Connect with us

Dawa

Dawa ya Pregabalin inatibu nini na kwa nini inaweza kuwa hatari?

Published

on

Dawa ya Pregabalin inatibu nini na kwa nini inaweza kuwa hatari?

Dawa ya pregabalin inahusishwa na vifo duniani kote. Watumiaji hununua dawa hiyo, mara nyingi kutoka katika tovuti zisizo rasmi.

Pregabalin ni nini na inatumikaje?

Dawa ya pregabalin hutumiwa kutibu magonjwa ikiwa ni pamoja na kifafa, maumivu ya neva na wasiwasi.

Inatengenezwa kama vidonge au maji, na inaweza kuitwa Alzain, Axalid, Lyrica au Signature, kulingana na mtengenezaji.

Je,Dawa ya Pregabalin ina madhara gani?

Wengine huiita Valium au Bud (Budweiser) kwa sababu inaweza kuwafanya watumiaji wahisi wametulia, kwa njia sawa na dawa za kutuliza au pombe.

Kuitumia kupita kiasi – haswa ikichanganywa na dawa nyingine za mitaani ambazo pia zina athari – kunaweza kusababisha kusinzia pamoja na shida ya kupumua.

Wagonjwa ambao wameagizwa kutumia pregabalin wanashauriwa kuepuka unywaji wa pombe.

Utegemezi wa pregabalin ni hatari hasa kwa wale walio na historia ya awali ya matumizi mabaya ya dawa za kulevya au uraibu.

Baadhi ya watu hupata ugumu kuacha kutumia pregabalin. Ukitaka kuachana na uraibu wa dawa hii unaweza kupata mabadiliko ya hisia kama vile hasira na kuwashwa, wasiwasi na woga pamoja na dalili za kimwili kama vile kutokwa na jasho, kichefuchefu na baridi.

Historia ya dawa hii ya Pregabalin

Pregabalin ilianzishwa nchini Marekani na Uingereza mwaka 1993.

Yeyote anayejaribu kuacha kutumia dawa hiyo anapaswa kutafuta ushauri wa kiafya kwanza.

Hupaswi kuacha ghafla kutumia pregabalin isipokuwa uache baada ya ushauri wa daktari. Dozi hupunguzwa kwa wiki moja au zaidi.

Katika nchi kadhaa, ikiwa ni pamoja na Uingereza kumiliki dawa hii bila sababu halali ya kimatibabu ni kosa la jinai.

Hata hivyo dawa hiyo inauzwa katika maduka ya dawa katika nchi kadhaa za Mashariki ya Kati, na pia katika majimbo mengi nchini India.

Utafiti uliochapishwa na jarida la matibabu la Nature Communications unakadiria kuwa idadi ya dozi za pregabalin zinazotumika kila siku duniani kote iliongezeka zaidi ya mara nne kati ya 2008 na 2018.

Zaidi ya maagizo milioni nane ya pregabalin yalitolewa nchini Uingereza mwaka wa 2022. Mwaka huo, kulikuwa na vifo 441 vilivyoripotiwa kuhusiana na dawa hiyo nchini Uingereza na Wales.

Mwaka 2023, ripoti ya Kila mwaka ya Overdose ya Australia iligundua vifo 887 vilivyohusishwa na pregabalin kati ya 2000 na 2021 – 93% vinahusishwa na pregabalin.

Rekodi kutoka Uingereza zinaonyesha vifo vingi kati ya 2004 na 2020 vinavyohusishwa na pregabalin vilitokea wakati ilipotumika pamoja na dawa nyingine kama vile methadone au morphine.

Matumizi ya pregabalin na gabapentin nchini Serbia yaliongezeka kwa 60% kila mwaka kati ya 2008 na 2018.

Kulingana na data kutoka Kituo chake cha Kitaifa cha Kudhibiti Sumu, watu 374 walikuwa na sumu kali kutokana na dawa hizi kati ya 2012 na 2022. Kati ya 96% walikuwa wametumia pregabalin.

Ripoti rasmi zinaonyesha kuwa dawa hiyo pia inazidi kutumiwa nchini Saudi Arabia na Jordan, hasa na vijana wa kiume.

