Connect with us

Dawa

Matumizi sahihi ya dawa za kutibu maambukizi ya bakteria – maarufu kama Antibayotiki

Avatar photo

Published

on

Usugu wa antibayotiki na inapogeuka kuwa sumu

Tarehe 18 mpaka 24 mwezi Novemba ilikuwa wiki ya uhamasishaji juu ya matumizi sahihi ya dawa za kutibu maambukizi ya bakteria – maarufu kama Antibayotiki, na sababu zinaozoweza kusababisha usugu wa dawa hizo.

Katika ulimwengu usio na anti-biotics, magonjwa tunayoyatibu kwa urahisi hii leo yanaweza kugeuka tishio la maisha, kutokana na bakteria zaidi kujenga usugu dhidi ya dawa za kawaida. Hebu fikiria kwa mfano, kwamba una maambukizi kwenye njia ya mkojo, UTI.

Mwanzoni unaweza kuwa wasiwasi tu, lakini kwa haraka hali inageuka kuwa maumivu makali, ambayo hayawezi kutulizwa kwa kulala chini na kujikanda na kunywa maji mengi.

Lakini kuna njia rahisi; Unaenda kwa daktari wako na kupata dawa ya kutibu maambukizi ya bakteria.

Dalili zako zinaweza kutoweka ndani ya siku tatu hadi tano baada ya kuanza kumeza vidonge hivyo vidogo. Haya ndiyo maajabu ya tiba za kisasa.

Lakini hebu sasa fikiria hali ambapo hakuna dawa hizo! Maambuzi yanaweza kusambaa kwenye figo zako, au kuingia kwenye mzunguko wako wa damu. Maisha yako yangekuwa hatarini.

Maisha bila antibayotiki yanawezekana?

Ulimwengu usiyo na dawa za kutibu maambukizi ya bakteria siyo ulimwengu mbadala au filamu ya kutisha. Ni hali inayotukabili sasa hivi.

Bakteria zaidi na zaidi wanakuwa sugu kwa dawa zilizotengenezwa kutibu maambukizo yanayosababishwa na bakteria hawa.

Wazo la msingi ni kuua bakteria kwa antibiotics. Lakini kuna uwezekano kwamba bakteria hao wataishi na kuwa sugu.

Kuwa na antibiotic zisizofanya kazi tena na sawa na kutokuwa na antibiotic kabisaa.

Mnamo mwaka 2019, karibu watu milioni 1.27 kote duniani walikufa kutokana na maambuzi ya bakteria wasiosikia tena dawa, kulingana na utafiti uliochapishwa katika jarida la kitabibu la The Lancet.

Kituo cha Ulaya cha Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa kinakadiria kwamba Ulaya hushuhudia zaidi ya maambukizo 670,000 na bakteria sugu wasiosikia dawa kila mwaka, na kwamba takriban watu 33,000 katika bara hilo hufa kila mwaka kutokana na tatizo hilo.

Wataalamu wa matibabu wanazidi kuwa na wasiwasi kuhusu kupungua kwa ufanisi wa dawa zetu nyingi zinazoaminika.

Chris Dowson, aliefanya utafiti juu ya usugu wa dawa za antiobiotic kwa miongo kadhaa na ndiye mkuu wa kundi la utafiti wa magongwa ya kuambukizwa katika chuo kikuu cha Warwick cha nchini Uingereza, anasema dawa hizo zitaacha kufanya kazi na hivyo kuna haja ya kutafuta mbadala.

Lakini je, tumefikaje hapa? Kwanini kuna bakteria wengi wasioweza kuuawa kwa matibabu ya dawa zetu tena?

Usugu umeongezeka pakubwa katika miaka iliyopita kutokana na matumizi yaliopitiliza ya antibiotics.

Madaktari huwaandikia wagonjwa dawa hizo kwa urahisi zaidi kuliko hapo awali, ikiwa ni pamoja na katika hali ambapo inaweza kuwa siyo lazima.

Na wakati mwingine wagonjwa huacha kutumia dawa zao za antibiotic wanapojisikia nafuu ― licha ya madaktari kusema wagonjwa wanapaswa wakati wote kutumia dozi nzima ya antibiotics.

Kwanini ni rahisi kukatisha dozi za Antibayotiki?

Sababu ni rahisi: Mgonjwa anaweza kujisikia vizuri, lakini maambukizi yanaweza kuwepo bado, na kwa sababu haujameza dozi kamili, inaweza kuwa haitoshi kuua bakteria wote.

Hapo ndipo bakteria hupata nafasi ya kupambana kushinda kiwango cha chini cha antibiotics na kuzowea.

Na katika baadhi ya nchi, unaweza kupata antibiotics bila maelezo ya daktari, jambo ambalo huongeza uwezekano wa matumizi mabaya. Sababu zote hizi huchangia bakteria kuwa sugu kwa dawa zilizokuwa zikiwaua hapo awali.

Wakati gani wa kutumia antibiotiki na wakati gani hupaswi?

Katika kilimo, dawa za antibiotic hunyunyizwakwenye matunda bustani ili kuzuia wadudu, au hulishwa kwa wanyama katika uzalishaji mkubwa wa nyama. Kwa njia hii, antibiotics huingia kwenye maji yetu na chakula chetu.

Viwango vya antibiotics wanavyokutana navyo bakteria havitoshi kuwaua, na badala yake hufanya kazi kama nyenzo za mafunzo: Bakteria hujifunza kutoka kwao na kubadilika ili kuwa sugu.

Soma pia:Dawa za kusisimua misuli: Paul Pogba asimamishwa kwa muda

Kwa mujibu wa shirika la afya duniani, WHO, idadi ya maambukizi yanayosababishwa na bakteria wasiosikia dawa imeongezeka kwa asilimia 15 kutoka mwaka 2017 hadi 2021.

Bakteria wanaosababisha maambukizzi kwenye njia ya mkojo wanazidi kuwa sugu pia. Kifua kikuu pia kinazidi kuwa kigumu kutibu kwa sababu ya usugu wa dawa.

Watafiti kutoka nchini Ujerumani na Msumbiji waligundua kuwa  kuna vimelea vya kifua kikuu vinavyosambaa nchini Msumbiji ambavyo haviskii dawa, ambazo WHO inazipendekeza kwa matibabu.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa4 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa1 month ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa2 months ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa1 day ago

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 days ago

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi

Ugonjwa unaosababishwa na kula nyama mbichi Madhara ya kula nyama ya ng’ombe mbichi Ni desturi ya baadhi ya watu kula...

Magonjwa1 week ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa1 week ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa3 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa3 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa4 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...