Connect with us

magonjwa ya wanawake

Fibroids ni ugonjwa gani, Fibroids ni nini

Avatar photo

Published

on

Fibroids ni ugonjwa gani

Fibroids, ambapo pia huitwa myoma, ni uvimbe usio wa saratani (benign) unaokua katika au kwenye kuta za kizazi (uterus) cha mwanamke,

Hivo basi, Fibroids ni uvimbe unaoweza kutokea kwenye Kizazi lakini sio Saratani.

Uvimbe huu unaweza kuwa wa ukubwa tofauti, kutoka kwa udogo usioonekana kwa macho hadi kwa ukubwa unaoweza kusababisha kizazi kubadilika umbo na ukubwa.

Chanzo cha Fibroids

Chanzo halisi cha fibroids hakijulikani, lakini kuna visababishi kadhaa vinavyohusishwa na ukuaji wa fibroids, ikiwa ni pamoja na:

– Mabadiliko ya homoni:

Homoni za estrogen na progesterone, zinazochochea ukuta wa kizazi kukua kila mwezi kama sehemu ya mzunguko wa hedhi, pia zinaaminika kuchochea ukuaji wa fibroids.

– Sababu za kijenetiki:

Fibroids inaweza kurithiwa katika familia.

– Sababu zingine:

Kama vile uzito wa mwili ulio juu(kuwa na uzito mkubwa/overweight), upungufu wa vitamini D, na matumizi ya pombe, pia yamehusishwa na ukuaji wa fibroids.

Dalili za Fibroids

Baadhi ya wanawake wenye fibroids hawapati dalili zozote, huku wengine wakikumbwa na dalili zifuatazo:

  • Kupata Menstruation au damu ya hedhi nzito au kwa muda mrefu zaidi ya kawaida
  • Kupata Maumivu,shinikizo au hali ya mkazo katika pelvis
  • Kupata Maumivu wakati wa kujamiiana
  • Kukojoa Mara kwa mara au kupata hisia za haraka za kukojoa
  • Kupata choo kigumu au kukosa choo Constipation
  • Kupata Maumivu ya miguu
  • au kupata maumivu chini ya mgongo n.k

Hakikisha unawahi hospital ikiwa unapata dalili hizi;(See your doctor if you have:)

1. Maumivu ya Pelvic hayaishi licha ya kutumia dawa za kuyatuliza

2. Unapata damu ya Hedhi nzito au maumivu makali ambayo hukusababisha hata ushindwe kufanya chochote

3. Unapata damu vitone vitone kila mara au unapata hedhi katikati ya mwezi

4. Ukikojoa mkojo haushi

5. Unapata uchovu ambao hauishi, na mwili kuwa dhaifu au kukosa nguvu kabsa,

dalili hizi huweza kuashiria pia tatizo lingine la Upungufu wa damu(anemia) ambalo unaweza kuwa nalo kutokana na kuvuja damu nyingi na kwa muda mrefu.

Madhara ya Fibroids(Complications)

Mara nyingi Tatizo la Uterine fibroids sio hatari sana kwa afya yako. Ingawa huweza kuleta maumivu na kusababisha madhara zaidi hasa usipopata matibabu.

Moja ya madhara ni kusababisha shida ya kushuka kwa seli nyekundu za damu(Red blood cells-RBCs) au kusababisha tatizo la Upungufu wa damu(anemia)

Hali hiyo inaweza kusababisha uchovu kutokana na kupoteza damu nyingi. Ikiwa unavuja damu nyingi wakati wa kipindi chako cha Hedhi, daktari wako anaweza kukuambia kuhusu kupata zaidi madini chuma(iron supplement) ili kuzuia au kusaidia kudhibiti upungufu wa damu mwilini. Wakati mwingine, mtu mwenye upungufu wa damu anahitaji kupewa damu kutoka kwa watu wengine(Blood transfusion), kutokana na kupoteza damu nyingi.

Utambuzi wa Fibroids

Fibroids mara nyingi hugundulika wakati wa uchunguzi wa kawaida wa pelvic. Vipimo vya ziada kama ultrasound ya pelvic, MRI, na aina nyingine za uchunguzi zinaweza kufanywa kuthibitisha uwepo na ukubwa wa fibroids.

Matibabu ya Fibroids

Matibabu ya fibroids hutegemea ukubwa wa fibroids, dalili, umri, afya ya jumla ya mwanamke, na kama anataka kuzaa siku za usoni.n.k

Matibabu yanaweza kujumuisha:

âś“ Udhibiti wa dalili: Dawa za kutuliza maumivu na dawa za homoni kudhibiti dalili zingine huweza kutumika

âś“ Njia za upasuaji: Kama vile myomectomy kwa kuondoa fibroids, au hysterectomy kwa kuondoa kizazi kizima (chaguo la mwisho, hasa kwa wanawake ambao hawataki kuzaa tena).

âś“ Tiba zisizo za upasuaji: Kama vile utaratibu wa embolization ya artery ndani ya kizazi au uterine, ambayo inapunguza damu inayotiririka kwenye fibroid, na kusababisha ipungue ukubwa.n.k

Kwa wanawake wengi, fibroids si hatari na zinaweza kudhibitiwa na matibabu yanayolenga kupunguza dalili.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

YOU MUST READ(IMPORTANT)

Magonjwa3 weeks ago

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani

Maumivu chini ya kitovu ni dalili za ugonjwa gani. Watu wengi huweza kupata maumivu chini ya kitovu, lakini umewahi kujiuliza...