Mwaka 2017, Kituo cha Kitaifa cha Kurekebisha Tabia cha Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kilisema pregabalin na gabapentin ndizo dawa zinazotumiwa vibaya zaidi na walio na umri wa chini ya miaka 30.

Mwezi Machi, tembe milioni 2.75 zilinaswa kutoka genge la wasafirishaji huko UAE.

Mwaka 2023, mamlaka nchini Kuwait ilikamata vidonge milioni 15 vya pregabalin na nusu ya tani ya dawa hiyo ikiwa katika hali ya unga.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Afyaclass Social Ask

Kuna aina mbili za vidonge vya majira ni zipi?

Published

on

Ndiyo, vidonge vya uzazi wa mpango (vinavyojulikana pia kama “vidonge vya majira”) kwa ujumla vimegawanyika katika aina mbili kuu:

1.Vidonge vyenye homoni mbili (Combined Oral Contraceptive Pills)

  • Vinakuwa na homoni za estrogen na progestin.
  • Hunywewa kila siku kwa mpangilio maalum.

2.Vidonge vyenye homoni moja (Progestin-Only Pills – POPs au Mini Pills)

  • Vinakuwa na homoni ya progestin pekee.
  • Mara nyingi hupendekezwa kwa baadhi ya wanawake, ikiwemo wanaonyonyesha.

Ni muhimu kutumia aina inayokufaa baada ya ushauri wa mtaalamu wa afya, kwani uchaguzi hutegemea umri, historia ya afya, na hali nyingine za kiafya.

KUMBUKA:Kwa wanawake wanaonyonyesha, vidonge vya homoni moja (Progestin-Only Pills/Mini Pills) vinaweza kusababisha mabadiliko ya hedhi, ikiwemo:

  • Damu kutoka kidogo-kidogo bila mpangilio.
  • Hedhi kuwa nyepesi sana.
  • Hedhi kutokuwepo kabisa kwa muda (amenorrhea).

Hii hutokea kwa baadhi ya watumiaji na mara nyingi si ishara ya tatizo kubwa. Kwa kweli, kutopata hedhi wakati wa kunyonyesha pia kunaweza kuchangiwa na homoni zinazozalishwa wakati wa kunyonyesha.

Ikiwa damu imekatika ghafla, una wasiwasi wa ujauzito, au kuna dalili nyingine zisizo za kawaida, ni vyema kufanya kipimo cha ujauzito na kuwasiliana na mtoa huduma wa afya.

Continue Reading

Dawa

Madhara ya p2 kwa mwanamke

Published

on

Madhara ya p2 kwa mwanamke 

Fahamu P2 ni dawa ya dharura yaani kwa kitaalam hujulikana kama emergency contraceptive pill, dawa hii inazuia mtu asipate Mimba kwenye mazingira ambayo umefanya mapenzi pasipo kupanga na upo siku za hatari,au umelazimishwa kufanya mapenzi au umebakwa,ili kuzuia mimba zisizotarajiwa unalazima Kunywa hizi dawa.

Ukweli ni kwamba dose ya hormones ndani ya p2 ni kubwa kuliko vidonge vya kawaida vya Uzazi(birth control pills) kitu ambacho kinaifanya isifae kwa Matumizi ya kila siku,

Hii husababisha madhara Zaidi kwa Mtu mwenye mazoea ya kuzitumia mara kwa mara. Na moja ya madhara ni mzunguko wako wa hedhi kuathiriwa sana – Periods yako inaweza isitoke kama kawaida, inaweza kuwa nyingi,zito sana,isiyoeleweka(Irregular bleeding) n.k.

Pia baadhi ya Wanawake huongezeka uzito, Hivo basi P2 haishauriwi kabsa kwa matumizi ya kila siku au kutumia kama njia ya uzazi wa mpango ya muda mrefu.

