Connect with us

Dawa

Matumizi makubwa ya dawa za Antibiotics kipindi cha COVID-19,hatari ya kuongeza Usugu

Avatar photo

Published

on

Matumizi makubwa ya dawa za Antibiotics kipindi cha COVID-19,hatari ya kuongeza Usugu.

Ushahidi mpya uliotolewa na shirika la afya ulimwenguni, WHO unaonesha kuwa wakati wa janga la COVID-19 kulikuweko na matumizi yasiyo ya lazima na ya kupita kiasi ya viuavijasum au antibiotics ambayo huenda yamesababisha kusambaa kwa usugu wa viuavijiumbe maradhi au Antimicrobials.

Taarifa iliyotolewa leo Geneva, Uswisi na WHO inasema ingawa ni asilimia 8 tu ya wagonjwa waliolazwa kwa ajili ya COVID-19 ndio walikuwa na maambukizi yatokanayo na bakteria au vimelea na hivyo kuhitaji viuavijasumu, takwimu zinaonesha kuwa wagonjwa watatu kati ya wanne sawa na asilimia 75 ya wagonjwa walitibiwa kwa viujavijasumu pengine tu ingaliweza kuwasaidia hata kama haikuwa inahitajika.

Wagonjwa wasio mahututi Afrika walipatiwa viuavijasumu

Matumizi ya viuavijasumu yalikuwa ni kuanzia asilimia 33 kwa wagonjwa ukanda wa Pasifiki Magharibi hadi asilimia 83 ukanda wa Mediteranea Mashariki na Afrika.

Kati ya mwaka 2020 hadi 2022 kitendo cha daktari kuandikia dawa aina ya viuavijasumu kwa wagonjwa kilipungua huko Ulaya na Amerika, ilhali kiliongeza katika nchi za Afrika.

Kwa wastani kiwango kikubwa cha matumizi ya dawa hizo miongoni mwa wagonjwa wa COVID-19 waliokuwa mahututi kilifikia asilimia 81.

Ingawa hivyo kulikuwa na utofauti mkubwa wa utoaji wa dawa hizo kwa wagonjwa ambao hawakuwa mahututi lakini ukanda wa Afrika uliongoza kwa kupatiwa wagonjwa wa kiwango hicho kwa asilimia 79.

Matumizi holela ya viuavijasumu huweza kusababisha usugu wa dawa

“Pindi mgonjwa anapohitaji viuavijasumu, manufaa yake yanazidi hatari zitokanazo na matumizi ya dawa hizo au hatari za kuleta usugu hapo baadaye,” ameesma Daktari Silvia Bertagnolio, Mkuu wa kitengo cha Ufuatiliaji, Ushahidi na uimarishaji wa Maabara WHO.

Amesema “hata hivyo pindi viuavijasumu vinapotumika pale isipo lazima, hazina faida yoyote zaidi ya kuongeza hatari na matumzi yake yanaweza kusababisha kuibuka au kusambaa kwa usugu wa dawa hizo kwa vijiumbe maradhi, au microbes.”

Daktari Bertagnolio  amesema takwimu hizi mpya zinataka sasa kuimarisha matumizi sahihi ya viuavijasumu na kupunguza madhara yasiyo ya lazima kwa wagonjwa na jamii.

Kwa ujumla matumizi ya viuavijasumu hayakuimarisha tiba ya wagonjwa wa COVID-19. Badala yake, inaweza kuwa iliongeza hatari kwa watu ambao hawakuwa na maambukizi ya bakteria au vimelea ikilinganishwa na wale ambao hawakupatiwa dawa hizo wakati wanaugua COVID-19.

Utafiti huu kuchangia kwenye mapendekezo yajayo

Uchambuzi zaidi utafanyika wa takwimu hizi mpya ili ziweze kujumuishwa kwenye mapendekezo yajayo ya matumizi ya viujavijasumu kwa wagonjwa wa COVID-19, kama sehemu ya mwongozo wa tiba dhidi ya ugonjwa huo. Mkutano utafanyika Hispania mwezi ujao.

Na baadaye mwezi Septemba mwaka huu, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa litakuwa na kikao cha viongozi kukubaliana hatua za kupunguza usugu wa viuavijiumbe maradhi kwa ajili ya afya ya binadamu, Wanyama, na sekta ya kilimo pamoja na mazingira, halikadhalika kusongesha uongozi na ufadhili wa fedha ili kupunguza usugu wa dawa hizo au AMR.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa3 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa4 weeks ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa1 month ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa4 days ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa5 days ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa2 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa3 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...

Magonjwa3 weeks ago

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho Kuna magonjwa mengi yanayohusiana na macho, mengi yanatibika lakini kuna baadhi ya magonjwa...

Magonjwa4 weeks ago

Kunguni husababisha ugonjwa gani

Kunguni husababisha ugonjwa gani Kunguni ni wadudu wadogo ambao chakula chao kikubwa ni damu, wadudu hawa huweza kunyonya damu kutoka...