia dawa za vichocheo wako hatarini zaidi.

Kuna dawa zaidi ya upasuaji?

Kwa mujibu wa Dk Ajee, tiba sahihi ya kutibu ‘fibroads’ au ‘mayoma’ ni mgonjwa kufanyiwa upasuaji na hakuna dawa ya kunywa ya kukwepa upasuaji.

“Kilichopo ni kwamba wapo watu wana mayoma na wakati mwingine inakuwa kubwa na anatokwa na damu, akiwa kwenye shatua hii anapewa dawa ya kuchoma ili uvimbe usinyae na baada ya hapo anafanyiwa upasuaji kuitoa. Dawa hii haiondoi uvimbe kazi yake ni kuufanya usinyae tu,” amesema Dk Ajee.

Hivyo, ameonya watu wasidanganywe kwamba kuna dawa za kunywa kuuondoa zaidi ya kufanyiwa upasuaji.

“Na kuna watu wanaosema wanatibu uvimbe kwa kuwapa wagonjwa dawa za kunywa, hilo ni kosa kimatibabu kwa kuwa mpaka sasa hakuna dawa ya kutibu ‘fibroid zaidi ya kufanya upasuaji na kuzitoa,” amesema.

Tofauti uvimbe ndani ya kizazi na nje ya kizazi

Kwa mujibu wa daktari huyo bingwa, uvimbe ukitokea ndani ya kizazi, mgonjwa atakuwa akitokwa na damu nyingi wakati wa hedhi na kupata maumivu makali huku ule wa nje ya kizazi, mgonjwa hapati maumivu ila athari yake zinaweza kuwa kubwa endapo utajishikiza kwenye kizazi na husababisha maumivu kwa sababu damu haisambai.

Akizungumzia siku tatu walizofanya huduma za mkoba katika Hospitali ya Mkoa wa Geita, Dk Ajee amesema wamewahudumia wanawake zaidi ya 150 na wengi wao wakiwa na changamoto za uzazi na hedhi, kutokwa uchafu sehemu za siri na uvimbe kwenye kizazi.

Dk Ajee amewataka wanawake wanaobainika kuwa na matatizo hayo wasikate tamaa ya kutafuta huduma za tiba.

Karibu AfyaUpdates Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In https://afyaclass.com  Also Follow us on Instagram @afyaclass

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...