Madhara baada ya kutumia p2,

Haya ni baadhi ya Madhara au matokeo baada ya kutumia p2(emergency contraceptive pills):

  • Kupata kichefuchefu
  • Kutapika
  • Mwili kuchoka Sana
  • Kupata kizunguzungu
  • Kupata maumivu ya kichwa
  • Kupata maunivu ya tumbo
  • Maziwa kuuma au kuvuta zaidi
  • Kubadilika kwa hedhi yako ya kawaida,ikiwemo kuvuja damu nyingi au kwa muda mrefu,au kuvuja katikati ya mzunguko n.k

Kutokwa na Vitone vya damu mara kwa mara(spotting) – Unaweza kupata vitone vya damu ndani ya wiki ijayo baada ya kumeza kidonge cha dharura cha kuzuia mimba yaani P2,

Pia, hedhi yako inayofuata inaweza kuwa nyepesi au nzito, ikawahi kutoka mapema au kuchelewa kuliko kawaida. Hakikisha unapata Msaada wa Tiba ikiwa unakutana na changamoto hizi.

Mzunguko wa hedhi usio wa kawaida(Irregular menstrual cycle) – Kwa sababu ya tembe za dharura za kuzuia mimba(p2), kipindi chako cha hedhi kinaweza kufika mapema au kuchelewa, jambo ambalo hutokea sana kwa wanawake wanaotumia vidonge hivi. Hata hivyo, unapaswa kufanya kipimo cha ujauzito ikiwa hupati kipindi chako cha hedhi ndani ya wiki mbili za tarehe inayotarajiwa.

MADHARA YA KUTUMIA P2

P2 Ni Dawa iliyotengenezwa kutumiwa mara chache tu,inapokulazimu.Sio dawa unayotakiwa kutumia kama njia ya uzazi wa mpango ya muda mrefu. Kuna wanawake humeza p2 kila mwezi,hii haitakiwi. Katika mazingira ya kawaida,haipaswi kumezwa zaidi ya mara 3 kwa mwaka. Kuendekeza kila mwezi kunywa hizi p2 sio sahihi,Unatakiwa ende hospitali ili upate njia sahihi ya uzazi wa mpango ya muda mrefu.

Baadhi ya Side effects/madhara ni ya matumizi holela ya dawa hizi ni

1.Unaweza kujisikia kichefuchefu au kutapika baada ya kumeza,

2.Maumivu ya tumbo

3.Matiti kuuma na kujaa

4.Pia hedhi zako zinazofuata zinaweza zikawahi au zikachelewa au zikatoka nyingi sana( ukiona zimezidi siku 8 fika muone daktari) au ukawa unapata hedhi nyepesi sana,au pia haupati hedhi kabisa (amenorhoea)

5.Kichwa kuuma na kizunguzungu

6.Mabadiliko ya Ute ukeni (change in cervical secretion,hapa unakuta Ute wa ovulation mtu hapati).

7.Kupata maambukizi ukeni,vaginal infections

8.Hatari ya kupata PID

9.Maumivu wakati wa sex(dyspareunia)

10.Mama anakuwa hatarini kutungisha mimba nje ya kizazi yaani ectopic pregnancy.

11.Lakini pia kuna wanawake hupata Ovarian cyst,vivimbe kwenye mfuko wa mayai.

Kuna sababu hapo juu kama PID,kutopata UTE,infections kwenye uke hizi zinakuja athiri mwanamke anakuwa anapata taabu kwenye Kupata mimba

Kama hujapanga kupata mimba,tafadhari fuata njia ya uzazi wa mpango ya muda mrefu inayokufaa,achana na kumeza p2 kila mwezi.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Soma Zaidi;

Vyanzo:
https://www.who.int/news-room/fact-sheets/detail/emergency-contraception
https://www.mayoclinic.org/tests-procedures/morning-after-pill/about/pac-20394730
https://my.clevelandclinic.org/health/treatments/23386-morning-after-pill
Continue Reading

Dawa

Matumizi sahihi ya p2,Fahamu hapa

Published

on

Matumizi sahihi ya p2

Vidonge vya dharura vya kuzuia mimba (emergency contraceptives), vinavyojulikana pia kama P2, hutumika kusaidia kuzuia ujauzito baada ya kufanya ngono bila kinga au kama kinga imeharibika.

Aina zinazotumika sana zina dawa ya Levonorgestrel.

Matumizi sahihi ya p2

Jinsi ya kutumia kwa Usahihi Vidonge vya P2

-Meza kidonge haraka iwezekanavyo baada ya tendo la ngono bila kinga.

