Connect with us

Events

Zaidi ya watu 45 wamefariki dunia nchini Kenya baada ya bwawa kupasua kingo

Avatar photo

Published

on

Zaidi ya watu 45 wamefariki dunia nchini Kenya baada ya bwawa kupasua kingo zake kufuatia mvua kubwa na mafuriko, maafisa wamesema.

Watu katika vijiji karibu na Mai Mahiu, yapata kilomita 60 kutoka mji mkuu, Nairobi, walisombwa na maji walipokuwa wamelala.

Zaidi ya watu 100 wameuawa katika mafuriko ambayo yameharibu sehemu za Kenya katika mwezi uliopita.

Vikosi vya waokoaji vinachimba matope kusaka manusura katika vijiji kadhaa, vikiwemo Kamuchiri na Kianugu kaunti ya Nakuru.

Maelezo ya video,Makumi ya watu wamepoteza maisha baada ya bwawa kuvunja kingo zake nchini Kenya

Kati ya miili 42 iliyopatikana mapema wasubuhi 17 ilikuwa ya watoto, kamanda wa polisi Stephen Kirui alisema, akinukuliwa na shirika la habari la Reuters.

“Maji yalikuja kwa kasi kutoka Bwawa la Old Kijabe na kusomba nyumba na magari mengi. Hatujawahi kuona mafuriko makubwa kama haya tangu tulipozaliwa hapa Mai Mahiu,” David Kamau aliiambia BBC.

Mkazi mwingine, Peter Muhoho, alisema kuwa wengi wa majirani zake walisombwa na maji katika kijiji cha Kianugu chenye takriban nyumba 18.

“Nilikuwa nimelala niliposikia kishindo kikubwa na mayowe. Maji yalikuwa yamefurika eneo hilo. Tulianza kuokoa watu,” Bw Muhoho aliambia BBC.

Akionyesha begi alilokuwa ameshikilia, Bw Muhoho aliongeza: “Mkoba huu ni wa mtoto niliyemfahamu. Alisombwa na maji. Niliupata [mfuko huo] chini ya mkondo.”

Serikali imeahirisha kufunguliwa kwa shule kote nchini Kenya huku mvua zaidi ikitarajiwa kunyesha, kulingana na idara ya utabiri wa hali ya anga .

Zaidi ya watu 130,000 wamekimbia makazi yao kutokana na mafuriko hayo, huku watu wengi wakipata hifadhi shuleni.

Mvua kubwa pia imenyesha katika nchi jirani za Tanzania na Burundi.

Takriban watu 155 wameuawa nchini Tanzania tangu Januari.

Nchini Burundi, karibu watu 100,000 wamekimbia makazi yao.

Idadi ya waliopoteza maisha haijulikani, lakini tovuti inayohusishwa na Umoja wa Mataifa inaripoti kuwa watu 68 waliuawa katika mji mkuu, Bujumbura, tarehe 10 Februari pekee baada ya mvua kubwa kuharibu nyumba 3,500.

Mwandishi wa BBC anayeshughulikia utabiri wa hali ya hewa Chris Fawkes anasema kuwa mojawapo ya vichochezi vikubwa vya mvua ni Dipole ya Bahari ya Hindi (IOD).

IOD – ambayo mara nyingi huitwa “Indian Niño” kwa sababu ya kufanana kwake na sehemu yake ya Pasifiki – inaelezea tofauti ya halijoto ya uso wa bahari katika sehemu tofauti za Bahari ya Hindi.

Wakati wa awamu chanya, maji katika Bahari ya Hindi magharibi yana joto zaidi kuliko kawaida na hii inaweza kuleta mvua kubwa bila kujali El Niño.

Hata hivyo, wakati wote IOD chanya na El Niño hutokea kwa wakati mmoja, kama ilivyokuwa mwaka jana, mvua katika Afrika Mashariki inaweza kuwa kali.

Mojawapo ya mifumo chanya ya IOD kwenye rekodi ililingana na mojawapo ya mifumo thabiti zaidi ya El Niño mwaka wa 1997 na 1998, huku mafuriko makubwa yakiripotiwa. Haya yalisababisha vifo zaidi ya 6,000 katika nchi tano katika eneo hilo.

Mada: Via BBC

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa2 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...