Magonjwa4 weeks ago

Kaswende ni ugonjwa gani, soma hapa kufahamu

Kaswende ni ugonjwa gani, Kaswende ni maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Mara nyingi, huenea kupitia mawasiliano ya kingono au kwa kujamiiana....

Magonjwa1 month ago

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani

Koo kukauka ni dalili ya ugonjwa gani Koo kukauka kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na: Upungufu wa...

Magonjwa2 months ago

Amiba ni ugonjwa gani,Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Amebiasis

Amiba ni ugonjwa gani Wengi wamezoea kusema hivo ila Amiba(amoeba) ni vimelea vyinavyosababisha ugonjwa, na Ugonjwa huo kitaalam ndyo hujulikana...

Magonjwa3 months ago

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba

kuwashwa nyayo za miguu husababishwa na nini? chanzo na Tiba kuwashwa nyayo za miguu; zipo sababu nyingi ambazo huchangia shida...

magonjwa ya wanawake4 months ago

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease)

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) Pid ni ugonjwa gani? PID ni Maambukizi ya bacteria Kwenye Via vya Uzazi...

Magonjwa2 years ago

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE)

SHINGO YA MTOTO KULEGEA(CHANZO CHAKE) Mabadiliko ya Watoto wengi huanza kwenye miezi mitatu ya Mwanzo wakati ambapo Shingo ya mtoto...

Magonjwa3 years ago

MAUMIVU MAKALI SEHEMU YA HAJA KUBWA

Baadhi ya watu wanachanganya tatizo la maumivu makali sehemu ya haja kubwa pamoja na tatizo la Bawasiri,japo mojawapo ya chanzo...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus)

TATIZO LA MASIKIO KUPIGA KELELE,CHANZO NA TIBA YAKE(Tinnitus) tatizo la masikio kupiga kelele Tinnitus, ni Tatizo la masikio kupiga kelele,...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO)

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?)

Tatizo la Uke Kujamba TATIZO LA UKE KUJAMBA PAMOJA NA TIBA YAKE(chanzo cha tatizo hili ni nini?) Moja ya vitu...

Magonjwa3 years ago

DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

 FANGASI • • • • • DALILI ZA FANGASI UUMENI,KORODANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE Mashambulizi ya Fangasi sehemu za siri...

Magonjwa3 years ago

CHANZO CHA TATIZO LA KUOTA NYAMA PUANI PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Chanzo cha tatizo la NYAMA PUANI,Dalili zake Pamoja na Tiba yake, Soma makala hii kwa Makini ili upate Kujua kuhusu...

Magonjwa3 years ago

SABABU ZA KUVIMBA KWA MASHAVU YA UKE(TEZI LA BARTHOLIN)

KUVIMBA MASHAVU YA UKE • • • • • • Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu sababu za kuvimba mashavu...

Magonjwa3 years ago

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia) Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama...

MAGONJWA MBALI MBALI

Magonjwa4 days ago

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani

Mkojo kuuma ni dalili ya ugonjwa gani Mkojo kuuma au kupata maumivu wakati wa kukojoa ni hali ambayo kwa kitaalam...

Magonjwa5 days ago

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono dalili Zake

 UGONJWA WA KISONONO DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa...

Magonjwa2 weeks ago

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu

Maana ya hiv negative,Soma hapa kufahamu Haya ni maneno ambayo umekuwa ukiyasikia sana linapokuja swala la vipimo cha UKIMWI, je...

Magonjwa2 weeks ago

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia

Kama ndiyo Umegunduliwa ugonjwa wa Kisukari,Soma hii itakusaidia. Kutana na Ilene Raymond Rush ambaye aligunduliwa Kisukari aina ya Pili(Type 2...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa unaosababishwa na konokono

Ugonjwa unaosababishwa na konokono Ugonjwa unaosababishwa na konokono unaitwa schistosomiasis, au bilharzia. Ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na minyoo wanaoitwa...

Magonjwa2 weeks ago

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake

Ugonjwa wa Pink Eye,chanzo,dalili na Matibabu yake. Wengi tumesikia kuhusu Red Eyes(Macho mekundu) Lakini je umewahi kusikia kuhusu Pink Eyes,?...

Magonjwa3 weeks ago

Omeprazole inatibu ugonjwa gani,Fahamu hapa

Omeprazole inatibu ugonjwa gani Omeprazole inatibu ni nini?, Hili ni swali ambalo limekuwa likiulizwa mara kwa mara na wafwatiliaji wengi...

Magonjwa3 weeks ago

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani

Mate kujaa mdomoni ni dalili ya ugonjwa gani Mate kujaa Mdomoni,ni tatizo ambalo hutokea kwa baadhi ya watu, na zipo...

Magonjwa3 weeks ago

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho

Glaucoma: Ugonjwa hatari unaopoteza nuru ya macho Kuna magonjwa mengi yanayohusiana na macho, mengi yanatibika lakini kuna baadhi ya magonjwa...

Magonjwa4 weeks ago

Kunguni husababisha ugonjwa gani

Kunguni husababisha ugonjwa gani Kunguni ni wadudu wadogo ambao chakula chao kikubwa ni damu, wadudu hawa huweza kunyonya damu kutoka...