Hufanya kazi vizuri zaidi ndani ya saa 24.

Kinaweza kutumika hadi saa 72 (siku 3), na baadhi ya aina hadi siku 5 lakini ufanisi hupungua kadri muda unavyoongezeka.

Muhimu kufahamu:

-Hakizuizi mimba iliyokwisha kutungwa tayari.

-Si dawa ya kutoa mimba.

-Hakikingi dhidi ya magonjwa ya zinaa.

-Si vizuri kutumia mara kwa mara kama njia kuu ya uzazi wa mpango; ni kwa dharura.

Madhara yanayoweza kutokea

  • Kichefuchefu
  • Maumivu ya kichwa
  • Uchovu
  • Kutokwa damu kidogo
  • Hedhi kuwahi au kuchelewa kwa siku chache

Wakati wa kufanya kipimo cha mimba

Ikiwa hedhi imechelewa zaidi ya wiki moja baada ya muda uliotarajiwa, ni vizuri kufanya pregnancy test.

Madhara ya p2,haya ni madhara ya matumizi ya Vidonge vya P2

Madhara baada ya kutumia p2,Fahamu hapa

Fahamu P2 ni dawa ya dharura yaani kwa kitaalam hujulikana kama emergency contraceptive pill, dawa hii inazuia mtu asipate Mimba kwenye mazingira ambayo umefanya mapenzi pasipo kupanga na upo siku za hatari,au umelazimishwa kufanya mapenzi au umebakwa,ili kuzuia mimba zisizotarajiwa unalazima Kunywa hizi dawa.

Ukweli ni kwamba dose ya hormones ndani ya p2 ni kubwa kuliko vidonge vya kawaida vya Uzazi(birth control pills) kitu ambacho kinaifanya isifae kwa Matumizi ya kila siku,

Hii husababisha madhara Zaidi kwa Mtu mwenye mazoea ya kuzitumia mara kwa mara. Na moja ya madhara ni mzunguko wako wa hedhi kuathiriwa sana – Periods yako inaweza isitoke kama kawaida, inaweza kuwa nyingi,zito sana,isiyoeleweka(Irregular bleeding) n.k.

Pia baadhi ya Wanawake huongezeka uzito, Hivo basi P2 haishauriwi kabsa kwa matumizi ya kila siku au kutumia kama njia ya uzazi wa mpango ya muda mrefu.

Madhara baada ya kutumia p2,

Haya ni baadhi ya Madhara au matokeo baada ya kutumia p2(emergency contraceptive pills):

  • Kupata kichefuchefu
  • Kutapika
  • Mwili kuchoka Sana
  • Kupata kizunguzungu
  • Kupata maumivu ya kichwa
  • Kupata maunivu ya tumbo
  • Maziwa kuuma au kuvuta zaidi
  • Kubadilika kwa hedhi yako ya kawaida,ikiwemo kuvuja damu nyingi au kwa muda mrefu,au kuvuja katikati ya mzunguko n.k

Kutokwa na Vitone vya damu mara kwa mara(spotting) – Unaweza kupata vitone vya damu ndani ya wiki ijayo baada ya kumeza kidonge cha dharura cha kuzuia mimba yaani P2,

Pia, hedhi yako inayofuata inaweza kuwa nyepesi au nzito, ikawahi kutoka mapema au kuchelewa kuliko kawaida. Hakikisha unapata Msaada wa Tiba ikiwa unakutana na changamoto hizi.

Mzunguko wa hedhi usio wa kawaida(Irregular menstrual cycle) – Kwa sababu ya tembe za dharura za kuzuia mimba(p2), kipindi chako cha hedhi kinaweza kufika mapema au kuchelewa, jambo ambalo hutokea sana kwa wanawake wanaotumia vidonge hivi. Hata hivyo, unapaswa kufanya kipimo cha ujauzito ikiwa hupati kipindi chako cha hedhi ndani ya wiki mbili za tarehe inayotarajiwa.

Rejea Zaidi hapa:

Continue Reading

Trending

Copyright © 2017 Zox News Theme. Theme by MVP Themes, powered by WordPress.